Title January 2023

YEYE ATAWABATIZA KWA ROHO MTAKATIFU NA KWA MOTO.

Maandiko yanasema kuwa Bwana Yesu hakuwahi kumbatiza mtu yeyote kwa maji katika huduma yake yote…

Yohana 4:1 “Kwa hiyo Bwana, alipofahamu ya kuwa Mafarisayo wamesikia ya kwamba, Yesu anafanya wanafunzi wengi kuliko Yohana, na kuwabatiza,

(lakini Yesu mwenyewe hakubatiza, bali wanafunzi wake)

Umeona?.. kila mahali Bwana Yesu alipofika aliwaachia wanafunzi wake wabatize!.. lakini yeye mwenyewe hakubatiza mtu yeyote kwa maji. Sasa hiyo haimaanishi kuwa ubatizo wa maji hauna maana!. (mbele kidogo tutaelewa zaidi umuhimu wake).

Sasa kufuatia mwenendo huo wa Bwana Yesu kutombatiza mtu yeyote, ni kuonyesha kuwa anao ubatizo mwingine ambao atawabatiza nao watu, ambao hakuna mwanadamu yeyote anayeweza kuufanya!… Ubatizo wa maji mwanadamu anaweza kuufanya kwa mwanadamu mwenzake, Lakini ubatizo huo ambao Bwana Yesu atakwenda kuwabatiza nao watu hakuna anayeweza kuufanya zaidi yake yeye mwenyewe.. Na ubatizo huo si mwingine zaidi ya ule wa Roho Mtakatifu.

Tunapobatizwa kwa Maji, miili yetu inazama kwenye maji mengi na kuibuka juu, kama ishara ya kufa na kufufuka na Kristo.. Lakini tunapobatizwa kwa Roho Mtakatifu ni kitendo cha Bwana Yesu kuzichukua roho zetu na kuzizamisha katika Roho Mtakatifu, Ni tendo kuu sana ambalo hakuna mwanadamu yeyote wala malaika yeyote anayeweza kulifanya.. kama maandiko yanavyosema katika Yohana 3:16.

Luka 3:16 “Yohana alijibu akawaambia wote, Kweli mimi nawabatiza kwa maji; lakini yuaja mtu mwenye nguvu kuliko mimi, ambaye mimi sistahili kuilegeza gidamu ya viatu vyake; YEYE ATAWABATIZA KWA ROHO MTAKATIFU NA KWA MOTO”

Hiyo ikimaanisha kuwa kama vile ubatizo wa maji ulivyo wa muhimu vile vile na ubatizo wa Roho Mtakatifu ni wa muhimu sana..Ni lazima tubatizwe na watu katika Maji na vile vile tubatizwe na Bwana Yesu katika Roho Mtakatifu.

Wapo watu wanaosema kuwa ubatizo wa Roho Mtakatifu sio wa muhimu, bali ule wa maji tu unatosha, na wapo wanaosema ubatizo wa Roho Mtakatifu ndio wa muhimu, hivyo mtu akishaupata ubatizo wa Roho Mtakatifu hakuna haja tena ya ubatizo wa maji. Nataka nikuambie kuwa hiyo imani ni imani potofu ambayo imetengenezwa na ufalme wa giza kuwaua watu kiroho, maandiko yanasema “…Mtu asipozaliwa kwa maji na kwa Roho, hawezi kuuingia ufalme wa Mungu (Yohana 3:5) ”

Kuzaliwa kwa maji ni ubatizo wa Maji, na kuzaliwa kwa Roho ni ubatizo wa Roho Mtakatifu (Haihitaji elimu kubwa kuelewa hili, ni tafakari nyepesi kabisa).

Na zaidi ya yote tunazidi kuthibitisha kuwa ubatizo wa maji ni wa muhimu hata baada ya kuupokea ule wa Roho Mtakatifu, wakati ule Petro alipofika nyumbani kwa Kornelio, maandiko yanasema baada ya wale watu wa nyumbani kwa Kornelio kushukiwa na Roho Mtakatifu, bado Mtume Petro aliwaagiza wakabatizwe katika maji na kwa jina la Yesu Kristo.

Matendo 10:44  “Petro alipokuwa akisema maneno hayo Roho Mtakatifu akawashukia wote waliolisikia lile neno.

45  Na wale waliotahiriwa, walioamini, wakashangaa, watu wote waliokuja pamoja na Petro, kwa sababu Mataifa nao wamemwagiwa kipawa cha Roho Mtakatifu.

46  Kwa maana waliwasikia wakisema kwa lugha, na kumwadhimisha Mungu. Ndipo Petro akajibu,

47  Ni nani awezaye kuzuia maji, hawa wasibatizwe, watu waliopokea Roho Mtakatifu vile vile kama sisi?

48  Akaamuru wabatizwe kwa Jina lake Yesu Kristo. Ndipo wakamsihi azidi kukaa siku kadha wa kadha”

Umeona?, hao watu walitangulia kubatizwa na Bwana Yesu mwenyewe kwa  ubatizo wa Roho mtakatifu, lakini bado walikwenda kubatizwa tena na akina Petro kwa ubatizo wa Maji. Kwasababu Petro alijua kuwa hawa wasipozaliwa kwa Maji na kuwaacha tu wawe wamepokea ubatizo wa Roho hawataweza kuuona ufalme wa Mungu, sawasawa na maneno ya Bwana.

Je! na wewe umebatizwa kwa Maji?.. Kama bado na umeshasikia ukweli namna hii, upo hatarini sana…Na kumbuka kama ulibatizwa uchangani, basi huna budi kubatizwa upya kwa sababu hukuwa umejitambua wakati huo, zaidi sana kama pia ulibatizwa kwa maji machache, ni lazima ubatizwe upya kwa maji mengi (Yohana 3:23)

Na je! umeshabatizwa pia kwa Roho Mtakatifu?.. kama Bado msihi Bwana naye ni mwaminifu atakupa Roho wake mtakatifu, kwasababu yeye anatamani uwe naye kuliko wewe unavyotamani.. lakini ni sharti kwanza utubu kwa kumaanisha kuacha dhambi zako zote na kubatizwa kwa maji kama tayari umeshausikia ukweli, kwa kukamilisha mambo hayo, maandiko yanasema Yule Roho ni kwaajili yetu, na kwa vizazi vyetu, Bwana Yesu anatubaziwa kwa huyo bureeeeeeeeee..

Matendo 2:37  “Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu?

38  Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.

39  Kwa kuwa ahadi hii ni kwa ajili yenu, na kwa watoto wenu, na kwa watu wote walio mbali, na kwa wote watakaoitwa na Bwana Mungu wetu wamjie”

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

TOFAUTI YA UBATIZO WA YOHANA NA UBATIZO WA BWANA YESU

JE! UMEBATIZWA UBATIZO SAHIHI?

NUNUA MAJI YA UZIMA.

MFANO WA MAMBO HAYO NI UBATIZO.

UBATIZO NI NINI NA ULIO SAHIHI NI UPI?

Rudi nyumbani

Print this post

Mofa ni nini? na inafunua nini kiroho?(1Samweli 28:24).

Jibu: Tusome,

1Samweli 28:24 “Naye yule mwanamke alikuwa na ndama aliyenona nyumbani; akafanya haraka kumchinja; akatwaa na unga, akaukanda, akafanya MKATE WA MOFA kwa unga huo”.

Mkate wa Mofa ni mkate uliotengenezwa bila kuwekwa “Hamira”.  Hamira kwa lugha ya kibiblia inaitwa “Chachu” kazi yake ni kuchachusha au kuumua unga uliokandwa, kama biblia inavyosema katika..

Mathayo 13:33  “Akawaambia mfano mwingine; Ufalme wa mbinguni umefanana na chachu aliyoitwaa mwanamke, akaisitiri ndani ya pishi tatu za unga, hata ukachachwa wote pia”

Na tena biblia inasema.. “Chachu kidogo huchachua donge zima (Wagalatia 5:9)”

Kwahiyo Mikate ya Mofa ni mikate iliyotengenezwa bila kuwekwa hamira, mfano wa chapati. Kwa  wayahudi baada ya sikukuu ya pasaka kupita, sikukuu iliyokuwa inafuata ilikuwa ni sikukuu ya mikate isiyotiwa chachu (yaani Mofa),  Ndani ya siku 7 Wana wa Israeli waliambiwa wale mikate ya Mofa, na mtu yeyote ambaye alionekana anakula mikate mingine zaidi ya hiyo, aliuawa kulingana na sheria ya torati.

Na ndani ya kipindi hicho pia mtu yeyote akionekana na Viungo vya Hamira ndani kwake, hata kama atakuwa hajaviweka kwenye unga, kitendo tu cha kuiweka ndani ilikuwa pia adhabu yake ni kifo

Kutoka 12: 15 “Mtakula mikate isiyochachwa muda wa siku saba; siku hiyo ya kwanza mtaondoa chachu yote isiwe katika nyumba zenu kabisa; kwa kuwa mtu ye yote atakayekula mkate uliochachwa tangu siku hiyo ya kwanza hata siku ya saba, nafsi hiyo atakatiliwa mbali na Israeli”.

Soma pia Walawi 23:5-6.

Lakini je! Mkate wa Mofa unawakilisha nini kiroho?

Mkate wa Mofa unawakilisha Mwili wa Bwana wetu Yesu Kristo,  Na ndio uliotumika na wakristo wa kanisa la kwanza katika kushiriki Meza ya Bwana, na ndio unapaswa utumike hata sasa katika kushiriki meza ya Bwana, na si biskuti au maandazi!.

Luka 22:19  “Akatwaa mkate, akashukuru, akaumega, akawapa, akisema, [Huu ndio mwili wangu unaotolewa kwa ajili yenu; fanyeni hivi kwa ukumbusho wangu”.

Sasa kwanini Bwana Yesu achague mkate wa Mofa, kuwakilisha Mwili wake?

Ni kwasababu Mwili wa Bwana Yesu haubadiliki wala hauwezi kubadilishwa maumbile. Hamira/chachu kazi yake ni kubadilisha maumbile ya vitu, ndio maana inapowekwa kwenye unga uliokandwa baada ya muda Fulani utakuta ule unga umeumuka!

  Sasa mwili wa Kristo hauumushwi, wala hauwezi kubadilishwa kimaumbile..bali siku zote ni ule ule!(Waebrania 13:8).. Maana yake kanuni za Bwana Yesu ni zile zile, hazibadilishwi na mazingira wala na mtu, Neno lake ni lile lile jana na leo na hata milele.

Hatuwezi kutia hamira Neno la Mungu, Neno la Mungu likisema ulevi ni dhambi!, hatuwezi kuliwekea hamira hapo na kusema ulevi sio dhambi!..likisema “mtu anapaswa avae mavazi ya kujisitiri” hatuwezi kulitia hamira kwa kusema “Mungu haangalii roho bali anaangalia mwili (1Timotheo 2:9)”

Na mambo mengine yote, biblia iliyoyataja ni lazima tuyazingatie yabaki kama yalivyo bila kuumuliwa na hamira za mafundisho ya uongo.

Bwana Yesu atusaidie katika hayo.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

MWILI NA DAMU YA YESU KRISTO.

Je ni lazima kushiriki Meza ya Bwana?

Sadaka ya unga na sadaka ya kinywaji zilikuwaje?

HII NDIO TABIA YA WATU WA KEILA, USIIGE

HERI YULE ATAKAYEKULA MKATE KATIKA UFALME WA MUNGU.

Rudi nyumbani

Print this post

NI WAPI UTAKUTANA NA MALAIKA WA BWANA?

Nakusalimu katika jina la Yesu Kristo aliye Bwana na mwokozi wetu. Utukufu na uweza ni vyake milele na milele. AMEN.

Leo tuone ni nini Bwana anasema nasi tena nyuma ya  tukio la Hajiri kijazi wa Sarai alipomtoroka bibi yake..

Kama tuonavyo katika maandiko mateso yalipozidi, alikimbilia jangwani..lakini akiwa kule jangwani, alilia sana  Bwana, amsaidie kwasababu kama tujuavyo jangwani ni mahali ambapo hakuna mahitaji yoyote ya kijamii..ukizingatia na yeye alikuwa mjamzito, hawezi kujihudumia kwa lolote.

Lakini upo uamuzi ambao hajiri aliuchukua ambao kama asingeuchukua kwa wakati ule, haijalishi angemlilia Mungu namna gani asingepata msaada wowote, wala asingeisikia sauti ya Mungu, ilipokuwa inamtafuta kusema naye kule jamgwani..

Na uamuzi wenyewe ulikuwa ni ule wa kukimbilia kwenye CHEMCHEMI YA MAJI. 

Mwanzo 16:6-12

[6]Naye Abramu akamwambia Sarai, Tazama, mjakazi wako yu mkononi mwako, mtendee lililo jema machoni pako. Sarai akamtesa, naye akakimbia kutoka mbele yake.

[7]MALAIKA WA BWANA AKAMWONA KWENYE CHEMCHEMI YA MAJI katika jangwa, chemchemi iliyoko katika njia ya kuendea Shuri.

[8]Akamwambia, Hajiri, wewe mjakazi wa Sarai, unatoka wapi, nawe unakwenda wapi? Akanena, Nakimbia mimi kutoka mbele ya bibi yangu Sarai.

[9]Malaika wa BWANA akamwambia, Rudi kwa bibi yako, ukanyenyekee chini ya mikono yake.

[10]Malaika wa BWANA akamwambia, Hakika nitauzidisha uzao wako, wala hautahesabika kwa jinsi utakavyokuwa mwingi.

[11]Malaika wa BWANA akamwambia, Tazama! Wewe una mimba, utazaa mwana wa kiume, nawe utamwita jina lake Ishmaeli, maana BWANA amesikia kilio cha mateso yako.

[12]Naye atakuwa kama punda-mwitu kati ya watu, mkono wake utakuwa juu ya watu wote na mkono wa watu wote utakuwa juu yake, naye atakaa mbele yao ndugu zake wote.

Ni vizuri tukaona kitu hapo…kumbe malaika alikuwa anamtafuta hamwoni…lakini alipofika katika ile chemchemi ya maji ndipo akamwona Hajiri kisha akazungumza naye na kumpa maagizo.

Hata sasa, watu wengi wanamlilia Mungu kweli awasaidie, wapo katika majangwa ya namna mbalimbali, na Mungu kweli anawasikia, lakini pale ambapo malaika wa Bwana wanatumwa kuwapa majibu yao hawawaoni, kwasababu hawapo katika chemchemi ya maji…wapo kwenginepo.

Na maandiko yanasema Yesu ndiye chemchemi ya maji ya uzima..

Yohana 4:13-14

[13]Yesu akajibu, akamwambia, Kila anywaye maji haya ataona kiu tena;

[14]walakini ye yote atakayekunywa maji yale nitakayompa mimi hataona kiu milele; bali yale maji nitakayompa yatakuwa ndani yake chemchemi ya maji, yakibubujikia uzima wa milele.

Ni mara ngapi tunakuwa wepesi wa kumlilia Mungu atusaidie, lakini kumuishi Kristo katika maisha yetu inakuwa ngumu.

Hatuna Muda wa kusoma Neno, hatuna muda wa kuomba, hatuna muda wa kufanya ibada, na kushuhudia habari njema, hatuna muda wa kudumu katika chemchemi ya maji ya uzima..lakini wakati huo huo tunalia Bwana tusaidie! Bwana tutetee! Bwana tubariki!, Bwana tuponye..tukiwa katika biashara zetu, katika kijiwe vyetu, katika mitandao ya kijamii tunachat, katika tv, tunaangalia movie, na tamthilia, katika party na starehe, tunakesha kila mwisho wa wiki, lakini kukesha kanisa mara moja kwa wiki hatuwezi. 

Tusahau kumwona malaika wa Bwana, akileta majibu ya maombi yetu..kwasababu macho yao hayaoni mahali pengine zaidi ya penye chemchemi ya maji ya uzima. Ndivyo walivyoumbwa, Kamwe malaika hawezi kukufuata kwenye kijiwe chako, au kwenye mihangaiko yako, kukupa majibu ya maombi yako. Atakuona tu, pindi uwapo uweponi mwa Kristo, hilo tu!…hawana shughuli na mambo ya ulimwengu huu.

Tumaanishe sasa kumrudia Bwana, kwa mioyo yetu yote..tujifunze kudumu uwepo mwa Kristo, Kuna faida nyingi. Ondoa uvivu wako katika masuala ya wokovu wa Roho yako. Ikiwa utaamka kila siku alafajiri kwenda kazini, kwanini uone uvivu kuhudhuria mikesha na ibada?

Bwana atusaidie…

Je umeokoka? Je! Unatambua ya kuwa tunaishi katika kizazi ambacho kinaweza kushuhudia tukio la kurudi kwa pili kwa Kristo duniani? Kwasababu dalili zote zimeshatimia. Na kanisa tunaloishi ndio la mwisho lijulikanalo kama Laodikia?

Umejiwekaje tayari, ikiwa upo tayari kumkabidhi Kristo maisha yako. Na unahitaji mwongozo huo, au utapenda kupata ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO, basi wasiliana nasi kwa namba zetu hizi 

+255693036618/ +254789001312

Bwana akubariki shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

WEWE U MUNGU UONAYE.

MADHARA YA KUKOSA MAJI YA UZIMA BAADA YA KIFO.

NUNUA MAJI YA UZIMA.

Kisima cha joka na lango la jaa ni nini?(Nehemia 2:13)

KISIMA CHA MAJI YA UZIMA NI KILE KILE CHA ZAMANI.

KWANINI DANI ALIKAA KATIKA MERIKEBU.

Rudi nyumbani

Print this post

HII NDIO TABIA YA WATU WA KEILA, USIIGE

(1Samweli 23:1-14)

Keila ni moja ya miji midogo  iliyokuwa Israeli, lakini kuna wakati ulipitia taabu kubwa sana ya kuvamiwa na wafilisti, wakateswa wakaibiwa nafaka zao, hivyo wakiwa katika mahangaiko hayo, na mateso hakuna wa kuwasaidia, Maandiko yanatuonesha akatokea Daudi katika maficho yake, alipokuwa anamkimbia Sauli..Akapita katikati ya mji huo,akasikia, kuwa wafilisti wapo huko wanawatesa watu wa Keila.

Lakini Daudi aliguswa sana moyo, hakujali Maisha yake na kuendelea na safari yake ya mafichoni bali alichokifanya ni kukiita kikosi chake kidogo, na kukiambia adhima yake ya kuwasaidia, japokuwa watu wake walikuwa wachache, walijitia nguvu, ndipo Daudi akaenda kumuuliza Mungu, kama akiwapigania watu wa Keila atashinda au hatashinda, Mungu akamwambia, hakika atashinda, akauliza tena na mara nyingine Mungu akamjibu hivyo hivyo kuwa watashinda.

Tengeneza picha, wenyeji wa mtu huyo wanasikia, Shujaa Daudi amekuja kuwasaidia, walifurahi kiasi gani, Na ndivyo ilivyokuwa Daudi akaenda kuwapigania watu hao, akashinda na kurejesha mateka yote, tena  na Zaidi akawarejeshea. 

Wanawake, wazee, vijana wa Keila wakahuika mioyo yao, wakafurahia kuona ng’ombe zao, ngano zao, watumwa wao, mali zao zimerudi.. Waliruka ruka na kucheza, na kumpenda sana Daudi.

Lakini habari mbaya ziliwafikia kwa ghafla watu wa Keila, biblia inasema, Sauli aliyekuwa anamwinda Daudi alipata taarifa kuwa adui yake amefika Keila, kuwasaidia watu wale. Hivyo, akatuma vikosi vyake, kwenda kumkamata. Lakini safari hii sio tena kumtafuta, bali kwenda kuwafuata wakuu wa mji huo, na kuwaambia wamkamate Daudi wamfikishe kwa Sauli ili amuue.

Lakini kabla Sauli hajatuma vikosi vyake, Daudi naye akapata taarifa kuwa Sauli amejua yupo kule, hivyo alichokifanya ni kwenda kumuuliza Mungu kama ilivyokawaida yake, kuhusiana na jambo hilo kama kweli watu wa Keila watamtoa na kumpa Sauli au La..

Matarajio ya Daudi yalikuwa ni hapana, akiamini kuwa wale watu aliowaokoa kwa mkono mkuu, watampa hifadhi watamficha, hawawezi kumsaliti, Lakini Bwana akamwambia Daudi kuwa, hao watu watakutoa kwa Sauli. Hapo Daudi akawa hana jinsi Zaidi ya kuingia tena maporini kwenda kutafuta mahali pa kujificha.

1Samweli 23:7 “Kisha Sauli aliambiwa ya kwamba Daudi amefika Keila. Sauli akasema, Mungu amemtia mkononi mwangu; kwa maana amefungwa ndani, kwa vile alivyoingia katika mji wenye malango na makomeo. 

8 Basi Sauli akawaita watu wote waende vitani, ili waishukie Keila, na kumhusuru Daudi na watu wake.  9 Naye Daudi alifahamu ya kuwa Sauli amemkusudia mabaya; akamwambia Abiathari, kuhani, Lete hapa hiyo naivera. 

10 Ndipo Daudi akasema, Ee Bwana, Mungu wa Israeli, mimi mtumwa wako nimesikia hakika ya kuwa Sauli anataka kuja huku Keila, ili kuuharibu mji kwa ajili yangu. 

11 Je! Watu wa Keila watanitoa, nitiwe mkononi mwake? Je! Sauli atashuka, kama mtumwa wako alivyosikia? Ee Bwana, Mungu wa Israeli, nakusihi, umwambie mtumwa wako. Naye Bwana akamjibu, Atashuka. 

12 Ndipo Daudi akasema, Je! Watu wa Keila watanitia mimi na watu wangu mkononi mwake Sauli? Bwana akasema, Watakutia. 

13 Basi Daudi na watu wake, ambao wapata kama mia sita, wakaondoka na kutoka Keila, wakaenda po pote walipoweza kwenda. Kisha Sauli akaambiwa ya kwamba Daudi amekimbia toka Keila; akaacha kutoka nje. 

14 Basi Daudi alikuwa akikaa nyikani ngomeni, akakaa katika nchi ya milima milima kwenye nyika ya Zifu. Naye Sauli alikuwa akimtafuta kila siku, lakini Mungu hakumtia mikononi mwake.”

Maana yake ni nini habari hii?

Wenyeji waliona ni heri mmoja wao aangamie lakini mji wote upone mikononi mwa jeshi la Sauli. Hawakujali msaada mkubwa aliowapatia, wakamwogopa mtu ambaye hakuwajali hata kidogo walipokuwa katika mateso yao. Mfano Dhahiri wa watu wa kipindi kile cha Bwana Yesu.. 

Hawakujali miujiza waliyotendewa, hawakujali wafu waliofufuliwa, pepo waliotolewa, vipofu walioona, habari njema za faraja zilizohubiriwa na Yesu, Watoto wao walioponywa. Lakini Waliposikia tu kuna hatari ya Herode kuja kuwaangamiza.. Wakasema ni heri Mmoja afe ili taifa zima lisiangamie.

Yohana 11:47  “Basi wakuu wa makuhani na Mafarisayo wakakusanya baraza, wakasema, Tunafanya nini? Maana mtu huyu afanya ishara nyingi.

48  Tukimwacha hivi, watu wote watamwamini; na Warumi watakuja, watatuondolea mahali petu na taifa letu.

49  Mtu mmoja miongoni mwao, Kayafa, aliyekuwa Kuhani Mkuu mwaka ule, akawaambia, Ninyi hamjui neno lo lote;

50  wala hamfikiri ya kwamba yafaa mtu mmoja afe kwa ajili ya watu, wala lisiangamie taifa zima”

Wakamsulibisha mwokozi wao.. Hata Sasa hatushangai kuona, watu wakimfurahia Kristo anapowasaidia tu nyakati za mateso yao, anapowabariki, anapowalinda, anapowaponya.. Lakini ikija tu tufani ndogo ya ibilisi kwa ajili ya Kristo, tayari wanamsaliti, wanautupilia mbali wokovu, akiambiwa anafukuzwa kazi kisa Yesu wake, anasahau, mema yote aliyofanyiwa na Bwana siku zote za Maisha yake. Anamwacha. Akiona umri umeenda haolewi, anasema huku kuvaa magauni ya nini tena, ngoja nivae vimini nitembee nusu uchi, ili nipate mchumba.

Tusiwe kama watu Keila, ambao walimsaliti shujaa wao kisa mtu asiyewajali, tusimwache Yesu kisa vitisho vya shetani vidogo vinavyopita mbeleni yetu. Kisa wazazi hawapendezwi na Imani yetu. Tukumbuke yeye ndio jemedari wetu, kama alitupigania vipindi vya nyuma atatupigania hata sasa.

Tumpende Bwana Mungu wetu kwa mioyo yetu yote, kwa nguvu zetu zote, kwa roho zetu zote, na kwa akili zetu zote.

Bwana atusaidie.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

KWANINI DAUDI ALIKUWA NI MTU ALIYEUPENDEZA MOYO WA MUNGU?

Naivera ni nini? Kwanini Daudi aliihitaji alipomtafuta Mungu?

Je! aliyemwua Goliathi ni Daudi au Elhanani.

WALA HAKUSIMAMA MTU PAMOJA NAYE, YUSUFU ALIPOJITAMBULISHA KWA NDUGUZE

UKIOKOKA, JIANDAE KUPITISHWA USIPOPATAZAMIA.

Je tunaruhusiwa kushirikiana na wasanii wa kidunia katika kumwimbia Mungu?

Rudi nyumbani

Print this post

Je unaruhusiwa kufanya tendo la ndoa ukiwa katika mfungo?

Haya ni Mafundisho maalumu kwa ajili ya wanawake..

JIBU: Ni vema kujua mfungo ni nini na madhumuni yake ni yapi.

Mfungo ni kitendo cha kujizuia kufanya jambo fulani la lazima kwa kipindi fulani kwa lengo la kumkaribia Mungu zaidi..

Kwamfano mfungo hasaa hulenga kujizuia kula au kunywa , wengine huzuia usingizi, wengine kazi, wengine mawasiliano n.k. inategemea unalenga nini.

Hivyo pale unapojizuia kula au kunywa lengo lako ni upate utulivu wa kuwa karibu zaidi na Mungu katika maombi na kumtafakari.

Kwahiyo kwa jinsi unavyojiweka mbali zaidi na masuala ya mwili ndivyo unavyoupa zaidi mfungo wako nguvu.

Hivyo tukirudi katika swali je tunaruhisiwa kushiriki tendo la ndoa tuwapo katika mfungo? 

Jibu ni kuwa hakuna katazo lolote..kwasababu shabaha ya mfungo wako lilikuwa katika kujizuia kula au kunywa..

Lakini ikiwa utapenda kuzuia pia tendo la ndoa, ni vizuri lakini hapo ni jambo la makubaliano na mwenzi wako, ikiwa ataliridhia kwa wakati huo msafanye tendo la ndoa, ili mwelekeze fikra zenu zote kwa Bwana…hapana shida. Ni vema.

Lakini ikiwa mmoja wenu hajaridhia, hapo hupaswi kuzuia, kwasababu uolewapo au uoapo, huna amri juu ya mwili wako, isipokuwa mwenzako, kwahiyo akikataa hupaswi kupinga.Ni lazima ufanye.

Biblia inasema..

1 Wakorintho 7:3-5

[3]Mume na ampe mkewe haki yake, na vivyo hivyo mke na ampe mumewe haki yake.

[4]Mke hana amri juu ya mwili wake, bali mumewe; vivyo hivyo mume hana amri juu ya mwili wake, bali mkewe.

[5]Msinyimane isipokuwa MMEPATANA kwa muda, ili mpate faragha kwa kusali; mkajiane tena, Shetani asije akawajaribu kwa kutokuwa na kiasi kwenu.

Vilevile ikiwa nyote hamjaridhia…pia bado hakuharibu mfungo wenu.

Hivyo kwa kuhitimisha ni kuwa kushiriki tendo la ndoa, ndani ya mfungo, hakubatilishi mfungo wa mtu. Isipokuwa tu maandiko yanatuelekeza  iwe ni kwa kiasi ili mpate na muda wa kusali 

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Je unaruhusiwa kufanya tendo la ndoa ukiwa katika mfungo?

JE NI DHAMBI KUWA NA MAHUSIANO KABLA YA NDOA?

MASWALI NA MAJIBU: YAHUSUYO NDOA- Sehemu ya 2.

Pale mwanandoa mmoja anaposhindwa kutimiza wajibu wake ufanyaje?

SIKU ZA MWISHO ZA UHAI WANGU.

Rudi nyumbani

Print this post

VYA MUNGU MPENI MUNGU.

Tunajua kuwa vya Kaisari tunavyopaswa tumpe ni “kodi” lakini je! Na Vya Mungu ambavyo tunapaswa tumpe ni vipi kulingana na Luka 20:25?

Tuanze kusoma mstari wa 21 ili tuelewe vizuri zaidi..

Luka 20:21 “Wakamwuliza, wakisema, Mwalimu, twajua ya kwamba wasema na kufundisha yaliyo ya haki, wala hujali cheo cha mtu, bali unafundisha njia ya Mungu kwa kweli

22  Je! Ni halali tumpe Kaisari kodi, au sivyo?

23  Lakini yeye alitambua hila yao, akawaambia,

24  Nionyesheni dinari. INA SURA NA ANWANI YA NANI? Wakamjibu, Ya Kaisari.

25  Akawaambia, Basi, vya Kaisari mpeni Kaisari, NA VYA MUNGU MPENI MUNGU.

26  Wala hawakuweza kumshitaki kwa maneno yake mbele ya watu; wakastaajabia majibu yake, wakanyamaa”.

Nataka tujifunze ni vigezo gani Bwana Yesu alitumia hapo kuhalalisha kuwa Kodi ni haki ya Kaisari, hiyo itatusaidia na sisi kujua vilivyo vya Mungu ni vipi?.. Na tunaona hakutumia kitu kingine chochote isipokuwa ile “Sura” inayoonekana kwenye ile sarafu pamoja na ‘Anwani” inayosomeka pale. Kwani Dinari ile ilikuwa na sura ya Kaisari na Anwani ya Kaisari, hivyo ni haki kuwa mali ya Kaisari.

Sasa kama vya Kaisari vilitambulika kwa sura iliyokuwa inaonekana juu ya Sarafu, ni wazi kuwa na vya Mungu vitatambulika kwa njia hiyo hiyo, Maana yake chochote chenye Sura ya Mungu hicho ni cha Mungu, na anapaswa apewe.. Sasa hebu tusome maandiko yafuatayo..

Mwanzo 1:27 “Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba”.

Umeona?..Kumbe! sisi tumeumbwa kwa Mfano wa Mungu, Nyuso zetu ni nyuso za Mungu, na kama tumeumbwa kwa mfano na Sura ya Mungu basi ni wazi kuwa sisi (yaani miili yetu na roho zetu) ni mali ya Mungu na si yetu! na hivyo ni LAZIMA TUMPE MUNGU VILIVYO VYAKE…Biblia inasema hivyo kuwa sisi si mali yetu wenyewe..

1Wakorintho 6:19  Au hamjui ya kuwa mwili wenu ni hekalu la Roho Mtakatifu aliye ndani yenu, mliyepewa na Mungu? WALA NINYI SI MALI YENU WENYEWE

Na tena inasema Miili yetu ni MALI INAPASWA ITOLEWE KWA BWANA..

1Wakorintho 6:13  “Vyakula ni kwa tumbo, na tumbo ni kwa vyakula; lakini Mungu atavitowesha vyote viwili, tumbo na vyakula. LAKINI MWILI SI KWA ZINAA, BALI NI KWA BWANA, naye Bwana ni kwa mwili”

Hiyo ikiwa na maana kuwa ni lazima tuitoe miili yetu kwa Bwana, ni lazima tumpe MUNGU vilivyo vyake, Tusipofanya hivyo tutakuwa tunafanya makosa makubwa sana..

Sasa tunampaje Mungu vilivyo vyake?

1.KWA KUOKOKA!

Kuokoka maana yake ni kumkabidhi Bwana roho zetu, kwa kutubu dhambi na kubatizwa kwa maji na kwa Roho.(Marko 16:16). Unapomwamini Bwana Yesu na kumkabidhi maisha yako, hapo umempa Mungu vilivyo vyake, na hivyo utakuwa umeyafanya mapenzi ya Mungu.. kwasababu Utu wako wa ndani umeumbwa kwa mfano wake.

2. KWA KUJITENGA NA DHAMBI.

1Wakorintho 6:13  “…LAKINI MWILI SI KWA ZINAA, BALI NI KWA BWANA, naye Bwana ni kwa mwili” Hapa maandiko yanaonesha dhahiri kuwa “mwili si kwa zinaa bali kwa Bwana ” maana yake mtu anayefanya zinaa inaiharibu mali ya Mungu, ambayo ni mwili wake.. Kwasababu mwili wake umeumbwa kwa mfano wa MUNGU, una anwani ya Mungu!!..

Hivyo si ruhusa kuuharibu kwa zinaa, au kwa pombe, au kwa sigara, au kwa kuuandika tattoo au kwa kuuvisha jinsi mtu atakavyo (nguo za kubana au zisizo za maadili) au kwa mambo mengine yote yanayofanana na hayo..

Hivyo kwa hitimisho ni kwamba.. Vya Mungu anavyopaswa apewe ni ROHO ZETU, na MIILI YETU. Kwasababu vitu hivyo vina sura na anwani ya Mungu mwenyewe, kama vile dinari iliyokuwa na sura na anwani ya Kaisari.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Nini maana ya tumeumbwa kwa mfano na sura ya Mungu?

Tofauti kati ya mtu na mwanadamu ni ipi?

Naomba kufahamu maana ya “sura ya kijiti” katika Marko 12:26.

Makerubi wenye sura nne, ni kweli wapo? na je! wanyama wataenda mbinguni?

Nuru yetu inapaswa iangaze au isiangaze kulingana na Mathayo 5:16 na Mathayo 6:1?

Rudi nyumbani

Print this post

WALA HAKUSIMAMA MTU PAMOJA NAYE, YUSUFU ALIPOJITAMBULISHA KWA NDUGUZE

Mwanzo 45:1 “Hapo Yusufu hakuweza kujizuia mbele yao wote waliosimama karibu naye. Akapiga kelele, na kusema, Mwondoeni kila mtu mbele yangu. Wala hakusimama mtu pamoja naye, Yusufu alipojitambulisha kwa nduguze.  2 Akapaza sauti yake akalia, nao Wamisri wakasikia. Watu wa nyumba ya Farao nao wakasikia.  3 Yusufu akawaambia ndugu zake, Mimi ndimi Yusufu; baba yangu angali hai bado? Wala ndugu zake hawakuweza kumjibu, maana waliingiwa na hofu mbele yake”.

Nakusalimu katika jina kuu sana la mwokozi wetu Yesu Kristo.

Yusufu baada ya kuuzwa na ndugu zake kwa watu wa mataifa, akidhaniwa kuwa ndio habari yake imeishia pale, lakini kama tunavyoifahamu habari, mambo yalikuwa ni kinyume chake, badala ya kuwa mtumwa akawa msaada na nguzo kubwa sana sio kwa wa-Misri peke yao bali pia kwa dunia nzima.

Lakini nachotaka tuone leo, ni ile siku alipojitambulisha kwa ndugu zake, ambao hawakumtambua siku zote ijapokuwa alikuwa ni ndugu yao kabisa wa damu, utaona  siku hiyo Yusufu hakujidhihirisha mbele ya kila mtu tu ilimradi, hakujidhihirisha mbele ya watu wake Misri waliompokea, bali aliwaondoa kwanza wote, akabaki yeye kama yeye pamoja na wale ndugu zake 11 tu.

 Ulishawahi kujiuliza ni kwanini iwe vile? Kwani kuna ubaya gani yeye kujifunua mbele ya kila mtu?..Kulikuwa hakuna ubaya wowote, lakini upo ufunuo mkubwa sana nyuma yake, kuhusiana na mpango wa wokovu wa Mungu.

Kibiblia habari ya Yusufu ni picha halisi ya Bwana wetu Yesu Kristo. Yeye alipokuja  duniani  kama mfalme, biblia inasema watu wake (Wayahudi), hawakumkubali, bali kinyume chake ndio wakamuua, ili tu asiwe mfalme wao.

Yohana 1:11  “Alikuja kwake, wala walio wake hawakumpokea”

Lakini neema walioikataa ilipohubiriwa kwetu sisi (watu wa mataifa), tuliipokea kwa shangwe, na ndio maana tunaona mpaka sasa Bwana Yesu ndio msingi na ngome ya mataifa yote ulimwenguni. Lakini cha ajabu ni kwamba Yesu ambaye alitoka kwa wayahudi, mpaka sasa hawamtambui, ijapokuwa miaka 2000, inakaribia kuisha.. Bado hawaoni kuwa huyu Yesu ndiye tegemeo la dunia yote, wala hakutakuwa na masihi mwingine atakayekuja kuwaokoa zaidi ya huyo. Hilo hawalioni, ukienda kumuhubiria sasa Rabi wa kiyahudi habari za Yesu, anakuona kama wewe ni kafiri.

Lakini maandiko yanatabiri kuwa, wakati wao wa kurudiwa tena utafika, na Yesu atajitambulisha kwao kwa mara nyingine, macho ya mioyo yao yatatiwa Nuru, wakati huo, wayahudi wote, watalia na kuomboleza kwa maombolezo makuu pale Israeli, watalia sana ni kwanini walimsulibisha Bwana wao na mfalme wao, waliyekuwa wanamsubiria..

Zekaria 12:10 “Nami nitawamwagia watu wa nyumba ya Daudi, na wenyeji wa Yerusalemu, roho ya neema na kuomba; nao watamtazama yeye ambaye walimchoma; nao watamwombolezea, kama vile mtu amwombolezeavyo mwanawe wa pekee; nao wataona uchungu kwa ajili yake, kama vile mtu aonavyo uchungu kwa ajili ya mzaliwa wake wa kwanza. 

11 Siku hiyo kutakuwa na maombolezo makuu huko Yerusalemu, kama maombolezo ya Hadadrimoni katika bonde la Megido.  12 Nayo nchi itaomboleza, kila jamaa peke yake; jamaa ya nyumba ya Daudi peke yao, na wake zao peke yao; jamaa ya nyumba ya Nathani peke yao, na wake zao peke yao; 

13 jamaa ya nyumba ya Lawi peke yao, na wake zao peke yao; jamaa ya nyumba ya Shimei peke yao, na wake zao peke yao.  14 Jamaa zote zilizosalia, kila jamaa peke yake, na wake zao peke yao”.

Hapo ndipo neema itarudi Israeli, ambapo inafananishwa ni lile tendo la Yusufu kujifunua tena kwa ndugu zake na kumtambua..Wakalia pamoja.

Lakini kabla hayo yote hayajatokea,  ni sharti kwanza, watu wa nyumbani mwa Yusufu “WAONDOLEWE”.

Yusufu hawezi, kuwahudumia wote wawili kwa mpigo..Alikuwa na utaratibu wake. Na ndivyo hata Kristo atakavyofanya pindi neema inarudi Israeli, sisi watumishi wake, (tulio katika mataifa), atatuondoa kwanza, kwa tukio lijulikanalo kama unyakuo, ndio ajifunue kwa Israeli.

Ndugu yangu, kama hujui mpango huu wa Mungu ni kwamba  mpaka sasa Israeli imeshakuwa taifa tangu 1948, ni taifa huru linalojitegemea, na hivi karibuni neema hii ya injili itarejea kwao. Hivyo mimi na wewe hatuna muda mwingi, Unyakuo upo karibu, tunachokisubiria hapa ni parapanda tu, hakuna kingine, dalili zote Yesu alizozisema zimeshatimia,(hilo kila mtu anajua) Kama unadhani, dunia itaendelea kuwepo kwa miaka mingine elfu, hilo wazo lifute,

Ikiwa unyakuo utapita leo, maana yake ni kuwa hii dunia itakuwa imebakiwa na miaka saba(7) tu mpaka iishie, na ndani ya hicho kipindi, Israeli itampokea Kristo, kisha mpinga-Kristo atanyanyuka mahususi kupigana nao, na baada ya hapo, Mungu ataiadhibu hii dunia kwa wote watakaopokea chapa ya Mnyama.  Kisha Bwana atawaokoa watu wake Israeli, kwa kurudi kwake mara ya pili duniani, na dunia itakuwa imeisha.

Ndugu yangu, angalia maisha yako, angalia unapoelekea, angalia mpango wa Mungu ulivyojidhihirisha wazi mbele yetu, utaendelea mpaka lini kudumu katika dhambi? Au katika maisha ya uvuguvugu?. Ikiwa hujazaliwa mara ya pili ni heri ufanye hivyo sasa katika hichi kipindi kifupi tulichobakiwa nacho. Na mtu anazaliwa mara ya pili kwanza kwa kutubu dhambi zake kwa kumaanisha kuziacha, na pili kwa kubatizwa katika ubatizo sahihi wa maji mengi, na kwa jina la Yesu Kristo, na mwisho kupokea Roho Mtakatifu.

Hivyo ikiwa utahitaji msaada ya Toba, au ubatizo sahihi wa maji mengi, basi wasiliana nasi kwa namba zetu hizi nasi tutakusaidia.

Bwana akubariki.

Maran Atha.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

WATAMTAZAMA YEYE AMBAYE WALIMCHOMA; NAO WATAMWOMBOLEZEA.

SIKU YA TAABU YA YAKOBO.

MZEITUNI HALISI UTAKAPOPACHIKWA.

ALIPO NA ATAKAPOKUWEPO BIBI-ARUSI WA YESU KRISTO.

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

MIHURI SABA

UNAWAZA NINI SASA, JUU YA UFALME WA MBINGUNI?

Rudi nyumbani

Print this post

WEWE U MUNGU UONAYE.

Mafundisho maalumu kwa ajili ya waajiriwa: Sehemu 1

Wewe U Mungu uonaye

Kwa kuwa tupo katika huu ulimwengu, na hivyo Bwana ametuagiza tufanye kazi za mikono (kwa sisi ambao hatuna huduma ya kudumu madhabahuni kwa Bwana).  tumeona ni vema pia tuwe na madarasa, ambayo, yatatupa mwongozo, wa namna ya kuishi katika maisha ya kazi. Na kama tujuavyo, kazi imegawanyika katika makundi mawili

  1. Ya Kujiajiri
  2. Ya Kuajiriwa

Lakini, watu wengi wameangukia sana katika hilo kundi la pili(Yaani kuajiriwa). Hivyo leo tutaangazia hapo. Kazi ya kuajiriwa maana yake ni kuwa ni sharti mtu awekwe chini ya mwajiri (Boss) wake. Tutatazama kimaandiko, migogoro inayotokea mara nyingi katika kazi za kuajiriwa.

Watu wengi ukiwauliza, shida ni nini? Mbona huna raha na kazi yako? Watakuambia shida ni boss wangu, mwingine atasema haniamini, mwingine atasema ananionea wivu, mwingine atasema ni mbinafsi sana, anawapandisha wengine cheo hanipandishi mimi,mwingine atasema hatujali wafanyakazi, n.k. n.k.

Lakini  wewe kama mkristo hupaswi umfikirie kiongozi wako, kwa jicho hilo, kwasababu, hata kama kweli anazo hizo tabia zinazokukwamisha, bado hawezi kuzuia kufanikiwa yako, au maono ambayo Mungu amekuwekea mbele yako.

Embu tutafakari kile Kisa cha Sarai na kijakazi wake Hajiri..Biblia inasema Sarai mwenyewe ndiye, aliyemwambia mumewe Abramu, amwingilie kijakazi wake ili ampatie uzao.. Wazo hilo halikuwa la Hajiri wala Abramu,. Kwa namna nyingine tunaweza kusema, Sarai alikusudia kumpandisha cheo kijakazi wake Hajiri, aonekane na yeye kama ni sehemu ya wake wa Ibrahimu.

Lakini mambo yalikuja kubadilika mbeleni, Hajiri alipoonekana ana mimba, Sarai akaanza kumtesa mama Yule. Na sababu ya kumtesa sio kwamba alimwonea wivu, hapana, bali aliona tabia za Hajiri zimebadilika ghafla hataki tena kuishi kama kijakazi bali anataka kuishi kama mke-mwenza, akiambiwa na Sarai aoshe vyombo anasema embu, niache hujui kama mimi ni mzazi!.

Hivyo Sarai kuona vile akaanza kumtesa, na kufadhaisha, mpaka uzalendo ukamshinda,Yule binti, ikabidi akimbilie jangwani huko akafie mbali. Lakini akiwa njiani, malaika alimtokea, akamwambia unakwenda wapi, akasema ninamkimbia bibi yangu Sarai kwasababu ananitesa nusu aniue,..Malaika akamwambia, Rudi kwa boss wako UKANYENYEKEE..

Tuisome habari..

Mwanzo 16:1 “Basi Sarai mkewe Abramu hakumzalia mwana, naye alikuwa na mjakazi, Mmisri, jina lake Hajiri.  2 Sarai akamwambia Abramu, Basi sasa, Bwana amenifunga tumbo nisizae, umwingilie mjakazi wangu labda nitapata uzao kwa yeye. Abramu akaisikiliza sauti ya Sarai.  3 Sarai mkewe Abramu akamtwaa Hajiri Mmisri mjakazi wake, baada ya kukaa Abramu katika nchi ya Kanaani miaka kumi, akampa Abramu mumewe, awe mkewe.  4 Basi akamwingilia Hajiri, naye akapata mimba. Naye alipoona ya kwamba amepata mimba, bibi yake alikuwa duni machoni pake.  5 Sarai akamwambia Abramu, Ubaya ulionipata na uwe juu yako; nimekupa mjakazi wangu kifuani mwako, naye alipoona kwamba amepata mimba, mimi nimekuwa duni machoni pake. Bwana na ahukumu kati ya mimi na wewe.  6 Naye Abramu akamwambia Sarai, Tazama, mjakazi wako yu mkononi mwako, mtendee lililo jema machoni pako. Sarai akamtesa, naye akakimbia kutoka mbele yake.  7 Malaika wa Bwana akamwona kwenye chemchemi ya maji katika jangwa, chemchemi iliyoko katika njia ya kuendea Shuri.  8 Akamwambia, Hajiri, wewe mjakazi wa Sarai, unatoka wapi, nawe unakwenda wapi? Akanena, Nakimbia mimi kutoka mbele ya bibi yangu Sarai.  9 Malaika wa Bwana akamwambia, Rudi kwa bibi yako, UKANYENYEKEE CHINI YA MIKONO YAKE.  10 Malaika wa Bwana akamwambia, Hakika nitauzidisha uzao wako, wala hautahesabika kwa jinsi utakavyokuwa mwingi.  11 Malaika wa Bwana akamwambia, Tazama! Wewe una mimba, utazaa mwana wa kiume, nawe utamwita jina lake Ishmaeli, maana Bwana amesikia kilio cha mateso yako.  12 Naye atakuwa kama punda-mwitu kati ya watu, mkono wake utakuwa juu ya watu wote na mkono wa watu wote utakuwa juu yake, naye atakaa mbele yao ndugu zake wote.  13 Akaliita jina la Bwana aliyesema naye, WEWE U MUNGU UONAYE, kwani alisema, Hata hapa nimemwona yeye anionaye”?

Tafakari kwa umakini hiyo habari..

Rudi ukanyenyekee, Mungu anajua kuwa unateswa, lakini wakati mwingine ni kwasababu ya kukosa  kwako unyenyekevu..Rudi, kwasababu Baraka zako haziwezi kuzuiliwa na  mtu yeyote kama mtoto utazaa tu, naye atakuwa taifa kubwa..Na kweli Hajiri akatii, japo hapo mwanzo alidhani kuwa Mungu haoni mateso yake..lakini hapa mpaka akasema, hakika  “Wewe U Mungu uonaye”

Ndugu uliyeajiriwa, hakuna mtu anamchukia “mnyenyekevu”, usishindane na boss wako, hata kama ni mkali, wala usimkimbie, ukaacha kazi kwasababu za chuki, na fitina n.k., unaweza usipate nyingine nzuri kama hiyo.. bali kuwa tu mtulivu, kwasababu “Yupo aonaye”..Ukidhulumiwa mshahara “Yupo aonaye”.. Baraka zako zipo palepale. Yusufu alinyanyuliwa visa na boss wake wa kike, akawekwa gerezani, lakini mwisho wake tunaujua.

Hivyo zingatia hilo kama mkristo, katika maisha ya kuajiriwa,kuwa mnyenyekevu, ili uifurahie kazi yako.

 na Bwana atakubariki.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Biblia inasemaje kuhusu Kazi?

JINSI MUNGU ATAKAVYOTOA THAWABU ZAKE, NA VIGEZO ATAKAVYOTUMIA. (Sehemu ya 3)

Biblia inapotumia neno “Bila kazi ya mikono”, ina maana gani?

USIISHI BILA KUIFANYA KAZI YA MUNGU KABISA..

Moyo wake mwenye hekima upo upande wa kuume, maana yake nini?

Maji ya Zamzam yapo kibiblia?

JE! UNAMPENDA BWANA?

MIEZI 13 YA KIYAHUDI.

Rudi nyumbani

Print this post

USIIKARIBIE DHAMBI, KAA NAYO MBALI.

Je unajua kwamba kuikaribia dhambi ni “DHAMBI”, Hata tu kabla ya kuifanya?.

Mungu hakumpa tu Adamu maagizo ya kutokula yale matunda ya mti wa katikati…bali  pia alimwambia “Asiyaguse yale matunda”..asije akafa. Wengi wetu tunaona tu habari ya “kula” kama kosa, lakini hatujui kuwa  Mungu aliwaagiza kwamba hata kuyagusa wasiyaguse, (maana yake wakae mbali nayo).

Mwanzo 3:2 “Mwanamke akamwambia nyoka, Matunda ya miti ya bustanini twaweza kula;

3 lakini matunda ya mti ulio katikati ya bustani Mungu amesema, Msiyale wala MSIYAGUSE, msije mkafa”.

Kumbe hata wangeyagusa tu yale matunda bila hata ya kuyala, bado Wangekufa!!.

Hii ni hatari sana..na inatupa fundisho kubwa sana..

Kwanini Mungu akataze wasiyaguse?..Je kuna ubaya wowote katika kuyagusa???… Jibu ni ndio!… kwasababu chanzo cha dhambi ya kula tunda ni kulishika lile tunda kwanza, (Hawa asingeweza kulipeleka mdomoni kabla ya kulishika) kabla ya kulichunguza chunguza kwanza, kabla ya kulidadisi dadisi, ndipo akaangukia katika ushawishi wa kulila.

Hivyo Mungu aliona chanzo cha dhambi kuwa ni “kushika” ndipo akatoa maagizo kwamba WASIYAGUSE!! Wasije wakafa… lakini wenyewe (Waligusa, na tena wakala) Hivyo ikawa ni makosa mawili yaliyozaa Mauti kamilifu.

Na hata leo Bwana anatuonya tukae mbali na dhambi, tusiikaribie kabisa dhambi, tusiiguse dhambi licha ya kuitenda!!..

Tukae mbali na Wizi kama ya wizi wenyewe kutendeka,…tukae mbali na  Ulevi kabla ya ulevi wenyewe kutendeka… tukae mbali na Utukanaji, Uadui, Kiburi, Uasherati, kabla ya kufanya mambo hayo (Wagalatia 5:19-20)… Tusizikaribie kabisa hizi dhambi!!.. tukae nazo mbali maili nyingi sana, kwasababu kitendo cha kuzikaribia tu tayari ni kosa..

leo hii utaona mtu anasema  hazini, wala hafanyi uasherati lakini katika simu yake kumejaa picha zinazochochea mambo hayo, kumejaa miziki inayochochoea mambo hayo, kumejaa filamu zi kidunia zenye maudhui hayo ya kiasherati, simu yake imejaa magroup ya mizaha, na uhuni, unaochochea mambo hayo…pasipo kujua kuwa anafanya makosa makubwa kuisogelea dhambi kwa namna hiyo..

Neno la Mungu linasema kwamba tuikimbie zinaa, sio tuishi nayo, au tuikemee!..bali tuikimbie (Soma 1Wakorintho 6:18 )...kama vile Yusufu alivyoikimbia mbele ya mke wa Potifa, na sisi tunapaswa tuikimbia hivyo hivyo Yusufu hata hakukubali kuzungumza na Yule mwanamke..

Lakini ni kinyume chake katika siku hizi za mwisho, utaona binti anayekiri kumpokea Yesu anapiga maneno na mwanaume anayemtaka, kijana anayekiri kumpokea Yesu anapiga maneno ya kidunia na binti anayemtamani, na hata kufanya naye mizaha..Hii ni hatari kubwa!, kumbuka ushawishi wa Hawa kula tunda haukuanzia mdomoni bali mkononi!..baada ya kulishika ndipo ushawishi ukamwingia..

Na sisi tukijishikamanisha na dhambi, basi ni lazima tutazitenda tu!, haijalishi itachukua muda gani ni lazima tutazitenda tu!…Hauwezi kusema umeacha utukanaji, lakini kila kukicha kampani zako ni za watu wanaotukana…ni lazima tu na wewe utatukana, haijalishi itakuchukua muda gani kudumu bila kutukana lakini mwisho wa siku utaishia kurudia matukano tu.

Hauwezi kukaa unasikiliza usengenyaji na wewe usiwe msengenyaji..ni suala la muda tu!, utajikuta na wewe upo kama wao.. Kumbuka Adamu na Hawa waliambiwa “wasiukaribie kabisa ule mti, na hata kuugusa”.. Vile vile na sisi leo hii tunapaswa tusiikaribie miti ya dhambi…wala tusiguse mashina yake wala matawi yake.. maana kugusa ndio chanzo cha kula..

Bwana atusaidie na kutuwezesha katika yote.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

MWENDO UNAOSHANGAZA SANA!

MUME / MKE BORA KUTOKA KWA BWANA UTAMWONA UKIWA KATIKA MAZINGIRA GANI?

HUJAPEWA MBAWA ZA KUKIMBIA MATATIZO

FANYA MAAMUZI KABLA HAZIJAKARIBIA SIKU ZA HATARI.

Mambo yale yaliyo mbali, na yale yaendayo chini sana,

Rudi nyumbani

Print this post

Kuna tofauti gani kati ya  “Edeni” na “Adeni”?

Nini tofauti kati ya Bustani ya Edeni (Mwanzo 2:8) na bustani ya Adeni (Ezekieli 28:13 na  Yoeli 2:3)

Jibu:Tusome

Mwanzo 2:8 “Bwana Mungu akapanda bustani upande wa mashariki wa EDENI, akamweka ndani yake huyo mtu aliyemfanya”.

Isaya 51:3 “Maana Bwana ameufariji Sayuni; amepafariji mahali pake palipokuwa ukiwa; amefanya jangwa lake kuwa kama BUSTANI YA EDENI, na nyika yake kama bustani ya Bwana; furaha na kicheko zitaonekana ndani yake, kushukuru, na sauti ya kuimba”. 

Hapa tunaona ikitajwa bustani ya “Edeni” lakini tukisoma mahali pengine tunaona ikitajwa bustani nyingine ya “Adeni”

Ezekieli 28:13 “Ulikuwa ndani ya ADENI, bustani ya Mungu; kila jiwe la thamani lilikuwa kifuniko chako, akiki, na yakuti manjano, na almasi, na zabarajadi, na shohamu, na yaspi, na yakuti samawi, na zumaridi, na baharamani, na dhahabu; kazi ya matari yako na filimbi zako ilikuwa ndani yako; katika siku ya kuumbwa kwako zilitengenezwa tayari”

Yoeli 2:3 “Moto unakula mbele yao; na nyuma yao miali ya moto inateketeza; hiyo nchi inafanana na BUSTANI YA ADENI mbele yao, na nyuma yao imekuwa jangwa tupu; naam, hakuna aliyeokoka asipatikane nao”.

Na pia katika Ezekieli 31:9, Ezekieli 31:16-18, na  Ezekieli 36:35 utaona ikitajwa Adeni na si Edeni, swali je kuna utofauti wowote?

 Jibu ni la! hakuna utofauti wowote iliyopo kati kati ya “Adeni” na “Edeni”, hayo ni maneno mawili yenye maana moja, sehemu moja biblia imetaja Edeni, sehemu nyingine Adeni lakini maana ni ile ile..Na maana ya neno Edeni au Adeni ni “paradiso ya raha”.

Mungu alipoiumba dunia, alimweka mwanadamu wa kwanza katika bustani ya Edeni, na alikusudia mahali pale pawe Paradiso yake ya milele. Dunia yote ilikuwa ni nzuri, lakini pale Edeni palikuwa ndio kitovu cha utukufu wa mwanadamu.

Lakini baada ya shetani kumdanganya Hawa, ndipo Uovu ukaingia na kusababisha mwanadamu kuondolewa katika bustani ile, na Mungu kuitowesha kabisa!

Lakini Bwana ameahidi kuumba Mbingu Mpya na Nchi mpya (Isaya 65:17), ambayo itakuja baada ya utawala wa miaka elfu kuisha hapa duniani. Katika mbingu mpya na nchi mpya, Bwana ametuandalia mambo mazuri kuliko yaliyokuwepo Edeni, maandiko yanasema jicho halijawahi kuona wala sikio kusikia mambo ambayo Mungu kawaandalia wale wampendao..(1Wakorintho 2:9).

Lakini ahadi hiyo kulingana na Neno lake ni kwa wale waliomwamini Yesu Kristo na kuoshwa dhambi zao kwa damu yake.

Je umempokea Yesu?..kama bado unasubiri nini?. Mwamini leo na ukabatizwe katika ubatizo na ujazwe Roho Mtakatifu kulingana na Matendo 2:38.

Maran atha.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Bustani ya Edeni ipo nchi gani?

EDENI YA SHETANI:

Je! Ni kweli Yesu alirejesha kila kitu kama pale Edeni?

MBINGU MPYA NA NCHI MPYA. (Sehemu ya 1)

MIGAWANYO MINNE (4), YA HUDUMA YA YESU.

Rudi nyumbani

Print this post