Hazina za gizani ni zipi? (Isaya 45:3).

Hazina za gizani ni zipi? (Isaya 45:3).

Jibu: Tusome,

Isaya 45:3 “nami nitakupa hazina za gizani, na mali zilizofichwa za mahali pa siri, upate kujua ya kuwa mimi ni BWANA, nikuitaye kwa jina lako, naam, Mungu wa Israeli”.

Hazina za gizani ni baraka zote zilizoshikiliwa na adui shetani ambazo zingepaswa ziwe zetu.

Hazina hizi zinakuwa zinashikiliwa na adui kwa kitambo tu, na pale tunapotia bidii basi tunaweza kuzitwaa na kuzirejesha kwetu.

Mfano wa hazina za gizani ni zile wana wa Israeli walizozipata kutoka katika jeshi la Washami.

Wakati ule ambao Israeli walikuwa wana njaa kali, hata kufikia hatua watu kula mavi ya njiwa, na kichwa cha punda…na wakati huo huo mji wote ulikuwa umezungukwa na jeshi la Washami pande zote.

na Mungu akayasikilizisha majeshi ya washami mishindo ya farasi, na kwa hofu kubwa wakaacha vyakula vyao vyote na kukimbia kutoka katika zile kambi zao walizokuwepo, na wana wa Israeli wakaenda kuzitwaa zile Nyara na vile vyakula.. Hivyo wakawa wamepewa na Bwana hazina zilizikuwepo gizani.

2 Wafalme 7:5 “Basi wakaondoka kabla ya mapambazuko, ili waende mpaka kituo cha Washami; na walipofika mwanzo wa kimo cha Washami, kumbe! Hapana mtu.

6 Kwa maana Bwana alikuwa amewasikizisha Washami kishindo cha miendo ya magari, na kishindo cha farasi, kama kishindo cha jeshi kubwa; wakaambiana, Tazama, mfalme wa Israeli amewaajiri wafalme wa Wahiti, na wafalme wa Wamisri, waje wapigane nasi.

7 Kwa hiyo wakaondoka, wakakimbia kungali giza bado, wakaziacha hema zao, na farasi zao, na punda zao, na kimo chao vile vile kama kilivyokuwa, wakakimbia wapate kujiponya nafsi zao.

8 Basi wale wenye ukoma walipofika mwisho wa kituo, waliingia katika hema moja, wakala, na kunywa, wakachukua fedha, na dhahabu, na mavazi, wakaenda wakavificha; wakarudi, wakaingia katika hema ya pili, vile vile wakachukua vitu, wakaenda, wakavificha.

9 Ndipo wakaambiana, Mambo haya tufanyayo si mema; leo ni siku ya habari njema, na sisi tunanyamaza; mkingoja hata kutakapopambazuka, madhara yatatupata; basi twende tukawaambie watu wa nyumba ya mfalme.

10 Basi wakaenda, wakawaita mabawabu wa mji; wakawaambia, Tulifika kituo cha Washami, na tazama, hapana mtu ye yote huko, wala sauti ya mtu, ila farasi wamefungwa, na punda wamefungwa, na hema zao kama walivyoziacha.

11 Na mabawabu wakaita wakawaambia watu wa nyumba ya mfalme.

12 Mfalme akaondoka usiku, akawaambia watumishi wake, Sasa nitawaonyesha ninyi walivyotutendea Washami. Wanajua ya kuwa tuna njaa; basi wametoka kituoni, ili kujificha kondeni, wakisema Watakapotoka mjini, tutawakamata hai; tena tutapata kuingia mjini.

13 Na mmojawapo wa watumishi wake akajibu, akasema, Kunradhi; baadhi ya watu na watwae farasi watano katika hao waliosalia, waliobaki ndani ya mji (tazama wamekuwa kama mkutano wote wa Israeli waliobaki ndani yake; tazama, wamekuwa kama mkutano wote wa Israeli walioangamia), tukawapeleke tukaone.

14 Basi wakatwaa magari mawili na farasi zake; mfalme akawatuma kuwafuata Washami, akasema, Enendeni, mkaangalie.

15 Wakawafuata mpaka Yordani; na kumbe! Njia yote ilikuwa imejaa mavazi na vyombo, walivyovitupa Washami, wapate kukimbia upesi. Watu wale waliotumwa wakarudi, wakamwambia mfalme.

16 Basi watu wakatoka, wakaziteka nyara hema za Washami. Ikawa kipimo cha unga mzuri kikauzwa kwa shekeli, na vipimo viwili vya shayiri kwa shekeli, sawasawa na neno la BWANA”.

Sasa huo ni mfano wa hazina ambazo zilikuwa gizani (yaani zimeshikiliwa na adui), lakini baadaye zikaondolewa kutoka kwa adui na kupewa watu wa Mungu.
Na hata sasa zipo hazina nyingi ambazo zipo gizani, ambazo zinapaswa ziwe za kwetu..Adui kazishikilia, na sisi tusipopiga hatua kwenye kuteka nyara basi adui ataendelelea kuzimiliki na sisi tutaendelea kutateseka.

Na hazina zenyewe zinaweza kuwa ni WATU au VITU. Kuna watu wetu wengi leo ambao wameshikwa na adui vile vile kuna vitu vyetu vingi ambavyo vimeshikwa na adui, ambavyo tukiwa imara katika Imani tunaweza kuvitwaa na kuviteka.
Maandiko yanasema..

2 Wakorintho 10:4 “maana silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome;)

5 tukiangusha mawazo na kila kitu kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu; NA TUKITEKA NYARA KILA FIKRA IPATE KUMTII KRISTO”.

Maana yake tukivaa silaha hizo za Mungu, basi tutakuwa na uwezo wa kuziteka hazina zote za gizani…kama ni watu wetu wapo gizani, basi tunaweza kuwatoa huko, kama ni vitu vyetu vipo gizani, basi tunaweza kuvirejesha endapo tukivaa silaha hizo na kuingia vitani.

Sasa swali ni je!. Hizo silaha za kwenda kuteka nyara hazina za gizani ni zipi?
Si nyingine zaidi ya zile silaha 7 tunazozisoma katika kitabu cha Waefeso 6:10-18, ambazo ni WOKOVU, KWELI, HAKI, IMANI, UTAYARI,NENO, na MAOMBI.

Ni kupitia silaha hizo tu, ndio tunaweza kuzipata hazina za gizani na mali zilizofichwa sawasawa na hiyo Isaya 45:3.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

Silaha za Mkono wa kuume na za mkono wa kushoto ni zipi

TUZIDI KUWA HODARI KATIKA BWANA.

Je Mkristo kutembea na walinzi (Bodyguards),ni sawa?

Kwanini Mungu aseme, Alaaniwe azuiaye upanga wake usimwage damu (Yeremia 48:10).

Deraya ni nini? Kama tunavyosoma katika Isaya 59:17

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments