Kwanini Mungu alituumba?

Kwanini Mungu alituumba?

Swali: Kwanini Mungu ametuumba? Na Sababu ya sisi kuwepo ni ipi?.. Na kwanini mmoja aumbwe hivi mwingine vile? kwa ujumla kwanini Mungu aliiumba dunia?


Jibu: Mungu katuumba sisi kwa “Kupenda kwake yeye (Mapenzi yake)”… Ili yeye afurahi kuwa pamoja nasi na sisi tufurahi kuwa pamoja naye!.

Ufunuo 4:11 “Umestahili wewe, Bwana wetu na Mungu wetu, kuupokea utukufu na heshima na uweza; kwa kuwa wewe ndiwe uliyeviumba vitu vyote, na KWA SABABU YA MAPENZI YAKO VILIKUWAKO, navyo vikaumbwa”.

Kwetu kuumbwa ni “faida kubwa”…kwasababu hakuna faida yoyote ya “kutokuwepo”.. tengeneza picha haupo au hatupo!..je ni faida gani unapata au tunapata?..Lakini kama tukiwepo na tukaishi maisha ya milele na furaha basi ni heri sana!.

Na Mungu mwenyewe ametuahidia uzima wa milele kupitia mwanae YESU KRISTO.

Yohana 3:16 “Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele”

Lakini kama mtu hatapenda kuishi, na wala hataki maisha basi njia ya kupoteza maisha ni kumkataa YESU.

1Yohana 5:12  “Yeye aliye naye Mwana, anao huo uzima; asiye naye Mwana wa Mungu hana huo uzima”

swali la pili; kwanini mmoja aumbwe hivi mwingine vile?

Jibu rahisi ni kwasababu ndivyo ilivyompendeza yeye ili kututofautisha sisi kwa sisi (hajapenda wote tufanane kama sisimizi)…na hatuwezi kuhoji Zaidi!.

Warumi 9:20  “La! Sivyo, Ee binadamu; wewe u nani umjibuye Mungu? Je! Kitu kilichoumbwa kimwambie yeye aliyekiumba, Kwani kuniumba hivi?

21  Au mfinyanzi je! Hana amri juu ya udongo, kwa fungu moja la udongo kuumba chombo kimoja kiwe cha heshima, na kimoja kiwe hakina heshima?”

Lakini kwa vyovyote vile tulivyoumbwa tunapaswa tuutafute uzima wa milele na pia ni muhimu kufahamu kuwa kwa Mungu hakuna upendeleo wa mmoja Zaidi ya mwingine, wote tupo sawa mbele zake, pasipo kuangalia mwonekano, wala kimo, wala umri, wala jinsia.. Wote tunapendwa sawa, na tunapimwa sawa mbele zake .

Je unao uzima wa milele ndani yako?..Kumbuka uzima wa Milele upo kwa mmoja tu! YESU KRISTO!, Ikiwa bado hujampokea na unahitaji msaada katika kumpokea basi  waweza wasiliana nasi kwa namba zetu..

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

TAFUTA UZIMA WA MILELE NA SI UZIMA TU!.

NUNUA MAJI YA UZIMA.

UNATAKA KUBARIKIWA? BASI USIKWEPE GHARAMA ZAKE.

FAHAMU VIASHIRIA VYA MTU ALIYESAMEHEWA DHAMBI ZAKE.

Kwanini Yakobo alimshinda Mungu, Je! Mungu huwa anashindwa na wanadamu?

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments