Konzo la Ng’ombe ni nini? (Waamuzi 3:31).

Konzo la Ng’ombe ni nini? (Waamuzi 3:31).

Swali: Lile Konzo la Ng’ombe Shamgari alilowapigia Wafilisti mia sita lilikuwa ni nini?

Jibu: Tusome,

Waamuzi 3:30 “Basi Moabu alishindwa siku hiyo chini ya mikono ya Israeli. Nayo nchi ikawa na amani muda wa miaka themanini

 31 Tena baada yake huyo alikuwapo Shamgari mwana wa Anathi, aliyepiga katika Wafilisti watu mia sita KWA KONZO LA NG’OMBE; yeye naye aliwaokoa Israeli”

“Konzo” ni lugha nyingine ya “Mchokoo”. Na mchokoo ni kipande kifupi cha fimbo ya chuma, ambayo mwishoni ina ncha kali, fimbo hii ilitumika enzi za kale kuongozea ng’ombe wakati wa kulima. Wakati ambapo Ng’ombe waligoma kulima au kutembea kwa kasi inayohitajika na mkulima, basi fimbo hiyo ya chuma yenye ncha iliwekwa nyuma yao, na kuwachoma migongo yao.. Hivyo walipoguswa na ncha hiyo ya chuma na kusikia maumivu, basi walisonga mbele…

Mchokoo tunaweza kuusoma katika

Matendo 26:14 “Tukaanguka nchi sote, nikasikia sauti ikisema nami kwa lugha ya kiebrania, Sauli! Sauli! Mbona waniudhi? NI VIGUMU KWAKO KUUPIGA MATEKE MCHOKOO.

15  Nami nikasema, Wewe u nani, Bwana? Bwana akaniambia, Mimi ni Yesu, ambaye wewe unaniudhi”.

Paulo alikuwa anashindana na maagizo ya Mungu, na ndipo Bwana Yesu akampa hiyo mithali, kumwonyesha jinsi hali yake ya kiroho ilivyo..

Sasa kwa maelezo marefu zaidi kuhusu Mchokoo, na jinsi leo hii watu wanavyopiga mateke mchokoo wa Bwana Yesu unaweza kufungua hapa >>USIPIGE MATEKE MCHOKOO!

Lakini tukirudi kwa Shamgari, Mwamuzi aliyetiwa mafuta na Mungu kuwaokoa wana wa Israeli, maandiko yanatuambia alitumia hilo Konzo/Mchokoo kuwapiga wafilisti mia sita.

Hiyo ni kuonyesha ushujaa aliokuwa nao katika Bwana, na kuonyesha kuwa Mungu haokoi tu kwa mapanga na majeshi, bali anaokoa kwa jina lake kupitia vitu vilivyo dharaulika, Kama alivyofanya kwa Daudi.

Daudi alimwangusha Goliathi kwa jiwe moja tu, ambalo alilirusha kwa Goliathi na kumwua shujaa yule wa Wafilisti. Na ndivyo Mungu alivyomtumia huyu Shamgari kwa Konzo moja la Ng’ombe kuangusha mashujaa 600 wa kifilisti.

Hiyo ikitufundisha kuwa na sisi hatuna budi kumtegemea Bwana asilimia zote..pasipo kutegemea uwezo wetu, wala nguvu zetu wala uwezo wetu, kwasababu siku zote vita ni vya Bwana… Na Bwana anavitumia vitu vidhaifu kuviabisha vile vyenye nguvu. (sawasawa na 1Wakorintho 1:27-29).

1Samweli 17:42 “Hata Mfilisti alipotazama huku na huku, akamwona Daudi akamdharau; kwa kuwa ni kijana tu mwekundu, tena ana sura nzuri. 

43 Mfilisti akamwambia Daudi, Je! Mimi ni mbwa hata umenijia kwa fimbo? Mfilisti akamlaani Daudi kwa miungu yake.

 44 Mfilisti akamwambia Daudi, Njoo huku kwangu; nyama yako nitawapa ndege wa angani na wanyama wa mwituni. 

45 NDIPO DAUDI AKAMWAMBIA YULE MFILISTI, WEWE UNANIJIA MIMI NA UPANGA, NA FUMO, NA MKUKI, BALI MIMI NINAKUJIA WEWE KWA JINA LA BWANA WA MAJESHI, MUNGU WA MAJESHI YA ISRAELI ULIOWATUKANA.

 46 Siku hii ya leo Bwana atakuua mkononi mwangu, nami nitakupiga, na kukuondolea kichwa chako, nami leo nitawapa ndege wa angani na wanyama wa nchi mizoga ya majeshi ya Wafilisti, ili kwamba dunia nzima wajue ya kuwa yuko Mungu katika Israeli.

 47 NAO JAMII YA WATU WOTE PIA WAJUE YA KWAMBA BWANA HAOKOI KWA UPANGA WALA KWA MKUKI; MAANA VITA NI VYA BWANA, NAYE ATAWATIA NINYI MIKONONI MWETU”.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

KUNA NGUVU YA ZIADA KATIKA KULING’ANG’ANIA KUSUDI LA MUNGU.

Nini maana ya usimfunge ng’ombe kinywa apurapo nafaka!.(Kumbukumbu 25:4)

Kwanini Bwana Yesu aliwaambia wanafunzi wake wasichukue chochote isipokuwa fimbo tu?

Maji ya Farakano ni nini katika biblia?

Naye atawachunga kwa fimbo ya chuma.

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments