Nuru yetu inapaswa iangaze au isiangaze kulingana na Mathayo 5:16 na Mathayo 6:1?

Nuru yetu inapaswa iangaze au isiangaze kulingana na Mathayo 5:16 na Mathayo 6:1?

Swali: Katika Mathayo 5:14 biblia inasema kuwa “Nuru yetu na iangaze mbele za Watu”, halafu tukienda kwenye Mathayo 6:1 maandiko yanasema “tusifanye wema wetu machoni pa watu”, hapa nahitaji ufafanuzi.


Jibu: Tusome

Mathayo 5:14 “Ninyi ni nuru ya ulimwengu. Mji hauwezi kusitirika ukiwa juu ya mlima.

15 Wala watu hawawashi taa na kuiweka chini ya pishi, bali juu ya kiango; nayo yawaangaza wote waliomo nyumbani.

16 VIVYO HIVYO NURU YENU NA IANGAZE MBELE YA WATU, WAPATE KUYAONA MATENDO YENU MEMA, WAMTUKUZE BABA YENU ALIYE MBINGUNI”.

Tusome pia Mathayo 6:1-2..

Mathayo 6:1 “Angalieni msifanye wema wenu machoni pa watu, KUSUDI MTAZAMWE NA WAO; kwa maana mkifanya kama hayo, hampati thawabu kwa Baba yenu aliye mbinguni.

2 Basi wewe utoapo sadaka, usipige panda mbele yako, kama wanafiki wafanyavyo katika masinagogi na njiani, ILI WATUKUZWE NA WATU

Mistari hiyo miwili haijichanganyi, isipokuwa fahamu zetu ndizo zinazojichanganya.

Bwana Yesu aliposema Nuru yetu na iangaze mbele za watu.. ni ili Mungu atukuzwe kupitia matendo yetu mema tunayoyafanya!… Lakini tukifanya jambo lolote ambalo halitamrudishia Mungu utukufu bali litatupa sisi utukufu, huo sio wema Bwana Yesu alioumaanisha kuwa tuungaze..Ndio maana hapo kwenye Mathayo 5:16 anamalizia kwa kusema.. “wapate kuyaona matendo yenu mema, WAMTUKUZE BABA YENU ALIYE MBINGUNI.”..Na sio watutukuze sisi!!!.

Lakini tunapofanya Wema huku lengo letu ni watu watupe sisi utukufu, au watusifu, au watuone ni mashuhuri, huo sio wema bali ni Ubaya uliovaa vazi la wema ndani yake.. ndio maana katika huo mstari wa 2, Bwana anaweka msisitizo kwa kusema…

Mathayo 6:2 “Basi wewe utoapo sadaka, usipige panda mbele yako, kama wanafiki wafanyavyo katika masinagogi na njiani, ILI WATUKUZWE NA WATU”.

Umeona hapo lengo la wao kufanya mema yote hayo ni ili watukuzwe na watu, na si Mungu atukuzwe kupitia wao!..Hivyo hiyo ni dhambi!..

Jambo lolote tulifanyalo lisilomrudishia Mungu utukufu hata kama liwe jema kiasi gani, mbele za Mungu ni dhambi!.

Wakati Fulani Mfalme Herode aliwafanyia Wema watu wa Tiro kwa kuwasamehe na kuwapatia riziki, na akaandaa hotuba ambayo iliwafurahisha sana watu wa Tiro, hata kufikia hatua watu hao kumtukuza kwa kusema “Sauti yake ni sauti ya Mungu na si mwanadamu!”..

Na utaona baada ya pale, Mungu alimpiga Herode kwa Chango, kwasababu hakumpa Mungu utukufu, bali alijitukuza yeye!..(Habari hiyo unaweza kuisoma katika kitabu cha Matendo 12:20-24).

Kwahiyo na sisi hatuna budi kuzipima dhamira zetu katika wema wote tunaoufanya.. Je! Lengo letu ni kumpa Mungu utukufu, au kujitukuza sisi. Kama wema tunaoufanya ni kwa lengo la Mungu kutukuzwa basi huo tuufanye kwa bidii sana kwasababu mwisho wake ni Mungu kutukuzwa, lakini kama lengo ni sisi kutukuzwa, basi tujihadhari na huo.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

NGAZI 7 AMBAZO MKRISTO NI LAZIMA AZIPANDE KUUFIKIA UKAMILIFU.

LAKINI NINYI, NDUGU, MSIKATE TAMAA KATIKA KUTENDA MEMA.

NI SAA KUMI NA MBILI (12) TU, ZA KRISTO KWAKO.

Ibada ni nini,Na je ili ikamilike inapaswa iwe na nini na nini?

IFAHAMU HUZUNI NA FURAHA YA MALAIKA.

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
3 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
M
M
2 years ago

Amina

Lucas mhula
Lucas mhula
2 years ago

Amina mtumishi asante kwa ujumbe

Emmanuel Kitengule
Emmanuel Kitengule
2 years ago

Barikiwa sana mwalimu kwa mafundisho mazuri yaletayo UZIMA,hili litaokoa wengi.