Wanaowachukua wanawake wajinga mateka ni akina nani?

Wanaowachukua wanawake wajinga mateka ni akina nani?

2Timotheo 3:6 Inazungumzia watu wanaowachukua wanawake wajinga mateka, Je! Mstari huu una maana gani?


JIBU: Ukianzia kusoma tokea mstari wa kwanza utaona pale Paulo anamwonya Timotheo juu ya baadhi ya tabia za ajabu ambazo zitaanza kujitokeza katika siku za mwisho, alimwambia..

2Timotheo 3:1 “Lakini ufahamu neno hili, ya kuwa siku za mwisho kutakuwako nyakati za hatari…”

Ukiendelea kusoma utaona akizihorodhesha tabia zenyewe zitakazozuka..anasema watatokea watu wanaopenda fedha, watu wenye kiburi,wasio safi, wanaopenda anasa kuliko kumpenda Mungu..n.k. Lakini ukushuka mpaka mstari wa tano anasema tabia nyingine kuwa, nyakati hizo kutaibuka pia wimbi la watu wenye mfano wa utauwa, lakini wakizikana nguvu zake, na hapa ndipo pa hatari zaidi..Tusome..

2Timotheo 3:5 “wenye mfano wa utauwa, lakini wakikana nguvu zake; hao nao ujiepushe nao.

6 Kwa maana katika hao wamo wale wajiingizao katika nyumba za watu, na kuchukua mateka wanawake wajinga wenye mizigo ya dhambi, waliochukuliwa na tamaa za namna nyingi;

7 wakijifunza siku zote, ila wasiweze kabisa kuufikia ujuzi wa kweli”.

Unaona hapo?

Na wanawake pia wanahusishwa na watu hawa wanatajwa kuwa wao ndio waathirika wakubwa wa wimbi hilo la hao watu wanaojifanya kuwa ni watu wa Mungu(wenye mfano wa utauwa) lakini nyuma yake hawana Habari na Mungu hata kidogo (ni vyombo vya ibilisi dhahiri).

Hapa ndipo wewe kama mwanamke unapaswa ujichunge sana, tupo katika nyakati za hatari, kwasababu shetani tangu Edeni alikuwa anaufahamu mlango mwepesi wa kuuingilia ni mwanamke na si mwanaume (1Timotheo 2:14).. Leo hii utaona watu wa aina hii, hifadhi yao imekuwa wanawake wengi.., tena biblia inatumia neno

“Wanawake wajinga wenye mizigo ya dhambi na waliochukuliwa na tamaa za namna nyingi ”.

Ikiwa na maana kuwa wanawake hawa suala la wokovu kwao halina maana sana,(ni wajinga katika roho) wanachotafuta ni mambo ya mwilini tu, wabarikiwe kazi zao, wapewe waume, wapate fedha, wapigiwe maadui zao, na huku waendelee na mavazi yao ya nusu uchi barabarani, waendelee kuwasengenya majirani zao, waendelee kuzini, waendelee kuishi kidunia..

Hawataki kujishughulisha na mambo ya rohoni,(hawaupendi utakatifu hata kidogo!) wakiona tu nabii yule ni mtanashati, anachekesha, ana magari, ana majumba, ana wafuasi wengi bila kujiuliza mara mbili kwasababu tu kashajiita ni mtu wa Mungu wanaingiwa na tamaa wanakwenda kujiunganisha naye.

Hayo yote, ni mambo yaliyotabiriwa kuwa yatatokea katika siku za mwisho, na tunayaona sasa.. Na kibaya Zaidi wanawakaribisha kwenye majumba yao, wewe angalia utaliona hilo, ni mara chache sana utawaona kwenye nyumba zenye mchanganyiko wa wanaume, muda wote utawaona wanazunguka kwenye nyumba za wanawake tu, na wakigundua mwanamke huyo kaolewa hawataenda kwake au kama wakienda wataenda wakati mumewe hayupo!…(Na wanawachukua mateka kimwili na kiroho)

hiyo yote ni ili maandiko yatimie, kwamba siku za mwisho watatokea watu wa namna hiyo.

Na ndio maana mtume Yohana alipomwandika wakara yule MAMA Mteule, mtakatifu kuwa alimwonya asiwakaribishe watu kama hawa ambao wanakuja kwake lakini hawaleti mafundisho ya Kristo..

2Yohana 1:10 “Mtu akija kwenu, naye haleti mafundisho hayo [ya Kristo/utakatifu], msimkaribishe nyumbani mwenu, wala msimpe salamu.

11 Maana yeye ampaye salamu azishiriki kazi zake mbovu”.

Hivyo wewe kama mwanamke, iga mfano wa huyo “Mama mteule” Ipende kweli. Na sisi wote kwa Pamoja vivyo hivyo tu tutafute utakatifu.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

KWANINI UNAPASWA UJIWEKE TAYARI SASA, KABLA YA ULE WAKATI KUFIKA?.

JINSI SODOMA NA GOMORA ILIVYOKUWA INAVUTIA SANA..

YONA: Mlango wa 4

MKUMBUKE MKE WA LUTU.

KAMA ZILIVYOKUWA SIKU ZA NUHU NA ZA LUTU.

KUTAKUWA NA MATETEMEKO YA NCHI, NJAA NA TAUNI.

Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
1 Comment
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Emmanuel Kitengule
Emmanuel Kitengule
1 year ago

Amina mwalimu,nimebarikiwa sana.