TUMEKUWA TAMASHA KWA DUNIA; KWA MALAIKA NA WANADAMU.

TUMEKUWA TAMASHA KWA DUNIA; KWA MALAIKA NA WANADAMU.

Paulo alipouna utumishi wake, na wenzake jinsi ulivyo, na kuona magumu anayoyapitia katika huduma yake, mwisho wa siku alisema maneno haya..

1Wakorintho 4:9 “Maana nadhani ya kuwa Mungu ametutoa sisi mitume mwisho, kama watu waliohukumiwa wauawe; kwa sababu TUMEKUWA TAMASHA kwa dunia; kwa malaika na wanadamu.

10 Sisi tu wapumbavu kwa ajili ya Kristo, lakini ninyi ni wenye akili katika Kristo; sisi tu dhaifu, lakini ninyi mna nguvu; ninyi mna utukufu, lakini sisi hatupati heshima.

11 Hata saa hii ya sasa, tuna njaa na kiu, tu uchi, twapigwa ngumi, tena hatuna makao;

12 kisha twataabika tukifanya kazi kwa mikono yetu wenyewe. Tukitukanwa twabariki, tukiudhiwa twastahimili;

13 tukisingiziwa twasihi; tumefanywa kama takataka za dunia, na tama ya vitu vyote hata sasa:.

Kumbuka Matamasha ya zamani sio kama haya tuliyo nayo sasa.

Matamasha ya zamani yalikuwa yanafanyika katika viwanja vikubwa sana vya michezo, na michezo yenyewe vilevile  haikuwa  kama hii tuliyonayo sasa hivi, mfano mpira, au riadha, hapana, bali ni michezo ya kupigana miereka ya kufa na kupona, , ambayo ilikuwa inapiganwa na watu waliobebea sana katika vita, watu hawa walikuwa aidha ni wafungwa walioshindikana, kwa kesi za mauaji au watumwa, walionunuliwa kutoka mbali, hivyo walichokuwa wanafanya ni kuwachukua na kuwapeleka katika mafunzo haya ya muda mrefu kujifunza kupigana

Hivyo wakati Fulani unafika, ndio wanawaleta sasa kwenye viwanja hivyo vikubwa ili wapambane, ambapo maelfu ya watu walikuwa wanakusanyika kutazama mapigano hayo. Hayakuwa mapigano ya  miereka kama tunayoyaona sasa hivi kwenye Tv, watu wanaumizana tu kidogo halafu baadaye wanaachana hapana, bali mapigano kweli kweli ya kushika mapanga na ngao.

Kule juu kila mtu akikaa akimshangilia mchezaji wake., Na mwishoni ni lazima mmojawapo auawe. Na wakati mwingine ilikuwa ni kupigana na wanyama wakali kama vile, simba, chuo au vifaru.

Sasa wakristo wa kwanza waliokuwa wanauawa, waliingizwa kwenye viwanja hivi, vya mapambano, vilivyojulikana kama Arena. na huko ndani wanakutana na hawa wapiganaji waliobebea na kama sio hao basi waliachiliwa wanyama wakali kama Simba au chui, wapambane nao. Kwa namna ya kawaida unaelewa ni nani atashinda hapo. Kwasababu sikuzote wakristo sio wapiganaji, pengine watakachofanya tu ni kutafuta njia ya kunusuru maisha yao, lakini mwisho wa siku watauliwa tu, . Kumbuka wakati huo waelfu wa watu wapo majukwaani wanawatazama kama vile tamasha, wakishabikia, na kufurahia, kama vile timu Fulani ya simba na Yanga inacheza.

Sasa Mtume Paulo aliutolea mfano huo kuonyesha ni jinsi gani watumishi wa Mungu, wanavyoonekana duniani leo hii. Wanatolewa ili watazamwe jinsi wanavyouawa, Paulo alisema tunakufa kila siku, 1Wakorintho 15:31,

Na kama vile teknolojia ilivyokuja juu sana, watamazaji wa matamasha wameongeza, kiasi kwamba sio tu wale walio kwenye viwanja wanaona mchezo wote, bali na wa mbali pia, vivyo hivyo, dhiki hizi wa watumishi wa Mungu zinaonekana mpaka kwa malaika wa Mungu mbinguni, wanatuona na kutuhurumia.

Lakini kwanini Mungu aruhusu iwe hivyo?

Hiyo inatupa chachu ya mambo mawili, la kwanza, ni kuwa wewe kama mtumishi wa Mungu, ufanyapo kazi ya Mungu, fahamu kuwa wewe ni kama tamasha la ulimwengu, matusi ni lazima yawe sehemu ya maisha yako, dhihaka zitakuwa zako, kupigwa na wakati mwingine kufukuzwa na kuuliwa vitakuwa vyako, hivyo kama vile Bwana Yesu alivyosema..

Luka 6:22 “Heri ninyi watu watakapowachukia, na kuwatenga, na kuwashutumu, na kulitupa nje jina lenu kama neno ovu, kwa ajili ya Mwana wa Adamu.

23 Furahiwani siku ile na kuruka-ruka, kwa kuwa, tazama, thawabu yenu ni kubwa mbinguni, maana, baba zao waliwatenda manabii vivyo hivyo”.

Vivyo hivyo na wewe furahi kwasababu ufalme wa mbinguni ni wako.

Lakini kwa wewe ambaye unahubiriwa injili na unaipuuzia, unatoa maneno ya dhihaka, unacheka, unatukana, unaleta fitina, ujue kuwa, Bwana Yesu alisema maneno haya vilevile..

Mathayo 10:14 “Na mtu asipowakaribisha wala kuyasikiliza maneno yenu, mtokapo katika nyumba ile, au mji ule, kung’uteni mavumbi ya miguuni mwenu.

15 Amin, nawaambia, itakuwa rahisi nchi ya Sodoma na Gomora kustahimili adhabu ya siku ya hukumu, kuliko mji ule”.

Unaona, ikiwa unaigeuza kazi ya Mungu kama tamasha tu la kusikiliza, kuambiwa, kuona wengine wanamtafuta Mungu lakini wewe unakuwa kama mshabiki tu, na hutaki kukitendea kazi kile ulichoambiwa, ujue huko ng’ambo adhabu yako itakuwa ni  kubwa sana.. Zaidi hata ya wale watu wa Sodoma na Gomora, ambao kulingana na maneno ya Bwana Yesu tunaona hadi sasa adhabu yao haijaisha, sasa jiulize wewe utakuwa wapi?

Bwana alisema pia..

Luka 12:47 “Na mtumwa yule aliyejua mapenzi ya bwana wake, asijiweke tayari, wala kuyatenda mapenzi yake, atapigwa sana.

48 Na yule asiyejua, naye amefanya yastahiliyo mapigo, atapigwa kidogo. Na kila aliyepewa vingi, kwake huyo vitatakwa vingi; naye waliyemwekea amana vitu vingi, kwake huyo watataka na Zaidi”.

Jiulize wewe unaishi kwa ajili ya nini? Kama watumishi wa Mungu wanapitia adhabu ya Mungu wakiwa hapa duniani, jiulize wewe mwenye dhambi utaonekania wapi siku ile kama mtume Petro alivyosema katika 1Petro 4:15-17 Kumbuka mbinguni hakitaingia kinyonge..Unauchukulia wokovu wako juu juu tu, ufahamu kuwa unyakuo ukipita leo, huendi popote. Hata kama utasema wewe ulibatizwa, au ulimpa Yesu maisha yako, hutakwenda popote ndugu. Usipojikana nafsi na kumfata Yesu, utabakia hapa hapa duniani. Nivyo ilivyo hukumu ipo.

Maran Atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

MAUAJI YA HALAIKI NDANI YA KANISA.

MATARAJIO YA KILA MWANADAMU DUNIANI NI YAPI?

Hanithi ni nini katika biblia? (kumbukumbu 23:17)

CHUKIZO LA UHARIBIFU

MWANZO WA INJILI YA YESU KRISTO.

KITABU CHA YUDA: SEHEMU YA 1

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments