ASIYEFANYA KAZI NA ASILE

ASIYEFANYA KAZI NA ASILE

Biblia ina maanisha nini iliposema “Asiyefanya kazi na asile”?

Maandiko hayo yanapatikana kutoka katika kitabu cha 2 Wathesalonike 3:10 “Kwa kuwa hata wakati ule tulipokuwapo kwenu tuliwaagiza neno hili, kwamba ikiwa mtu hataki kufanya kazi, basi, asile chakula”.

Mstari huo unatafsiriwa isivyopaswa na wengi wanaousoma..

Lakini mstari huo, unawahusu Wakristo! yaani watu wanaokusanyika  pamoja kanisani.

Katika Kanisa la Kwanza ulikuwepo utaratibu wa Waumini wote kufanya vitu kwa shirika,  ikiwemo kila mmoja kutoa sehemu ya mali zake na kuzileta kanisani ili zitumike katika kusaidiana pamoja na kunyanyuana..hususani kwa wale wenye mahitaji…. Hilo tunalisoma katika kitabu cha Matendo ya Mitume 2

Matendo 2:44 “Na wote walioamini walikuwa mahali pamoja, na kuwa na vitu vyote shirika,

45 wakiuza mali zao, na vitu vyao walivyokuwa navyo, na kuwagawia watu wote kama kila mtu alivyokuwa na haja.

46 Na siku zote kwa moyo mmoja walidumu ndani ya hekalu, wakimega mkate nyumba kwa nyumba, na kushiriki chakula chao kwa furaha na kwa moyo mweupe,

47 wakimsifu Mungu, na kuwapendeza watu wote. Bwana akalizidisha kanisa kila siku kwa wale waliokuwa wakiokolewa”.

Sasa kilichokuwa kinatokea ni kwamba, kulikuwepo na watu wachache ambao, walikuwa na uwezo wa kwenda kufanya kazi, lakini kwasababu wanaona kuna ofa hiyo ya kugawiwa baadhi ya vitu bure ikiwemo chakula kanisani, wakawa hawaendi kufanya kazi, na kukaa kusubiria hilo fungu la kanisa lifike wapewe, hivyo hiyo ikawa inasababisha kanisa kulemewa, kwa kuongezeka kwa watu wasio na shughuli zao na huku bado wanataka kupewa fungu kutoka kanisani.

Sasa kulitatua tatizo hilo, Ndipo Mtume Paulo kwa Uwezo wa Roho akaagiza katika makanisa yote kwamba watu wakafanye kazi, wale chakula chao wenyewe ili kanisa lisilemewe…Wabakie tu wale wanaostahili kweli kweli kupata fungu kutoka kanisani…Na wengi wa hao wanaostahili walikuwa ni wajane wenye umri wa miaka 60 na kuendelea, tena wasio na ndugu wa kuwasaidia, wameachwa wenyewe, na pia wana rekodi nzuri ya kuifanya kazi ya Mungu kanisani…hao ndio waliostahili kupokea sehemu ya fungu… na watu wasio na uwezo kabisa..Lakini wengine waliosalia wasipewe kitu chochote hata chakula kutoka kanisani, wakafanye kazi ili kanisa lisilemewe.


Mada Nyinginezo:

TOFAUTI KATI YA NDOTO NA MAONO NI IPI?

TUNAPOSEMA TUISHI KWA NENO, INAMAANISHA TUISHI MAISHA YA NAMNA GANI?

FUATILIA NDOTO HII, UTAJIFUZA KITU.

JE! KUBET NI DHAMBI?


Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments