Maongeo ni nini?(Wakolosai 2:19)

Maongeo ni nini?(Wakolosai 2:19)

Maongeo ni maongezeko,

Kwa mfano Neno hilo utalisoma katika vifungu hivi;

 Kutoka 23:10 “Utapanda mbegu katika nchi yako muda wa miaka sita na kuyavuna maongeo yake;

11 lakini mwaka wa saba utaiacha nchi ipumzike na kutulia; hao maskini miongoni mwa watu wako wapate kula; na hicho watakachosaza wao, wapate kula wanyama wa kondeni. Utafanya vivyo katika shamba lako la mizabibu, na katika shamba lako la mizeituni”.

Soma pia Walawi 19:24

Maana yake ni kuwa kwa muda wa miaka sita Mungu aliwaruhusu wana wa Israeli wapande na kuvuna, hata na vile vinavyoongeza katika mavuno yao. Lakini ufikapo mwaka wa saba, hawakuruhusiwa kuvuna chochote bali waviache kwa ajili ya maskini na Wanyama wa kondeni.

Isaya 9:7 “Maongeo ya enzi yake na amani Hayatakuwa na mwisho kamwe, Katika kiti cha enzi cha Daudi na ufalme wake; Kuuthibitisha na kuutegemeza Kwa hukumu na kwa haki, Tangu sasa na hata milele. Wivu wa Bwana wa majeshi ndio utakaotenda hayo”.

Maana yake ni kuwa maongezeko ya enzi yake, na amani hayatakuwa na mwisho yataendelea kuongezeka na kuongezeka milele. Na anayezungumziwa hapo si mwingine Zaidi ya Yesu Kristo Bwana wetu.

Wakolosai 2:18 “Mtu asiwanyang’anye thawabu yenu, kwa kunyenyekea kwa mapenzi yake mwenyewe tu, na kuabudu malaika, akijitia katika maono yake na kujivuna bure, kwa akili zake za kimwili;

19 wala hakishiki Kichwa, ambacho kwa yeye mwili wote ukiruzukiwa na kuungamanishwa kwa viungo na mishipa, hukua kwa maongeo yatokayo kwa Mungu”.

Hapo anaposema, “hukua kwa maongeo yatokayo kwa Mungu”, ana maana kuwa, mwili huo(ambao ndio kanisa la Kristo) ukishakwisha kushikamanishwa Pamoja viungo vyote.. Basi hukua, kwa maongezeko (maongeo), yatokayo kwa Mungu..Sio maongezeko yatokayo kwa mwanadamu.

Hii ikiwa na maana hata sisi kama wakristo, tukishikama Pamoja na Kristo tukamfanya kuwa kichwa chetu, basi, tutakuwa katika ukuaji (maongezeko )unaotoka kwa Mungu mwenyewe..

Lakini kinyume chake ni kweli tukimkataa Kristo, kama kichwa cha kanisa, na kuwafanya wanadamu kuwa ndio vichwa vyetu, basi hatutakuwa na maongezo yoyote ya rohoni au mwilini, na hata kama tukiwa nayo, basi yatakuwa hayatokani na Mungu bali ibilisi.

Hivyo hatuna budi kumfanya Kristo kichwa cha kila kitu.. kwasababu ufalme wake unadumu milele. Lakini tukifanya tunajua kujenga ngome zetu au falme zetu, tufahamu kuwa taabu zetu zitakuwa ni bure mwisho wa siku.

Ukuaji wetu wa ndani na nje, unamtegemea Yesu Kristo tu, zaidi yake hakuna mwingine.

Sifa heshima na utukufu vimrudie yeye milele na milele daima.

Bwana atusaidie.

Shalom..

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Sadaka ya kinywaji ilikuwaje? Na inawakilisha nini?

Mkatale ni nini katika biblia? (Matendo 16:24)

SIFONGO NA SIKI NI NINI?

Pakanga ni nini?

Talanta ni nini katika biblia (Mathayo 25:14-30)

Santuri ni nini? (Danieli 3:5,10)

Bushuti ni nini?

Donda-Ndugu ni nini?

Pango la Makpela ni lipi, je lina umuhimu wowote kwetu?

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments