Ulafi ni nini kibiblia?

Ulafi ni nini kibiblia?

Kikawaida ulafi ni tabia ya kupenda kula kuliko pitiliza, Sio vibaya kula, na pia sio dhambi kula na kushiba..

Lakini tabia hii inapovuka mipaka kiasi kwamba kila kitu kinachokuja mbele ya macho yetu ni kutamani kukila kama vile wanyama..(huo ni ulafi).

Biblia imetaja tabia hii kuwa haitokani na Roho Mtakatifu Kwasaababu matunda ya tabia hiyo ni mabaya.

Wagalatia 5:19 “Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi,

20 ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi,

21 husuda, ulevi, ULAFI, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu”.

Mtu mlafi atatoa chochote ili ale au anywe, hata kama ameshiba, atatafuta kila njia ili aliridhishe tumbo lake kwa chochote atakachokitamani, anaweza hata kuiba, au kudhulumu, au kufanya jambo lolote lisilo la kiMungu ilimradi tu, apate chakula anachokihitaji.

Anaweza kuhudhuria karamu yoyote atakayoalikwa hata kama hiyo karamu ni ya mashetani..lengo lake ni ili ale na kunywa tu!.

Mtu mlafi ni rahisi kuingia katika mtego wowote wa ibilisi, Esau aliuza haki yake ya mzaliwa wa kwanza kwa chakula,

Waebrania 12:16 “Asiwepo mwasherati wala asiyemcha Mungu, kama Esau, aliyeuuza urithi wake wa mzaliwa wa kwanza kwa ajili ya CHAKUKA KIMOJA”.

Hebu tuangalie hekima moja ya Sulemani aliyoiandika kuhusiana na ulafi na madhara yake.

Mithali 23:1 “Utakapoketi kwa chakula pamoja na mtawala, Mwangalie sana yeye aliye mbele yako.

2 Tena ujitie kisu kooni, KAMA UKIWA MLAFI.

3 Usivitamani vyakula vyake vya anasa; Kwa maana ni vyakula vya hila……

6 Usile mkate wa mtu mwenye husuda; Wala usivitamani vyakula vyake vya anasa;

7 Maana aonavyo nafsini mwake, ndivyo alivyo. ATAKUAMBIA HAYA, KULA, KUNYWA; LAKINI MOYO WAKE HAUWI PAMOJA NAWE.

8 Tonge lile ulilokula utalitapika, Na maneno yako matamu yatakupotea.”

Umeona?..wanawake wengi na mabinti wanaingia katika mtego wa dhambi ya uasherati kutokana na ulafi (wanatamani kila aina ya chakula wanachokiona), na shetani anakitumia hicho kuwakamata.

Wengine wanaingia katika mitego ya kula rushwa kwasababu ya Ulafi, wengine wanaingia katika mitego ya kuua, au kudhulumu kwasababu ya Ulafi.

Na hata wengine wanaingia katika umaskini kwasababu ya ulafi (biblia inasema hivyo katika Mithali 23:20-21), Kwasababu muda wote mtu huyo anakuwa anafikiria kula tu, na hafikiri vitu vingine.

Na mojawapo ya dalili za siku za mwisho, biblia imetabiri ni watu kuwa WALAFI (watu watakuwa wakila na kunywa).

Luka 17:26 “Na kama ilivyokuwa siku za Nuhu, ndivyo itakavyokuwa katika siku zake Mwana wa Adamu.

27 Walikuwa wakila na kunywa, walikuwa wakioa na kuolewa, hata siku ile Nuhu aliyoingia katika safina, gharika ikashuka ikawaangamiza wote”.

Hivyo hatuna budi kuwa na kiasi na kujihadhari na ulafi.

Luka 21:34 “Basi, jiangalieni, mioyo yenu isije ikalemewa na ULAFI, na ulevi, na masumbufu ya maisha haya; siku ile ikawajia ghafula, kama mtego unasavyo;

35 kwa kuwa ndivyo itakavyowajilia watu wote wakaao juu ya uso wa dunia nzima.

Na pia tabia ya ULAFI, siku zote inaenda kinyume na MFUNGO.

Mtu aliye mlafi, huwa hapendi wala hawezi kufunga na hivyo anakuwa pia anakosa baraka nyingi za kiroho kwasababu maandiko yanasema “mambo mengine hayatoki isipokuwa kwa kufunga na kuomba(Mathayo 17:21)”.

Hivyo kwa hitimisho ni kwamba tunapookoka hatuna budi kuacha na ULAFI pia!, Kwasababu tabia hiyo haitokani na Roho Mtakatifu.

1 Petro 4:3 “Maana wakati wa maisha yetu uliopita watosha kwa kutenda mapenzi ya Mataifa; kuenenda katika ufisadi, na tamaa, na ulevi, na KARAMU ZA ULAFI, na vileo, na ibada ya sanamu isiyo halali.

Bwana atubariki.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

Je! Mbinguni Kutakuwa na kula na kunywa?.

Je tunaruhusiwa kutumia vidonge wakati wa kufunga?

Nini maana ya “chakula hakituhudhurishi mbele za Mungu”?

Katika Mathayo 15:21-28, Yesu alikuwa na maana gani alipomwambia huyu Mama kwamba chakula cha watoto hawapewi mbwa?

CHAKULA CHA ROHONI.

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
5 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Lucy wambui
Lucy wambui
1 year ago

Nimeelimishwa zaidi…..barikiwa sana

Anonymous
Anonymous
1 year ago

amina

Lucas mhula
Lucas mhula
1 year ago

Asanteni sana kwa somo

Zuberi Moto
Zuberi Moto
1 year ago

Asante kwa somo nzuri