Chuo cha vita vya Bwana ni kipi?(Hesabu 21:14)

Chuo cha vita vya Bwana ni kipi?(Hesabu 21:14)

SWALI: Naomba kufahamu hichi “Chuo cha vita vya Bwana” kinachozungumziwa katika Hesabu 21:14  ni kipi?.


Hiki ni moja ya vitabu ambavyo vinatajwa katika biblia lakini leo hii havipo, vinginevyo ikiwemo kitabu cha Yashari,(2Samweli 1:18), Kitabu cha tarehe cha wafalme wa Yuda(1Wafalme 14:29), Kulikuwa pia na  kitabu cha tarehe ya Nathani nabii, halikadhalika kitabu cha tarehe ya Gadi mwonaji, Na kitabu cha tarehe cha Samweli mwonaji, (1Nyakati 29:29); Vitabu hivi vyote havipo kwenye biblia hadi hii leo, japokuwa vimezungumziwa.

Kama vile jina lake linavyojieleza kinadhaniwa kuwa ni kitabu kilichokuwa kinarekodi matukio yote ya vita ambavyo Bwana aliwapigania watu wake, na kuwaokoa kwa mkono mkuu.

Japo, habari zote za kitabu hicho hazijawa wazi hadi leo, ni mambo gani na gani yalizungatiwa kuandikwa ndani yake. Lakini enzi za agano la kale, kitabu hichi kilikuwa ni kitabu maarufu kati ya vitabu vya kihistoria vya kiyahudi.

Habari ya kitabu hichi utaipata sehemu moja tu katika biblia,

Hesabu 21:13 “Kutoka huko wakasafiri, wakapanga upande wa pili wa Arnoni, ulio jangwani, utokao katika mpaka wa Waamori; maana, Arnoni ndio mpaka wa Moabu, kati ya Moabu na Waamori.

14 Kwa hiyo imesemwa katika chuo cha Vita vya Bwana, Wahebu katika Sufa, Na bonde za Arnoni,”

Lakini ni kwanini Mungu hakukiruhusu kiwepo hadi leo?

Kama Biblia ingerekodi matendo yote makuu Mungu aliyowafanyia watu wake tangu kuumbwa kwa ulimwengu hadi sasa, vitabu vyote duniani visingetosha kwa habari zake. Kama tu habari za matukio ya Yesu aliyoyafanya hapa duniani biblia inasema vitabu havitoshi kuelezea itakuwaje yaanzie tangu agano la kale.

Hivyo habari hizo chache zilizoandikwa kwenye biblia, Mungu ameona walau zitamtosha kila mtu azisome na kumsaidia,. Sasa ikiwa tumerahisishiwa habari njema hizi njema, kwa bahari chache sana, halafu tutakataa kusoma, basi hapo tunaonyesha ni jinsi gani tulivyo wavivu.

Ni lazima ujiulize ni kwanini hadi wakati huu uliofikia hujawahi kuisoma biblia yote? Lakini wakati huo huo magazeti uliyoyasoma, pamoja na vitabu shuleni, na mtaani umemaliza hata kurasa milioni 5, lakini biblia hujamaliza. Jiulize tatizo ni nini? Au urahisishiwe nini tena ndio usome.?

Kusoma biblia ni kutia bidii kidogo tu, Paulo alimwambia Timotheo maneno haya;

1Timotheo 4:13 “Hata nitakapokuja, ufanye bidii katika kusoma…”

Hivyo jijengee utaratibu wa kusoma biblia kila siku.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Kitabu cha YASHARI kinachozungumziwa katika 2Samweli 1:17-18, ni kitabu gani?

NGURUMO SABA

KUSUDI LA MIMI KUWEPO DUNIANI NI LIPI?

Sadaka ya kuinuliwa ni sadaka ya namna gani?

Pomboo ni nini katika biblia?(Kutoka 25:5, Ezekieli 16:10)

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
2 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Augustino Mwakafwila
Augustino Mwakafwila
3 months ago

Niunganishe kwenye mafundisho