Uru wa Ukaldayo ni nini?

Uru wa Ukaldayo ni nini?

Neno “Uru” kama lilivyo katika Mwanzo 11:28, lina maana gani?.

Jibu: Tusome,

Mwanzo 11:28 “Harani akafa kabla ya baba yake Tera katika nchi aliyozaliwa, yaani, katika URU wa Wakaldayo.

29 Abramu na Nahori wakajitwalia wake. Jina la mkewe Abramu aliitwa Sarai, na jina la mkewe Nahori aliitwa Milka, binti Harani, ambaye alikuwa baba wa Milka na wa Iska”.

Neno “Uru”. Maana yake ni ARDHI/HIMAYA.. Kwahiyo hapo biblia iliposema “Harani akafa kabla ya baba yake Tera katika nchi aliyozaliwa, yaani, katika URU wa Wakaldayo”.. Maana yake ni kwamba “Tera alikufa katika Nchi/Himaya ya Wakaldayo”.

Kulingana na historia zilikuwepo “Uru” nyingi, enzi za kale, zilikuwepo Uru za Waashuri, Uru za Waajemi n.k.. Lakini iliyotajwa kwenye biblia ni moja tu ambayo ni Uru ya wakaldayo. (Kujua Wakaldayo walikuwa ni watu gani fungua hapa >> Wakaldayo)

Lakini kikubwa tunachoweza kujifunza ni kuwa Abramu aliambiwa atoke katika  nchi aliyozaliwa “Uru wa Wakaldayo”, aende nchi nyingine.

Ikifunua kuwa Mungu anapomwita mtu anapaswa atoke pale alipo na kwenda sehemu nyingine kiroho.

Mwanzo 12:1 “Bwana akamwambia Abramu, Toka wewe katika nchi yako, na jamaa zako, na nyumba ya baba yako, uende mpaka nchi nitakayokuonyesha;

 2 nami nitakufanya wewe kuwa taifa kubwa, na kukubariki, na kulikuza jina lako; nawe uwe baraka

 3 nami nitawabariki wakubarikio, naye akulaaniye nitamlaani; na katika wewe jamaa zote za dunia watabarikiwa”.

Je tangu ulipomwamini Yesu umetoka katika himaya ya ulevi?, umetoka katika himaya za wazinzi?, umetoka katika himaya za wachawi na washirikina, kama bado, ni Dhahiri kuwa bado hujaanza safari ya Wokovu. Anza leo kwa kujitenga na mambo hayo.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

JUMA LA SABINI (70) LA DANIELI

TUMEFANYIKA KUWA WANA WA MUNGU!

JINSI YA KUSOMA BIBLIA.

VIPINDI VINNE VYA MAISHA VILIVYO VIGUMU MTU KUMKUMBUKA MUUMBA WAKE.

Nini maana ya mtakayoyafunga duniani, yatakuwa yamefungwa mbinguni?

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
2 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Stephen Nchimbi
Stephen Nchimbi
2 years ago

Amina