Kisima cha joka na lango la jaa ni nini?(Nehemia 2:13)

Kisima cha joka na lango la jaa ni nini?(Nehemia 2:13)

SWALI:Bwana Yesu asifiwe naomba kuelewa “Kisima cha joka”  na “lango la jaa” vina maana gani kama tunavyosoma katika Nehemia 2:13


JIBU: Nehemia alipopata taarifa juu ya uharibifu wa mji wa Yerusalemu, alifunga na kumwomba Mungu kwa muda mrefu, ili aende kuujenga tena mji huo, ndipo Mungu akasikia maombi yake na kumfungulia mlango wa kwenda Israeli kwa ajili ya kazi hiyo ya ukarabati.

Sasa kama tunavyosoma alipofika,hakusubiri sana, bali aliondoka usiku wa tatu yeye ni baadhi ya watu wachache, ili kuuchunguza kwanza mji, jinsi kuta zake zilivyoharibiwa. Na kati ya sehemu tano (5) alizopita mojawapo ilikuwa ni hapo penye kisima cha joka, na lango la jaa.

Kisima cha joka: Ni kisima kilichokuwa kando ya kuta za mji, kinaaminika, kiliitwa hivyo kutokana na umbile la mdomo wake jinsi ulivyofanana na nyoka., japo wengine wanaamini kuwa hapo kale kilitumiwa na wapagani kwa ajili ya miungu yao ya majini, waliyoitambua kwa jina la joka. Hivyo jina la kisima hicho liliendelea kuwa hilo hadi wakati wa baadaye, Japo hilo halijathibitishwa ni kulingana tu na mapokeo kwasababu biblia haijaeleza sababu ya kuitwa vile.

Lango la Jaa: Jaa kwa jina lingine ni jalala, hivyo, lango hili lilitumika kutolea uchafu wote wa mji (kinyesi). Huko nako Nehemia alifika.

Nehemia 2:11 Basi nikafika Yerusalemu, nikakaa huko muda wa siku tatu.

12 Kisha nikaondoka usiku, mimi na watu wachache pamoja nami; wala sikumwambia mtu neno hili alilolitia Mungu wangu moyoni mwangu, nilitende kwa ajili ya Yerusalemu; wala hapakuwa na mnyama pamoja nami, ila mnyama yule niliyempanda mwenyewe.

13 Nikatoka nje usiku, kwa njia ya LANGO LA BONDENI, nikashika njia IENDAYO KISIMA CHA JOKA, na LANGO LA JAA; nikazitazama kuta za Yerusalemu, zilizokuwa zimebomoka; na malango yake yameteketezwa kwa moto.

14 Kisha nikaendelea mpaka lango la chemchemi, na ziwa la mfalme; lakini hapakuwa na nafasi ya kupita kwa yule mnyama aliyekuwa chini yangu.

15 Kisha nikapanda usiku kando ya kijito, nikautazama ukuta; kisha nikarudi nyuma, nikaingia kwa lango la bondeni, nikarejea hivyo.

Lakini  baada ya hayo yote tunaona, Nehemia haraka na mapema alianza ujenzi wa kuta za mji. Na kazi ikaja kukamilika kwa ufasaha wote,licha ya kupitia vipingamizi na vikwazo vingi kutoka kwa maadui zao.

Ni ujumbe gani tunaupata kutoka katika mawazo hayo ya Nehemia?

Ni kwamba hatuwezi kukarabati kitu bila kujua uharibifu wake upo wapi. Ni jinsi gani wakristo, tunapaswa tufumbue macho yetu tuone, uharibifu shetani aliousababisha kwenye kazi ya Mungu, jinsi watoto wanavyoharibiwa, jinsi vijana walivyopotoka kila kukicha, jinsi maasi yanavyoendelea kanisani.., Tukiyaona hayo hapo ndipo wote kwa pamoja tutaona sababu ya kumtumikia Mungu, kwa ushirikiano.

Vinginevyo tutaona kila siku mambo yote ni sawa tu, kama wale watu wa Mji Nehemia alivyowakuta wame RELAX.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Jaa ni nini katika biblia?

“Shinikizo” ni nini kibiblia, Na maana yake rohoni ni ipi?

Nini maana ya Dirii, Chepeo na Utayari?

Jehanamu ni nini?

UFUNUO: Mlango wa 12

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments