Je Mkristo kutembea na walinzi (Bodyguards),ni sawa?

Je Mkristo kutembea na walinzi (Bodyguards),ni sawa?

SWALI: Je Mkristo kutembea na walinzi (Bodyguards), katika huduma ni sawa? Kama sio mbona Bwana Yesu alitembea na mitume wake?


JIBU: Tufahamu kuwa mitume hawakuwa walinzi wa Bwana Yesu, Bali waliitwa kwa kazi ya kumshuhudia Yesu duniani.

Na ndio maana utaona wakati Fulani walijaribu kumtetea kwa silaha zao, Lakini Bwana Yesu alimkemea Petro, na kumwambia sikushindwa kuwaagiza Malaika wa Baba yangu kuja kunipigania,(Mathayo 26:52) hiyo ni kuonyesha kuwa kazi ya ulinzi ni ya Malaika sio ya wanadamu. Na pia hakuwaita, ili wamlinde, bali wajifunze kwake.

Kitendo cha mkristo, au askofu kutembea na askari wenye silaha, mikononi mwao wenye lengo la kumlinda, kama vile walindwavyo wanasiasa au watu mashuhuri, hiyo si sawa. Kwasababu hizo sio nyendo za Bwana wetu Yesu Kristo,alipokuwa hapa duniani.

Ndio upo wakati ambapo huduma itakuwa kubwa, na hivyo kutahitajika kuwekwe mipaka ya watu kukufikia, ili huduma itendeke kwa utaratibu, Lakini hiyo bado haikufanyi uwaajiri walinzi, bali  unapaswa uwaweke watendakazi wenzako katika shamba la Bwana walio chini yako, hiyo ndio kazi yao, kama Kristo alivyofanya kwa mitume wake, hakuwaweka  maakida wa kirumi, au watoza ushuru, au watu mataifa kuwa wahudumu wake.

Yohana 12:20 “Palikuwa na Wayunani kadha wa kadha miongoni mwa watu waliokwea kwenda kuabudu kwenye sikukuu.

21 Basi hao walimwendea Filipo, mtu wa Bethsaida ya Galilaya, wakamwomba, wakisema, Bwana, sisi tunataka kumwona Yesu.

22 Filipo akaenda, akamwambia Andrea; kisha Andrea na Filipo wakamwambia Yesu”.

Hivyo kibiblia sio sahihi, mtu wa Mungu kuwaajiri maaskari wa ulinzi, kumlinda. Ni vizuri Zaidi akawachagua watakatifu wenzake ambao atakuwa anahudumu nao, kila aendapo.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Wale mamajusi walikuwa ni wakina nani?

Je! dhambi zote ni sawa Kuna dhambi kubwa na ndogo?

KUMBE MUNGU ANAWEZA KUKULIPA KWA USICHOSTAHILI!

NITAUVUTAJE UWEPO WA ROHO MTAKATIFU KARIBU NAMI?

Talanta ni nini katika biblia (Mathayo 25:14-30)

Gongo na Fimbo ni nini? Na vinawezaje kumfariji mtu? (Zaburi 23:4).

Mti wa MLOZI alioonyeshwa nabii Yeremia 1:12 tafsiri yake ni nini?

Mshipi wa dhahabu matitini ni nini?

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
2 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Anonymous
Anonymous
1 year ago

Lakini mbona daudi alikuwa ame lindwa na alikuwa mutu wa mungu?

Anonymous
Anonymous
1 year ago

Amen,SOMO zuri sana, ubarikiwe saana