Mikono iliyotakata ni mikono ya namna gani? (1Timotheo 2:8).

Mikono iliyotakata ni mikono ya namna gani? (1Timotheo 2:8).

Swali: Katika 1Timotheo 2:8 tunaona Mtume Paulo akiwataja wanaume kuwa wanaposalisha wanyanyue mikono iliyotakata, sasa hii mikono iliyotakata ndio mikono ya namna gani?

Jibu: Tusome,

1Timotheo 2:8  “Basi, nataka wanaume wasalishe kila mahali, huku wakiinua mikono iliyotakata pasipo hasira wala majadiliano”

Mikono iliyotakata ni mikono isiyo na “Dosari”..Sasa ili tuelewe mikono isiyo na Dosari ni mikono ya namna gani, hebu tuangalie mikono yenye Dosari ni ipi. Tusome Isaya 1:15-17.

Isaya 1:15 “Nanyi mkunjuapo mikono yenu, nitaficha macho yangu nisiwaone; naam, mwombapo maombi mengi, sitasikia; mikono yenu imejaa damu. 

16 Jiosheni, jitakaseni; ondoeni uovu wa matendo yenu usiwe mbele za macho yangu; acheni kutenda mabaya;

 17 jifunzeni kutenda mema; takeni hukumu na haki; wasaidieni walioonewa; mpatieni yatima haki yake; mteteeni mjane”.

Umeona Mikono yenye dosari ni ipi?.. Ni ile inayomwaga damu, inayoonea wanyonge, inayokula rushwa, mikono inayoabudu sanamu…kwaufupi mwenye dhambi yoyote Yule mikono yake ni michafu, na ina dosari mbele za Mungu.

Kwahiyo tukirudi kwenye biblia hapo maandiko yanaposema kuwa “..wanaume wasalishe kila mahali, huku wakiinua mikono iliyotakata..” imemaanisha kuwa wawapo katika ibada, au kanisani wakiabudu au kuomba, au kumtolea Mungu wahakikishe mikono yao haina hila..sio watu wa kumwaga damu, sio watu wa kula rushwa, sio watu wa kuonea watu n.k Soma pia Zaburi 58:1. Isaya 37:1 na Isaya 59:3, utaona jambo hilo hilo.

Hivyo huo ni ujumbe kwetu wote, kwamba tuitakase mikono yetu.. sio tunakwenda kumfanyia Mungu ibada au kumtolea matoleo na huku mikono yetu ni michafu..Bwana hatazitakabari sadaka zetu kama alivyozikataa zile za Kaini, vile vile tunaponyosha mikono yetu ambayo ina visasi, au ina vinyongo, au ina rushwa, na kumwabudu Mungu kwayo, kibiblia ni machukizo mbele zake.

Yakobo 4:8 “Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi. ITAKASENI MIKONO YENU, enyi wenye dhambi, na kuisafisha mioyo yenu, enyi wenye nia mbili”.

Je umempokea Yesu katika maisha yako?.. Fahamu kuwa Yesu ndiye Njia, Kweli na Uzima.. wala hakuna mtu atakamwona Mungu, pasipo kupitia kwake yeye. Hivyo tubu leo kwa kumaanisha kuziacha dhambi zako na tafuta ubatizo sahihi ambao ni wa maji mengi (Yohana 2:23) na kwa jina la Bwana Yesu Kristo (Matendo 2:38), na Roho Mtakatifu atakuongoza na kukutia katika kweli yote sawasawa na ahadi yake (Yohana 16:13).

Marana atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Biblia inapotumia neno “Bila kazi ya mikono”, ina maana gani?

MIKONO YENU IMEJAA DAMU.

UTAKAPOKUWA MZEE, UTAINYOSHA MIKONO YAKO. NA MWINGINE ATAKUFUNGA

USIZISHIRIKI DHAMBI ZA WATU WENGINE.

FAHAMU JINSI MUNGU NA SHETANI WANAVYOZUNGUMZA NA WATU.

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments