Je unaruhusiwa kufanya tendo la ndoa ukiwa katika mfungo?

Je unaruhusiwa kufanya tendo la ndoa ukiwa katika mfungo?

Haya ni Mafundisho maalumu kwa ajili ya wanawake..

JIBU: Ni vema kujua mfungo ni nini na madhumuni yake ni yapi.

Mfungo ni kitendo cha kujizuia kufanya jambo fulani la lazima kwa kipindi fulani kwa lengo la kumkaribia Mungu zaidi..

Kwamfano mfungo hasaa hulenga kujizuia kula au kunywa , wengine huzuia usingizi, wengine kazi, wengine mawasiliano n.k. inategemea unalenga nini.

Hivyo pale unapojizuia kula au kunywa lengo lako ni upate utulivu wa kuwa karibu zaidi na Mungu katika maombi na kumtafakari.

Kwahiyo kwa jinsi unavyojiweka mbali zaidi na masuala ya mwili ndivyo unavyoupa zaidi mfungo wako nguvu.

Hivyo tukirudi katika swali je tunaruhisiwa kushiriki tendo la ndoa tuwapo katika mfungo? 

Jibu ni kuwa hakuna katazo lolote..kwasababu shabaha ya mfungo wako lilikuwa katika kujizuia kula au kunywa..

Lakini ikiwa utapenda kuzuia pia tendo la ndoa, ni vizuri lakini hapo ni jambo la makubaliano na mwenzi wako, ikiwa ataliridhia kwa wakati huo msafanye tendo la ndoa, ili mwelekeze fikra zenu zote kwa Bwana…hapana shida. Ni vema.

Lakini ikiwa mmoja wenu hajaridhia, hapo hupaswi kuzuia, kwasababu uolewapo au uoapo, huna amri juu ya mwili wako, isipokuwa mwenzako, kwahiyo akikataa hupaswi kupinga.Ni lazima ufanye.

Biblia inasema..

1 Wakorintho 7:3-5

[3]Mume na ampe mkewe haki yake, na vivyo hivyo mke na ampe mumewe haki yake.

[4]Mke hana amri juu ya mwili wake, bali mumewe; vivyo hivyo mume hana amri juu ya mwili wake, bali mkewe.

[5]Msinyimane isipokuwa MMEPATANA kwa muda, ili mpate faragha kwa kusali; mkajiane tena, Shetani asije akawajaribu kwa kutokuwa na kiasi kwenu.

Vilevile ikiwa nyote hamjaridhia…pia bado hakuharibu mfungo wenu.

Hivyo kwa kuhitimisha ni kuwa kushiriki tendo la ndoa, ndani ya mfungo, hakubatilishi mfungo wa mtu. Isipokuwa tu maandiko yanatuelekeza  iwe ni kwa kiasi ili mpate na muda wa kusali 

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Je unaruhusiwa kufanya tendo la ndoa ukiwa katika mfungo?

JE NI DHAMBI KUWA NA MAHUSIANO KABLA YA NDOA?

MASWALI NA MAJIBU: YAHUSUYO NDOA- Sehemu ya 2.

Pale mwanandoa mmoja anaposhindwa kutimiza wajibu wake ufanyaje?

SIKU ZA MWISHO ZA UHAI WANGU.

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments