Makerubi wenye sura nne, ni kweli wapo? na je! wanyama wataenda mbinguni?

Makerubi wenye sura nne, ni kweli wapo? na je! wanyama wataenda mbinguni?

SWALI: Wale  Makerubi wenye sura nne, ni kweli wapo au ni mfano wa picha tu? Na je! wanyama wataenda mbinguni?


Jibu: Awali ya yote ni muhimu kufahamu kuwa viumbe vyote na kila kitu tunachokiona duniani kimeumbwa kwa taswira ya viumbe na vitu vya mbinguni.

Kuanzia mwanadamu mpaka wanyama, ndege pamoja na mimea na vito, vyote vimeumbwa kwa taswira ya vitu vya mbinguni… Isipokuwa vya mbinguni vina utukufu mwingi kuliko vya duniani.

Kwamfano tukianza na mwanadamu.. Maandiko yanasema kaumbwa kwa “sura na mfano wa Mungu”.. Maana yake kimwonekano, mwanadamu anafanana na Mungu, lakini si Mungu.

Kadhalika tukimtazama ng’ombe, simba na tai.. Nyuso zao hizo zimeumbwa kwa taswira ya aina fulani ya malaika waliopo mbinguni, wajulikanao kama Makerubi.. Kwasababu Makerubi wana nyuso Nne, maandiko yanasema hivyo.

Ufunuo 4:6 “Na mbele ya kile kiti cha enzi kulikuwa na mfano wa bahari ya kioo, kama bilauri; na katikati ya kile kiti cha enzi, na pande zote za kile kiti, WALIKUWAKO WENYE UHAI WANNE, wamejaa macho mbele na nyuma.

7 NA HUYO MWENYE UHAI WA KWANZA ALIKUWA MFANO WA SIMBA; NA MWENYE UHAI WA PILI ALIKUWA MFANO WA NDAMA; NA MWENYE UHAI WA TATU ALIKUWA NA USO KAMA USO WA MWANADAMU; NA MWENYE UHAI WA NNE ALIKUWA MFANO WA TAI ARUKAYE”.

Kadhalika wapo farasi wa kimbinguni, (Ufunuo 19:14) na wapo wa kiduniani.. na vile vile vipo vito vya kimbinguni na vya kiduniani..

Kwahiyo, tukirudi kwenye swali letu? Je ni mbinguni wapo kweli wale wenye uhai wanne?, jibu ni ndio wapo! na si nadharia tu!.. tukifika huko tutawaona.. Nabii Ezekieli aliwaona kwenye maono, Yohana naye aliwaona na sisi pia tutawaona.

Na kama hivyo ndivyo, je wanyama nao wataenda mbinguni?

Jibu ni hapana! Hakuna Twiga, wala mbwa, wala simba, wala ng’ombe wala tai arukaye, atakayeenda mbinguni.. Hivyo vyote ni viumbe vya kidunia.. vimeumbwa kutoka mavumbini, na havina nafsi iliyo hai.. maana yake vikifa vimekufa vinarudi mavumbini, havina ufufuo..Na mavumbi hayawezi kuingia mbinguni.

Ni mwanadamu peke yake aliye na ahadi ya kuingia mbinguni, (Na si wanadamu wote bali wale waliooshwa dhambi zao kwa damu ya Mwanakondoo) ambapo siku ya unyakuo itakapofika watafufuliwa na kisha kuvaa miili ya kimbinguni, lakini hawataingia mbinguni na hii miili ya mavumbi.. bali watabadilishwa na kuvikwa ya kimbinguni.

1Wakorintho 15:50 “Ndugu zangu, nisemayo ni haya, ya kuwa nyama na damu haziwezi kuurithi ufalme wa Mungu; wala uharibifu kurithi kutokuharibika.

51 Angalieni, nawaambia ninyi siri; hatutalala sote, lakini sote tutabadilika,

52 kwa dakika moja, kufumba na kufumbua, wakati wa parapanda ya mwisho; maana parapanda italia, na wafu watafufuliwa, wasiwe na uharibifu, nasi tutabadilika.

53 Maana sharti huu uharibikao uvae kutokuharibika, nao huu wa kufa uvae kutokufa”.

Sasa wanyama wenyewe hawana hiyo ahadi ya kufufuliwa na kuvikwa miili ya utukufu, na wala Kristo hajawafia wao.. ndio maana unaona hakuna mahali popote katika maandiko, inayoonyesha mfano wa mnyama yoyote kufufuliwa.

Na kama wapo wanadamu tu ambao wataikosa mbingu.. mnyama ni nani aweze kuingia?

Waliokombolewa kwa damu ya mwanakondoo, hao peke yao ndio walioahidiwa kwenda mbinguni.. lakini wanadamu wengine wote, ikiwemo wanyama na miti, na nzige, na bakteria hawana nafasi mbinguni..wakifa wamekufa, kama vile mti ukifa unavyopotea, hauna ufufuo wowote.

Sehemu pekee ambayo maandiko yanasema wanyama watakuwepo, ni katika ule utawala wa miaka elfu, hapa duniani tutakapotawala na Kristo. Huko ndiko wanyama watakuwepo. Kwa maelezo marefu kuhusu utawala huu unaweza  kuupata kupitia hapa > Utawala wa miaka elfu

Lakini itoshe kusema tu kwamba! Mbinguni hakitaingia kinyonge

Ufunuo 21:27 “Na ndani yake hakitaingia kamwe cho chote kilicho kinyonge, wala yeye afanyaye machukizo na uongo, bali wale walioandikwa katika kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo”.

Je na wewe unafanya machukizo? Je umeokoka?.. kama bado basi fahamu kuwa hutakwenda mbinguni, kwasababu huko haviingi vinyonge na wafanyao machukizo, huko hawaingii waasherati, walevi, wazinzi, watu wanaoupenda ulimwengu kuliko kumpenda Mungu.. n.k

Hivyo mpokee Yesu leo, uoshwe dhambi zako, ili uwe na uhakika wa kuingia mbinguni katika makao ya furaha ya daima.

Unyakuo upo karibu na Bwana yuaja.


Mada Nyinginezo:

Naomba kufahamu maana ya “sura ya kijiti” katika Marko 12:26.

Biblia inamaanisha nini inaposema “Mwenye haki huufikiri uhai wa mnyama wake”?

Je! Kuna malaika wangapi mbinguni?

HEKIMA YA KIMUNGU, INAINGIAJE MIOYONI MWETU?

Bahari mbalimbali zilizoorodheshwa kwenye biblia.

Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments