UWE KIKOMBE SAFI 

UWE KIKOMBE SAFI 

Nakusalimu katika jina la Bwana wetu Yesu Kristo. Karibu tuyasikilize maagizo ya Mungu.

Kuna wakati Bwana alipokutana na mafarisayo alisema maneno haya;

Mathayo 23:25-26

[25]Ole wenu waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mnasafisha nje ya kikombe na chano, na ndani yake vimejaa unyang’anyi na kutokuwa na kiasi.

[26]Ewe Farisayo kipofu, safisha kwanza ndani ya kikombe, ili nje yake nayo ipate kuwa safi.

Tengeneza picha ya kikombe. Kiuhalisia ili kifae Kwa matumizi ni lazima kiwe kisafi pande zote, yaani nje na ndani. Huwezi kutumia kikombe ambacho nje ni kisafi lakini ndani kina matope, vilevile huwezi tumia kikombe ambacho ndani ni kisafi lakini nje kina matope,. Bado uchafu ni ule ule..Hivyo ili kifae Kwa matumizi hakina budi kisafishwe kotekote ndani na nje.

Leo hii tunakosa shabaha kudhani, ni upande mmoja tu Mungu anautazama. Ndivyo walivyofanya mafarisayo Kwa nje walionekana wanyenyekevu, wafanya ibada, Wana staha, waalimu wazuri wa torati lakini ndani walijaa wivu, mashindani, majivuno, tamaa n.k.

Lakini vilevile wapo watu ambao Kwa ndani wanadai Wana upole, Upendo, amani, lakini Kwa nje, hawana ushuhuda wowote, Hawa ndio wale ambao wanasema Mungu anaangalia vya rohoni haangalii vya nje.

Ndugu ili utumiwe na Bwana, safisha kikombe kotekote. Rohoni na Mwilini 

Sasa haya ni baadhi ya mambo ambayo unapaswa uyafanye kotekote. Tukiangazia mifano kwa Bwana Yesu.

1) KUMPENDEZA MUNGU.

Yesu aliishi maisha ya kumpendeza Mungu, lakini alijua kwamba kabla ya kumpendeza Mungu ni lazima niwapendeze kwanza wanadamu. Hivyo akafanya bidii kuwa na sifa njema katika jamii pia, na kwa Mungu.

Luka 2:52

[52]Naye Yesu akazidi kuendelea katika hekima na kimo, akimpendeza Mungu na wanadamu.

Umeona? Hakuwa mtu wa kusema Mimi ni Mungu tu, lakini alitafuta sifa nzuri pia Kwa wanadamu ili Mungu wake atukuzwe, hivyo aliishi vizuri na wanadamu, alikuwa mtiifu, mwaminifu, mwenye utu, mwenye adabu kwa watu. Vivyo hivyo na wewe kama mkristo kama sifa zako nje zinavuma vibaya.. hata kama ni mtu mzuri kiibada hapo ni sawa na umesafisha kikombe Kwa ndani lakini nje ni kichafu. Hivyo bado hujakamilika. Safisha pande zote, mbinguni na ulimwenguni.

2) UPENDO

Maandiko yanasema, Mpende Bwana Mungu wako Kwa moyo wako wote, na Kwa Roho yako yote na Kwa nguvu zako zote..lakini kabla hayajasema maneno hayo, Mungu alitangulia kusema kwanza mpende jirani Yako,ili Upendo wako kwake ukamilike.

1 Yohana 4:20-21

[20]Mtu akisema, Nampenda Mungu, naye anamchukia ndugu yake, ni mwongo; kwa maana asiyempenda ndugu yake ambaye amemwona, hawezi kumpenda Mungu ambaye hakumwona.

[21]Na amri hii tumepewa na yeye, ya kwamba yeye ampendaye Mungu, ampende na ndugu yake.

Kabla hujampenda Mungu mpende mwanadamu. Safisha kikombe nje na ndani.

3) USAFI

Mungu anatutaka tuwe wasafi moyoni moyoni.(Mathayo 5:8)..Lakini usafi wa ndani unakamilishwa na ule wa nje.

Soma

2 Wakorintho 7:1

[1]Basi, wapenzi wangu, kwa kuwa tuna ahadi hizo, na tujitakase nafsi zetu na uchafu wote wa mwili na roho, huku tukitimiza utakatifu katika kumcha Mungu.

Umeona kumbe Kuna uchafu wa mwili na pia wa roho. Ule wa Roho ndio wivu, kiburi, uongo n.k. lakini ule wa mwili ndio ulevu, uvaaji mbovu, uchoraji mwili, utukanaji, mazungumzo mabaya.n.k

Ikiwa unajiita Mtakatifu halafu unatembea na vimini barabarani, Binti unatembea na suruali, na nguo za mgongo wazi, huna tofauti na yule mhudumu wa pale bar.Fahamu kuwa huo usafi wako wa roho ni kazi bure. Kijana unatembea na suruali za milegezo, unafuga Rasta na viduku, huna tofauti na yule msanii wa kidunia.halafu unasema wewe ni msafi wa moyo fahamu kuwa hapo unayo dosari mbele za Bwana.

UWE KIKOMBE SAFI.

Shalom

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

KIKOMBE CHA GHADHABU YA MUNGU KINAJAA.

UPENDO NI NINI NA JE! KUNA AINA NGAPI ZA UPENDO?

KIASI NI NINI KATIKA UKRISTO?

UTAYAFIKIAJE MANENO SAFI YA MUNGU?

Njia zote za mtu ni safi machoni pake mwenyewe;(Mithali 16:2)

AINA SABA (7) ZA UNAFIKI, AMBAZO UNAPASWA UJIEPUSHE NAZO.

Maziara ni nini? Je! Na Tunaruhusiwa kuyajenga kwenye makaburi yetu?

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments