TUSIIFUATISHE KAWAIDA YA ULIMWENGU HUU.

TUSIIFUATISHE KAWAIDA YA ULIMWENGU HUU.

Bwana Yesu atukuzwe daima. Karibu tena tuyasogelee maneno matukufu ya Mungu wetu Yehova; 

Maandiko yanasema hivi; 

Waefeso 2:1-2

[1]Nanyi mlikuwa wafu kwa sababu ya makosa na dhambi zenu;

[2]ambazo mliziendea zamani KWA KUIFUATA KAWAIDA YA ULIMWENGU HUU, na kwa kumfuata mfalme wa uwezo wa anga, roho yule atendaye kazi sasa katika wana wa kuasi;

Kumbe hii dunia ina “kawaida yake”..yaani kwa ufupi ina desturi yake ambayo imeshajizoesha tangu enzi na enzi, tangu Adamu alipoasi hata sasa, kuendana nayo.

Kwamfano leo ukienda nchi nyingi za magharibi au Asia kama vile Japan na Nepal, utakuta wanaume na wanawake sehemu za umma wanashea vyoo . Tofauti na huku kwetu, jambo hilo halikubaliwi kabisa na ni ajabu sana ukikutwa mtu unatumia choo cha jinsia tofauti.

Hivyo huku kwetu ni jambo lisilo na heshima lakini kwao ni “la kawaida”..ndio desturi yao.

Mataifa mengine kama Jamaika kuvuta bangi, ni haki kisheria lakini kwetu sisi, ni kosa..kwao ni “kawaida” kwetu sisi ni kosa la jinai..

Vivyo hivyo na hii dunia ina kawaida yake ambayo inakinzana na kanuni za ufalme wa mbinguni, Na sisi kama wakristo hatupaswi kuiiga, hata kidogo…japokuwa tutaonekana ni watu wa ajabu sana, kama mtume Petro alivyosema katika;

1 Petro 4:3-5

[3]Maana wakati wa maisha yetu uliopita watosha kwa kutenda mapenzi ya Mataifa; kuenenda katika ufisadi, na tamaa, na ulevi, na karamu za ulafi, na vileo, na ibada ya sanamu isiyo halali;

[4]MAMBO AMBAYO WAO HUONA KUWA NI AJABU YA NINYI KUTOKWENDA MBIO PAMOJA NAO katika ufisadi ule ule usio na kiasi, wakiwatukana.

[5]Nao watatoa hesabu kwake yeye aliye tayari kuwahukumu walio hai na waliokufa.

Mwanamke mmoja alinifuata na kuniambia mwanaume kama huna mojawapo ya starehe hizi yaani; 1) Ushabiki wa mpira, 2) wanawake,  3) pombe.. Wewe sio mwanaume kamili, una mapungufu. Nikasema ni kweli kwasababu kawaida ya ulimwengu huu, inalazimisha watu wawe na tabia hizo.

Binti unaambiwa usipokuwa na boyfriend, usipotumia kidogo mkorogo, usipovaa visuruali na visketi vifupi vifupi utaitwa mama/mbibi.. Wala usishangae kwasababu kawaida ya ulimwengu huu ni lazima utaonekana hivyo.

Lakini sisi kama wapitaji, makao yetu yaliyo mbinguni wala sio hapa duniani, hatuna ruhusu ya kuifuata, haijalishi itaonekana ni njema mbele ya dunia nzima..Sisi tunaifuata ‘kawaida ya mbinguni’..ambayo inatufundisha kuishi maisha ya utakatifu na usafi, kama Mungu mwenyewe na malaika zake walivyo watakatifu.

Hatuna desturi ya kuzini kabla ya ndoa, hatuna desturi ya kutembea na vimini, na mavazi ya utupu barabarani, hatuna ruhusa ya kuzifurahia anasa za ulimwengu huu, miziki, disco, kamari, pombe.

Warumi 12:2

[2]WALA MSIIFUATISHE NAMNA YA DUNIA HII; bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu, mpate kujua hakika mapenzi ya Mungu yaliyo mema, ya kumpendeza, na ukamilifu.

Hivyo ndugu uliyeokoka, kamwe usitake kumpendeza mtu, ukafaraka na Mungu. Mambo mengi ya ulimwengu huu yamefaraka na Mungu..Huo ndio ukweli, Ukiupenda ulimwengu ukasema unampenda na Mungu pia hapo unajidanganya.

1 Yohana 2:15-17

[15]Msiipende dunia, wala mambo yaliyomo katika dunia. Mtu akiipenda dunia, kumpenda Baba hakumo ndani yake.

[16]Maana kila kilichomo duniani, yaani, tamaa ya mwili, na tamaa ya macho, na kiburi cha uzima, havitokani na Baba, bali vyatokana na dunia.

[17]Na dunia inapita, pamoja na tamaa zake, bali yeye afanyaye mapenzi ya Mungu adumu hata milele.

Chagua leo ni kawaida ipi, unasimama nayo..Je! ile ya mbinguni au ya duniani hii. Kamwe usijaribu kuwa hapo katikati, yaani vuguvugu..una hatari kubwa sana ya kutapikwa..kumchanganya Mungu na udunia, ni hatari kubwa sana.

Bwana akubariki

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Biblia inamaanisha nini iliposema “wakidhania kuwa ulevi wakati wa mchana ni anasa;?

KUTII NI BORA KULIKO DHABIHU.

HAMA KUTOKA GIZANI

ZIFAHAMU KAZI TATU ZA ROHO MTAKATIFU KATIKA ULIMWENGU.

Kutazama Nyakati mbaya ni kufanyaje?.

Vitabu vya Deuterokanoni ni vya kiMungu?

Biblia inamaana gani iliposema “Dhambi ilipozidi, Neema ilizidi kuwa nyingi Zaidi”.

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments