Je Mungu huwa anadhihaki watu?

Je Mungu huwa anadhihaki watu?

Je Mungu huwa anadhihaki watu kulingana na Mithali 1:26 na Zaburi 59:8?.

Jibu ni ndio!!..Mungu anadhihaki!!.. na sio tu kudhihaki, bali pia anafadhaisha, na vilevile anahuzunisha watu..

Lakini lengo la kudhihaki watu, au kuhuzunisha watu, au kufadhaisha watu ni tofauti na lengo kama tulilonalo sisi..

Sisi tunawadhihaki watu ili tuwakomoe, au ili tuwakomeshe, au ili  tuwatese.. Lakini Mungu lengo lake si hilo, yeye hatudhihaki ili atukomoe, au atukomeshe….Lengo lake yeye ni sisi tutubu, tugeuke, tuone aibu kwa njia zetu mbaya, kisha tutubu na kuacha njia zetu mbaya. Na tukishatubu basi anatufurahisha na kutufariji.

Ndio maana maandiko yanasema..

Mithali 1:23 “GEUKENI KWA AJILI YA MAONYO YANGU; Tazama, nitawamwagia roho yangu, Na kuwajulisheni maneno yangu.

24 Kwa kuwa nimeita, nanyi mkakataa; Nimeunyosha mkono wangu, asiangalie mtu;

25 Bali mmebatilisha shauri langu, Wala hamkutaka maonyo yangu;

26 Mimi nami nitacheka siku ya msiba wenu, NITADHIHAKI HOFU YENU IFIKAPO”.

Je! Unataka kudhihakiwa na Mungu siku ya msiba wako, au tabu yako..je unataka kuchekwa siku na shida yako?.

Kama hutaki basi jitenge na ulimwengu, na dhambi… Hizo ndizo zinazotuficha uso wa Mungu mbali nasi. Lakini habari njema ni kwamba, Bwana hafurahii misiba yetu, wala tabu zetu, lengo lake ni sisi tuone aibu,  tuache dhambi zetu… ili atupe faraja na furaha.

Maombolezo 3:31 “Kwa kuwa Bwana hatamtupa mtu Hata milele.

32 Maana AJAPOMHUZUNISHA atamrehemu, Kwa kadiri ya wingi wa huruma zake.

33 Maana moyo wake hapendi kuwatesa wanadamu. Wala kuwahuzunisha”.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

BASI, IWENI NA HURUMA, KAMA BABA YENU ALIVYO NA HURUMA

Nini maana ya Hukumu haina huruma kwake yeye asiyeona huruma?

JE! NI WAPI UTAPOKEA HISIA ZA KWELI ZA KI-MUNGU?

NDIPO HUENDA AKACHUKUA PEPO WENGINE SABA.

Biblia inamaanisha nini inaposema “Mwenye haki huufikiri uhai wa mnyama wake”?

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
2 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Anonymous
Anonymous
2 years ago

MUNGU ANATUPENDA SANA