LAKINI NINYI, NDUGU, MSIKATE TAMAA KATIKA KUTENDA MEMA.

LAKINI NINYI, NDUGU, MSIKATE TAMAA KATIKA KUTENDA MEMA.

2Wathesalonike 3:13 inasema..

“Lakini ninyi, ndugu, msikate tamaa katika kutenda mema”.

Unajua mpaka biblia inakuambia usikate tamaa, inamaanisha kuwa si kitu chepesi kukishikilia wakati wote. Si kitu ambacho unaweza ukaona faida yake moja kwa moja pale unapokifanya.. Lakini katika yote hayo bado inakuambia usikate tamaa.

Ili jambo lolote liwe wema, ni lazima malipo yake yasilingane na huduma iliyotolewa. Kwamfano mtu anapokwenda kuwasaidia yatima au maskini, huo ni wema, kwasababu hawana cha kumlipa hata baada ya kuwapa mahitaji yao, au pale anapowasomesha ndugu, huo nao ni wema, kwasababu pesa hizo ungeweza kuzitumia katika mambo yake mengine lakini ameona vema, ujinyime yeye uwape wengine maarifa.. Au unapowapa wengine chakula au mavazi bila kuwachaji pesa au kuwadai kitu chochote huo ni wema.. Au unapowapa wengine maarifa ya ufalme wa mbinguni bila malipo yoyote huo nao ni wema mkuu sana n.k.

Lakini katika hayo, kuna wakati akili inaweza kukujia, ukajisikia kuchoka na kusema nimeshasaidia watu sana mbona sioni faida yoyote ya kufanya hivyo? Au mbona sioni nikirudishiwa fadhila yoyote kutoka kwao? Wacha nipunguze wema wangu, nianze kujijali mimi mwenyewe. Au nitafute mambo yangu mwenyewe.

Katika mazingira kama hayo, biblia inasema.. usichoke kutenda wema..Kwasababu ni mbegu nzuri sana ambayo unaipanda leo, lakini siku moja utavuna matunda yake ukiwa mvumilivu.

Wagalatia 6:9 “Tena tusichoke katika kutenda mema; maana tutavuna kwa wakati wake, tusipozimia roho”.

Hata kama utaona wale uliowatendea mema wamekutangulia,wewe umekuwa daraja kwao la kufika juu, au wengine wamekudharau kwa ukarimu wako, bado usichoke katika kutenda kwako, kwasababu hicho unachokipanda thamani yake ni kubwa kuliko fedha au dhahabu. Utakuja kujua vizuri utakapovuka kule ng’ambo.

Katika biblia, tunamwona, mtu mmoja aliyeitwa Mordekai, yeye alikuwa ni mlinda mlango wa mfalme, lakini siku moja baadhi ya watumishi walipanga njama ili wamuue mfalme. Mordekai alipopata habari, kwasababu alikuwa ni mtu mwema, hakukaa kimya bali alikwenda kutoa taarifa ya njama hizo, na hatimaye mfalme akanusurika kifo, lakini biblia inatuonyesha akasahaulika, muda mrefu ukapita, wala hakuna aliyekumbuka wala kujali wema wake.

Siku moja akiwa katika hatihati ya kuuliwa na adui yake aliyeitwa Hamani, biblia inatuambia usiku huo huo mfalme alikosa uzingizi kabisa, ndipo akaanza kupitia vitabu vya kumbukumbu za taarifa za kifalme, ndipo akakutana na tukio la wema alilofanyiwa na Mordekai, mfalme akauliza je mtu huyu alitendewa fadhila gani?, wakasema, hakutendewa lolote. Ndipo akatoa maagizo kwamba avikwe mavazi yake ya kifalme anayoyavaa yeye, kisha apandishwe kwenye farasi ambaye yeye mwenyewe ndiye anayempanda, kisha wamzungushwe mji mzima, huku akipigiwa mbiu, ili atukuzwe mbele ya watu wote, kwasababu mfalme AMEMUHESHIMU biblia inasema hivyo;. Soma Esta 6

Sasa mambo hayo yanafunua na ya rohoni pia. Ukiwa ni mtenda wema, ipo Heshima ya kipekee sana, itokayo kwa Mungu mwenyewe, italetwa juu yako, siku ile ikifika. Atakugawia ule utukufu wake mwenyewe,.. Biblia inasema..

Warumi 2:6 “atakayemlipa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake; 7 wale ambao KWA SABURI KATIKA KUTENDA MEMA WANATAFUTA UTUKUFU NA HESHIMA NA KUTOKUHARIBIKA, watapewa uzima wa milele; 8 na wale wenye fitina, wasioitii kweli, bali wakubalio dhuluma, watapata hasira na ghadhabu; 9 dhiki na shida juu ya kila nafsi ya mwanadamu atendaye uovu, Myahudi kwanza na Myunani pia; 10 BALI UTUKUFU NA HESHIMA NA AMANI KWA KILA MTU ATENDAYE MEMA, Myahudi kwanza na Myunani pia”;

Unaona? hivyo, usichoke kutenda mema, kumbuka wema mkuu ni pamoja na kuwakumbuka walio katika dhambi na kuwavuta kwa Bwana. Pia kuwafariji na kuwaombea wale waliowadhaifu katika Imani. Swali ni je! Katika maisha yako, ni mema mangapi, ulishawahi kufanya kwa ajili ya Mungu?

Bwana atusaidie, tuyatimilize yote.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

NGAZI 7 AMBAZO MKRISTO NI LAZIMA AZIPANDE KUUFIKIA UKAMILIFU.

TUSIWE WATU WA KUPUNGUKIWA AKILI.

INJILI YA MANENO LAINI ITAKUGHARIMU.

FAHAMU UWIANO MUNGU ANAOHITAJI KUUONA KWETU.

Nini maana ya mhubiri 9:11? si wenye mbio washindao katika michezo?

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
2 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Anonymous
Anonymous
2 years ago

Amina. Barikiwa kwa ujumbe wa maandiko unaouhubiri kwa neema ya Mungu. Mungu azidi kuimulika na kuipa kibali zaidi huduma ya Injili katika jina la Yesu. 🙏

Faraja Benjamin
Faraja Benjamin
2 years ago

Thanks man of God, through your Inspiration words I learned a lot about how God powerful is. Be blessed 🙏