HIZI NI NYAKATI ZA KUFUNGA NA KUOMBA.

HIZI NI NYAKATI ZA KUFUNGA NA KUOMBA.

Mathayo 9:14  “Wakati ule wanafunzi wake Yohana wakamwendea, wakasema, Kwa nini sisi na Mafarisayo twafunga, BALI WANAFUNZI WAKO HAWAFUNGI?

15  Yesu akawaambia, Walioalikwa arusini wawezaje kuomboleza, muda bwana arusi akiwapo pamoja nao? Lakini siku zitakuja WATAKAPOONDOLEWA BWANA ARUSI; NDIPO WATAKAPOFUNGA”.

Wanafunzi walipokuwa na Bwana Yesu katika mwili, chochote walichokihitaji walikipata kirahisi kwasababu Neema walikuwa naye katika mwili, walipohitaji uponyaji Kristo alikuwepo kuwaponya, walipohitaji kuona ishara na miujiza kama ile ya mikate mitano kulisha elfu tano, waliiona kirahisi.

Kila walichokihitaji walikipata, kwasababu Mtenda miujiza walikuwa wanamwona dhahiri na kumshika. Lakini ulipofika wakati wa Kristo kuchukuliwa juu, mambo yalibadilika!!, ile hali ya kusubiria kufanyiwa mambo na Bwana ikapotea, ikawabidi waanze kutafuta wenyewe namna ya kufanya mambo!. Ni kama tu kifaranga cha kuku kilichoachwa na mama yake, kikawaida kinaanza kujitafutia chenyewe, kitatembea huku na kule kama mama yake kutafuta chakula.

Ndicho kilichowatokea Mitume Bwa Yesu, ulipofika wakati wanakutana na wagonjwa na yule Bwana Yesu wa kukimbiziwa  wagonjwa hayupo!!!.. ndipo ufahamu wa kutafuta nguvu alizokuwa nazo Bwana Yesu ukawajia!.

Ndipo wakaanza kutafiti ni vitu gani vilivyokuwa vinampa nguvu Bwana Yesu, kufanya miujiza ile na kuishi maisha yale!, ndipo wakaanza kutafakari maisha yake na kugundua kuwa muda mwingi Bwana aliutumia KUFUNGA na KUKESHA MILIMANI KUOMBA.

Na wao ikawabidi wabadilike na kuanza kuwa WAFUNGAJI NA WAOMBAJI kama Bwana Yesu ili baadhi ya mambo yawezekanike kama yalivyowezekanika kwa Bwana, vinginevyo baadhi ya mambo yasingeenda sawa, Ndio maana utaona akina Petro walipokuwa na Bwana ni kama walikuwa wanavutwa vutwa katika suala la uombaji (Utaona kuna mahali Bwana Yesu alikuja kuwaamsha Zaidi ya mara 2 waombe lakini wakarudi kulala).

Marko 14:34  “Akawaambia, Roho yangu ina huzuni nyingi kiasi cha kufa; kaeni hapa mkeshe.

35  Akaendelea mbele kidogo, akaanguka kifudifudi, akiomba ya kuwa, ikiwezekana, saa hiyo imwepuke. 36  Akasema, Aba, Baba, yote yawezekana kwako; uniondolee kikombe hiki; walakini, si kama nitakavyo mimi, bali utakavyo wewe.

37  AKAJA AKAWAKUTA WAMELALA USINGIZI, AKAMWAMBIA PETRO, JE! SIMONI, UMELALA? Hukuweza kukesha saa moja? 14.38  Kesheni mwombe, msije mkaingia majaribuni, roho i radhi ila mwili ni dhaifu.

39  Akaenda zake tena, akaomba, akisema neno lilo hilo.

40  AKAJA TENA AKAWAKUTA WAMELALA, maana macho yao yamekuwa mazito, wala hawakujua la kumjibu.

41  Akaja mara ya tatu, akawaambia, Laleni sasa, mpumzike; yatosha, saa imekuja; tazama, Mwana wa Adamu anatiwa mikononi mwao wenye dhambi”.

Hapa tunaona akina Petro wakiwa wanavutwa vutwa katika suala la uombaji, lakini tunaona mambo yanabadilika baada ya Bwana Yesu kuondoka, walianza kufunga na kukesha katika maombi mengi,.. Kuna mahali Petro anaonekana kufunga kwa kuomba mpaka anazimia kwa njaa.

Matendo 10:9  “Hata siku ya pili, walipokuwa wakisafiri na kuukaribia mji, Petro alipanda juu darini, kwenda kuomba, yapata saa sita ya mchana;

10  AKAUMWA NA NJAA SANA, AKATAKA KULA; LAKINI WALIPOKUWA WAKIANDAA, ROHO YAKE IKAZIMIA,

11  akaona mbingu zimefunuka, na chombo kikishuka kama nguo kubwa, inatelemshwa kwa pembe zake nne hata nchi”

Hii ikifunua nini?

Kristo mpaka sasa hayupo nasi katika Mwili, hivyo na sisi pia tupo katika Nyakati za KUFUNGA na KUOMBA.

Ndugu Hizi ni nyakati za “Kufunga na kuomba”. Bwana Yesu alisema mambo mengine hayawezekaniki isipokuwa kwa kufunga na kuomba/kusali.

Mathayo 17:21 “[Lakini namna hii haitoki ila kwa kusali na kufunga]”

Je Unataka kumwona Mungu katika maisha yako?..Funga na kuomba!..je  unataka kuongezeka viwango vya kumjua Mungu?..Funga na kuomba!…Je Unataka Neema iongezeke juu yako! Na mambo mengine mengi yaliyo mazuri uyaone??, basi funguo ni Mifungo na Maombi. (Na kumbuka hapa biblia inazungumzia Maombi na sio maombezi). Usifunge na kwenda kutafuta kuombewa na mtumishi!.. Bali funga na omba mwenyewe!.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

NJIA SAHIHI YA KUFUNGA.

HATUA ZA ROHO MTAKATIFU KATIKA KUTUONGOZA.

Kutazama Nyakati mbaya ni kufanyaje?.

NYAKATI SABA ZA KANISA NA WAJUMBE WAKE.

Kwanini maombi kwa Marehemu si sahihi kibiblia?

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
1 Comment
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Emmanuel Buberwa Kitengule
Emmanuel Buberwa Kitengule
10 months ago

Amina