Kisiwa cha Patmo kipo nchi gani?.

Kisiwa cha Patmo kipo nchi gani?.

Kisiwa cha Patmo kipo nchi ya Ugiriki kwa sasa…Kisiwa hicho kipo mashariki mwa Taifa la Ugiriki na magharibi mwa nchi ya Uturuki, kama vile Zanzibar ilivyo mshahariki mwa nchi ya Tanzania ndivyo kilivyo hichi kisiwa cha Patmo kwa Ugiriki.

Kisiwa hicho ndicho Mtume Yohana, ambaye alikuwa mwanafunzi wa Bwana Yesu, alifungwa.

Warumi walimkamata Yohana na kumtupa katika kisiwa hicho, kwa lengo la kumtesa kwa kosa la kumhubiri Yesu. (Kwa maelezo kwa njia ya sauti, fungua hapa chini)

[embedyt] https://www.youtube.com/watch?v=EhBLp-8-vPw[/embedyt]

Lengo la kumtupa Yohana katika kisiwa hicho cha Patmo, sio tu afe, bali afe kwa mateso. Kwani kisiwa hicho hakikukaliwa na mtu yeyote wakati huo, kwasababu kilikuwa ni kisiwa ambacho hakistawi nafaka, wala miti na zaidi sana, kilisifika kuwa na nyoka wengi.

Kwahiyo yoyote aliyetupwa katika kisiwa hicho, ilikuwa ni lazima afe kama hatakuja kuokolewa huko.

Lakini tunasoma, Yohana alipelekwa kule, kwaajili ya ushuhuda wa Neno la Mungu, wakati Jeshi la Warumi linaona limempeleka kwaajili ya mateso, yeye Yohana alijiona amepelekwa kwaajili ya ushuhuda…Kwamba akashuhudie mambo atakayokwenda kufunuliwa au kuambiwa na Mungu huko.

Ufunuo 1:9 “Mimi Yohana, ndugu yenu na mwenye kushiriki pamoja nanyi katika mateso na ufalme na subira ya Yesu Kristo, nalikuwa katika kisiwa kiitwacho Patmo, kwa ajili ya Neno la Mungu, na ushuhuda wa Yesu”

Hii ikifunua kuwa sio kila jaribu baya, lengo lake ni baya!. Yohana asingepelekwa Patmo, tusingekuwa na kitabu cha ufunuo, hali kadhalika Bwana Yesu asingepelekwa msalabani, tusingepata wokovu.

Kisiwa cha Patmo, sasahivi kinakaliwa na watu, kutokana na kuongeza kwa idada kubwa ya watu ulimwengu na yenye kuhitaji makazi..vile vile, kuongezeka kwa teknolojia ya mawasiliano, na usafiriwa wa haraka, umekifanya kisiwa hicho kiweze kukalika na watu leo.

Kisiwa cha Patmo, jina lake mpaka leo halijabadilika, kinaitwa hivyo hivyo Patmo, kama vile Yerusalemu jina lake lisivyobadilika siku zote.

Wakazi wa kisiwa cha Patmo kwasasa hawazidi 4,000 kulingana na sensa za Ugiriki.

Na kisiwa hicho, hakina miujiza yoyote ya kiroho, kwamba yeyote afikaye kule basi atapata ufunuo kama aliopata Yohana.

Bwana akubariki.

Maran atha.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

Kutakabari ni nini katika biblia?.

Je kauli ya Bwana Yesu inajichanganya? Katika Yohana 8:14 na Yohana 5:31?

Kwanini Yakobo na Yohana waliitwa “Wana wa Ngurumo”?

KWANINI KRISTO AFE?

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
21 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Anonymous
Anonymous
2 years ago

Shalom,kazi yenu njema.

Anonymous
Anonymous
2 years ago

Asante kwa somo hili.

Senior Pastor sammy
Senior Pastor sammy
2 years ago

Je ni mwanamke gani alikuwa mitume katika biblia

Anonymous
Anonymous
2 years ago

Amina asante sana. Na Mungu akubariki.

Anonymous
Anonymous
2 years ago

Amen Amen🙏🙏🙏

Samson Gikaro
Samson Gikaro
2 years ago

Mbarikiwe

Célestin
Célestin
2 years ago

Amen 🙏

JOSIAH LLOYD MURUVE
JOSIAH LLOYD MURUVE
2 years ago

Amen

Anonymous
Anonymous
2 years ago

Swali; Yohana alitokaje tokaje katika kisiwa hicho, kwa maana warumi walimtupa Kule na kumtelekeza, ndipo baadae Bwana Yesu anampa ule ujumbe wa Makanisa saba… Je alitokaje Kule patmo.??

UBARIKIWE.

Stephen Nchimbi
Stephen Nchimbi
2 years ago

Amina

Peter
Peter
2 years ago

Amen, Mtumishi wa Mungu ubarikiwe

Anonymous
Anonymous
2 years ago
Reply to  Peter

Mungu ni mwema sana

Anonymous
Anonymous
2 years ago

Swali; Yohana alitokaje tokaje katika kisiwa hicho, kwa maana warumi walimtupa Kule na kumtelekeza, ndipo baadae Bwana Yesu anampa ule ujumbe wa Makanisa saba… Je alitoka Kyle patmo.??

UBARIKIWE.

Anonymous
Anonymous
2 years ago

Amen.

lucas mhula
lucas mhula
2 years ago

Amen

Danieli
Danieli
2 years ago
Reply to  lucas mhula

Amina somo nzuri sana

Maige
Maige
2 years ago

Amen 🙏

Sumamwakalukwa
Sumamwakalukwa
2 years ago

Amen amen