Utasi ni ugonjwa gani? (Marko 7:32).

Utasi ni ugonjwa gani? (Marko 7:32).

Jibu: Kuna tofauti ya “Utasi” na “Utasa”.. Utasa ni hali ya mtu kutokuwa na uwezo wa kuzaa, lakini Utasi ni tatizo la udhaifu wa ulimi (yaani ulimi kuwa mzito), Mtu mwenye ugonjwa huu anakuwa hawezi kuongea vizuri, anakuwa hawezi kutamka maneno vizuri..Na wengi wenye tatizo hili wanakuwa wanazaliwa nalo.

Katika biblia tunaona ugonjwa huu ukitajwa mara moja tu!, kwa mtu mmoja ambaye Bwana Yesu..

Marko 7:32 “Wakamletea kiziwi, NAYE NI MWENYE UTASI, wakamsihi amwekee mikono.

33 Akamtenga na mkutano faraghani, akatia vidole vyake masikioni mwake, akatema mate, akamgusa ulimi,

34 akatazama juu mbinguni, akaugua, akamwambia, Efatha, maana yake, Funguka.

35 Mara masikio yake yakafunguka, kifungo cha ulimi wake kikalegea, AKASEMA VIZURI”.

Maandiko yanasema Bwana Yesu ni Yule Yule, alimponya mtu huyo, hata leo bado anaponya!, na haponyi Utasi tu peke yake, bali anaponya kila shida.. Na uponyaji mkuu kuliko yote ambao Bwana anautoa ni uponyaji wa Roho zetu. Huo ndio muujiza mkubwa ambao Bwana anaweza kutufanyia endapo tukimwamini.

Anatuponya roho zetu na mauti ya kiroho, na anatuokoa na ghadhabu ya Mungu, iliyo karibuni kumwangwa kwa ulimwenguni kwa watenda dhambi.

Je umepokea uponyaji huo leo?.. kama bado Tubu, mwamini Yesu na ukabatizwe katika ubatizo sahihi na kisha utapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

Na ulimi laini huvunja mfupa.(Mithali 25:15)

USIMLAANI KIZIWI, WALA USITIE KWAZO MBELE YA KIPOFU.

TATIZO LA NDANI LINALOWASUMBUA VIJANA, WALIOOKOKA.

USIKATE TAMAA UNAPOPITIA MAGONJWA.

 Nini maana ya “Uchungu wa mauti ni dhambi, na nguvu za dhambi ni torati”

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
7 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Emmanuel Kitengule
Emmanuel Kitengule
1 year ago

Barikiwa sana mwalimu kwa ufafanuzi mzuri.

Anonymous
Anonymous
1 year ago

Amin nabarikiwa sana

Stephen Nchimbi
Stephen Nchimbi
1 year ago

Amina