MWANANGU, NIPE MOYO WAKO;

MWANANGU, NIPE MOYO WAKO;

Mithali 23:26 “Mwanangu, nipe moyo wako; Macho yako yapendezwe na njia zangu.  27 Kwa maana kahaba ni shimo refu; Na malaya ni rima jembamba.  28 Naam, huotea kama mnyang’anyi; Huwaongeza wenye hila katika wanadamu”.

Nakusalimu katika jina la mwokozi wetu Yesu Kristo. Kwa neema zake karibu tujifunze maneno ya uzima.

Hapo anaanza kwa kusema ‘mwanangu nipe moyo wako’..Halafu baada ya moyo anasema na “macho yako pia yapendezwe na njia zangu”…..Ni kwanini aseme hivyo? Ni kwasababu hapo ndipo kiini cha tatizo sugu la uzinzi kilipo.

Nataka tuone kwa jicho la ndani kwamba kahaba au Malaya anayezungumziwa hapa sio Yule unayekutana naye barabarani,akijiuza, bali ni Yule ambaye amesimama katika macho yako. .. Bwana Yesu alimjua kahaba huyu ndio maana akasema 

Mathayo 5:28  “lakini mimi nawaambia, Kila mtu atazamaye mwanamke kwa kumtamani, amekwisha kuzini naye moyoni mwake”

Umeona, huyu anapitia machoni, kisha akishafunguliwa mlango anaingia moyoni mwako kuzini na wewe. Haonekani kwa macho ya kibinadamu, huyu hana gharama yoyote, hatoboi siri, wala hakuzungushi zungushi, wakati wowote ukimuhitaji yupo hapo mlangoni kwenye macho yako anataka kuingia.

Sasa akishapewa  nafasi ya kutosha ndio hapo anapochukua umbile la mtu ili kujidhihirisha kwa nje tu. Ataonekana aidha kwa kumfuata wewe, au yeye kukufuata wewe..sio makahaba wote watakufuata.

Daudi hakufuatwa na mke wa Uria, bali ni yeye ndiye aliyemfuata, mwisho wa siku akatumbukia katika shimbo refu, akajitia unajisi mwenyewe(akajiongezea hila). Ni kwasababu gani? Ni kwasababu alimpa nafasi Yule aliyesimama mbele ya macho yake, alipomwona mwanamke anaoga, badala ayafiche macho yake akimbie mbali, aikatae hiyo hali isiingie moyoni mwake akairuhusu, ndipo kahaba huyo aliyechukua umbile la mke wa mtu akajidhihirisha kwa nje, akamfuata na kwenda kuzini naye.

Samsoni, hakufuatwa na Delila, isipokuwa alivutiwa katika macho yake, alipoona wanawake wa kifilisti ni warembo zaidi ya wakiyahudi,wana maumbile mazuri, wanavaa vizuri, akayatii macho yake..Na ndio hayo hayo yalikuja kupofuliwa baadaye, akatumbukia katika rima jembamba, akafa bado ni kijana.

Sulemani, hakujazuia macho yake, wala moyo wake, Ndio maana akajikusanyia wanawake wengi kwa jinsi alivyopenda, yeye mwenyewe kama alivyoandika katika kitabu cha mhubiri;

Mhubiri 2:10 “Wala sikuyanyima macho yangu cho chote yalichokitamani; wala sikuuzuia moyo wangu katika furaha yo yote; maana moyo wangu ulifurahi kwa sababu ya kazi yangu yote, na hii ilikuwa sehemu yangu katika kazi yangu yote.

Matokeo yake ikawa ni wao kumgeuza moyo. Na kumkosea Mungu, akaabudu miungu mingine, akawa ni miongoni mwa wenye hila(dosari), katika wanadamu.

Lakini Yusufu, hakuruhusu moyo wake na macho yake yashawishwe na huyu kahaba sugu, hata alipojaribiwa kwa nguvu alikimbia kabisa. Akajiepusha na anguko hilo.

Hii ni kutufundisha nini?

Bwana Yesu alipokitazama kizazi kile, alikiona kama ni kizazi cha Uzinzi (Marko 8:38), sio kwasababu kila mtu alikuwa anazini tu ovyo ovyo huko barabarani, hapana, lakini aliwaona hawa makahaba wa siri wakizini nao mioyoni mwao, 

Tusemeje sasahivi.?

Picha na video za ngono ambazo zimewaharibu watoto na vijana, vipindi vya tv, na tamthimilia na muvi ambazo zinabeba maudhui ya kizinzi ndani yake, vinaongoza matendo haya rohoni.

Kujichua, na mazungumzo mabaya maofisini, mashuleni, na vijiweni  yanaongeza kwa kasi uasherati rohoni. Ni lazima tufahamu Ile kukutana na mvulana/msichana ni matokeo tu ya nje, ambayo hupaswi kujutiwa sana zaidi ya chanzo husika ambacho kinaanzia kwenye macho kisha baadaye moyoni.

Tutawezaje kupona?

Awali ya yote ni kwa kudhamiria kabisa kutubu dhambi zetu na kuuacha ulimwengu, kwa kumkaribisha Yesu mioyoni mwetu. Pili ni kwa kufanya agano na macho yetu, kama alivyofanya mtumishi wa Mungu Ayubu.

Ayubu 31:1 “Nilifanya agano na macho yangu; Basi nawezaje kumwangalia msichana”?

Usifungue macho yako kushawishwa na kimelea chochote ambacho kinaweza kukusababishia tamaa moyoni  mwako, pambana sana hapo, Ikiwa upo katika ndoa fungua tu kwa mkeo/mumeo..Ikiwa upo nje, usiruhusu kabisa.. weka mipaka na marafiki wa jinsia tofauti, acha kutazama muvi, au picha picha mitandaoni, acha mazungumzo mabaya, ukipishana na mwanamke amevaa kizinzi macho yako yasigeuke nyuma endelea mbele. Kwa kufanya hivyo utafanikiwa kumuua huyu kahaba atokeaye mbele ya macho yako.Na hawa wa nje watakufa wenyewe. Utaishi maisha ya ushindi sikuzote.

Bwana atuponye, Bwana atusaidie.

Mathayo 23:26  “Ewe Farisayo kipofu, safisha kwanza ndani ya kikombe, ili nje yake nayo ipate kuwa safi”

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Mruba ni mdudu gani kwenye biblia?(Mithali 30:15)

JE UPANGA UMEINGIA MOYONI MWAKO?

JE! JICHO LAKO LINAONA NINI KATIKATI YA MAJARIBU?

MOTO HUFA KWA KUKOSA KUNI.HATA UASHERATI NAO

LAKINI SISI HATUKUIPOKEA ROHO YA DUNIA.

Konzo la Ng’ombe ni nini? (Waamuzi 3:31).

KIASI NI NINI KATIKA UKRISTO?

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
2 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Anonymous
Anonymous
1 year ago

SHALLOM m yeremia giyamb toka (w) hanang mkoa manyara Nawa shukuru watumish wa mungu kwa kazi yenu njema na nzur kama hiyo mungu awa brikini sanaa nime jifunza mambo mengi sana