Wakaldayo ni watu gani?

Wakaldayo ni watu gani?

Wakaldayo ni wenyeji wakongwe wa Mji wa Babeli. Mji wa Babeli ulikuwepo maeneo ya nchi ya Iraq kwasasa.

Hawa wakaldayo ndio waliowachukua mateka wana wa Israeli na kuwapeleka utumwani Babeli..

Yeremia 21:8 “Nawe waambie watu hawa, Bwana asema hivi, Tazama naweka mbele yenu njia ya uzima, na njia ya mauti.

9 Yeye atakayekaa katika mji huu atakufa kwa upanga, na kwa njaa, na kwa tauni; bali yeye atakayetoka, na kujitia pamoja na Wakaldayo wanaowahusuru, yeye ataishi, na maisha yake yatakuwa nyara kwake.

10 Maana nimeweka uso wangu juu ya mji huu niuletee mabaya, wala nisiuletee mema, asema Bwana; utatiwa katika mkono wa mfalme wa Babeli, naye atauteketeza”.

Ezra 5:12 “Lakini hapo baba zetu walipomkasirisha Mungu wa mbingu na nchi, hata akaghadhibika, akawatia katika mkono wa Nebukadreza, mfalme wa Babeli, Mkaldayo, naye ndiye aliyeiharibu nyumba hii, akawachukua watu mateka mpaka Babeli”

Pia Ibrahimu kabla ya kuhamia nchi ya Kaanani, alikuwa anaishi huko Uru ya Wakaldayo. Kwasababu Babeli tayari ilikuwepo miaka mingi kabla hata ya Taifa la Israeli kuwepo, ndipo ule Mnara wa Babeli ulipotengenezewa.

Mwanzo 11:31 “Tera akamtwaa Abramu mwanawe, na Lutu mwana wa Harani, mwana wa mwanawe, na Sarai mkwewe, mke wa Abramu mwanawe, wakatoka wote katika Uru wa Wakaldayo, waende nchi ya Kanaani, wakafika mpaka Harani wakakaa huko”.

Hivyo popote biblia inapowataya Wakaldayo ina maanisha Wenyeji wa Babeli.

Je una habari kuwa Babeli iliyowachukua wana wa Israeli mateko kwa namna ya kimwili, ipo leo kwa namna ya kiroho?..Kama ulikuwa hujui basi kasome kitabu cha ufunuo mlango wa 17 na kuendelea.

Na Babeli hiyo ya rohoni inawachukua utumwa watu wengi leo pasipo wao kujua, na mwisho wa siku inawaua kiroho na kuwapeleka kuzimu. Na Babeli hii sasa inafanya kazi kwa nguvu katika dini na madhehebu, na Bwana ataihukumu katika siku za mwisho.

Ufunuo 14:8 “Kisha mwingine, malaika wa pili, akafuata, akisema, Umeanguka, umeanguka Babeli, mji ule ulio mkubwa, maana ndio uliowanywesha mataifa yote mvinyo ya ghadhabu ya uasherati wake”.

Kwa urefu kuhusu Babeli hii ya rohoni fungua hapa >> BABELI YA ROHONI

Je umeokoka?.  Kumbuka Kristo anarudi saa na wakati usiodhani?..Wakati unafikiri bado sana ndio wakati anaokuja..

Waebrania 10:37 “Kwa kuwa bado kitambo kidogo sana, Yeye ajaye atakuja, wala hatakawia”.

Kama hujampokea ni vizuri ikampokea sasa hivi, wala usisubiri hata dakika 5 mbele, kwasababu hujua yatakayojitokeza dakika mbili mbele. Hivyo hapo ulipo piga magoti, kisha tubu dhambi zako zote kwa kumaanisha kuziacha, na Bwana wa huruma na Neema atakusamehe bure, na kukutakasa. Na baada ya hapo tafuta ubatizo sahihi, wa maji mengi na kwa jina la Yesu, na  tafuta kanisa la Kristo la kiroho, lililo karibu nawe,  jiunge hapo na wakristo wenzako ili ujengeke kiroho, na Roho Mtakatifu atakuongoza kufanya yaliyosalia.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

MNARA WA BABELI

Mto Frati upo nchi gani, Umuhimu wake katika biblia ni upi?

Kongwa ni nini kwenye biblia?(Wagalatia 5:1)

NENO LA MUNGU NI DAWA ILIYO TOFAUTI NA DAWA NYINGINE.

JUKUMU LA MUHIMU LINALOKWEPWA NA WENGI.

Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
3 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Pangani Dickson
Pangani Dickson
2 months ago
Anonymous
Anonymous
9 months ago

Amen barikiwa mtumishi