Moyo wake mwenye hekima upo upande wa kuume, maana yake nini?

Moyo wake mwenye hekima upo upande wa kuume, maana yake nini?

SWALI: Nini maana ya huu mstari? Mhubiri 10:2 “Moyo wake mwenye hekima upo upande wa kuume; Bali moyo wake mpumbavu upo mkono wa kushoto”.


JIBU: Mstari huo unatuonyesha wazi kuwa kumbe moyo wa mwanadamu unao upande wa kukaa, haupo tu hewani bila una makao, ni aidha ukae upande wa mkono wa kuume, au upande wa mkono wa kushoto. Kumbuka moyo unaozungumziwa hapo sio huu wa nyama, bali ni ule wa rohoni ambao unaeleza tabia ya mtu.

Kama tunavyojua mkono wa kuume ni mkono wa heshima, mkono wa kuonyesha kujali, na usafi, tofauti na mkono wa kushoto, na ndio maana ukikutana na mtu yeyote mahali fulani huwezi kutoa salamu kwa mkono wa kushoto, bali utampa mkono wa kulia kuonyesha heshima, na kujali.

Vivyo hivyo na mioyo yetu, ikiwa haionyeshi Heshima, na usafi na kujali kwa Mungu na kwa wanadamu, rohoni inaonekana ipo upande wa kushoto. Na siku ile ya hukumu Mungu atatuweka upande wa mkono wake wa kushoto. Lakini tukiwa wasafi rohoni, na tunamjali Mungu na watu(hususani ndugu katika imani), siku ile Bwana atatuweka upande wa mkono wake wa kuume ambapo moyo upo.

Vifungu hivi vinaeleza wazi tabia zilizo upande wa mkono wa kuume na ule wa kushoto, Tusome;

Mathayo 25:31 “Hapo atakapokuja Mwana wa Adamu katika utukufu wake, na malaika watakatifu wote pamoja naye, ndipo atakapoketi katika kiti cha utukufu wake;

32 na mataifa yote watakusanyika mbele zake; naye atawabagua kama vile mchungaji abaguavyo kondoo na mbuzi;

33 atawaweka kondoo mkono wake wa kuume, na mbuzi mkono wake wa kushoto.

34 Kisha Mfalme atawaambia wale walioko mkono wake wa kuume, Njoni, mliobarikiwa na Baba yangu, urithini ufalme mliowekewa tayari tangu kuumbwa ulimwengu;

35 kwa maana nalikuwa na njaa, mkanipa chakula; nalikuwa na kiu, mkaninywesha; nalikuwa mgeni, mkanikaribisha;

36 nalikuwa uchi, mkanivika nalikuwa mgonjwa, mkaja kunitazama; nalikuwa kifungoni, mkanijia.

37 Ndipo wenye haki watakapomjibu, wakisema, Bwana, ni lini tulipokuona una njaa, tukakulisha, au una kiu tukakunywesha?

38 Tena ni lini tulipokuona u mgeni, tukakukaribisha, au u uchi, tukakuvika?

39 Ni lini tena tulipokuona u mgonjwa, au kifungoni, tukakujia?

40 Na Mfalme atajibu, akiwaambia, Amin, nawaambia, kadiri mlivyomtendea mmojawapo wa hao ndugu zangu walio wadogo, mlinitendea mimi.

41 Kisha atawaambia na wale walioko mkono wake wa kushoto, Ondokeni kwangu, mliolaaniwa, mwende katika moto wa milele, aliowekewa tayari Ibilisi na malaika zake;

42 kwa maana nalikuwa na njaa, msinipe chakula; nalikuwa na kiu, msininyweshe;

43 nalikuwa mgeni, msinikaribishe; nalikuwa uchi, msinivike; nalikuwa mgonjwa, na kifungoni, msije kunitazama.

44 Ndipo hao pia watajibu, wakisema, Bwana, ni lini tulipokuona wewe una njaa, au una kiu, au u mgeni, au u uchi, au u mgonjwa, au u kifungoni, tusikuhudumie?

45 Naye atawajibu, akisema, Amin, nawaambia, Kadiri msivyomtendea mmojawapo wa hao walio wadogo, hamkunitendea mimi.

46 Na hao watakwenda zao kuingia katika adhabu ya milele; bali wenye haki watakwenda katika uzima wa milele.

Umeona, hivyo Bwana atujalie tuwe na hekima, kuhakikisha kuwa mioyo yetu haipo upande wa kushoto, kwa tabia zilizoorodheshwa hapo juu.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

Shetani ni nani?

TABIA YAKO NI YA MNYAMA GANI?

JE UNAMTHAMINI BWANA?

UFUNUO: Mlango wa 1

YAKINI NA BOAZI.

Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments