WITO WA MUNGU HAUVUKI NENO LAKE.

by Admin | 27 November 2021 08:46 pm11

Bwana Yesu atukuzwe ndugu yangu. Karibu tuyatafakari maneno ya uzima pamoja..

Tunaposoma biblia..tujue kuwa tunausoma ufahamu wa Mungu. Mtu asiyeitafakari biblia halafu anakimbilia kwenda kumtumikia Mungu.. Ajue kuwa anajiweka katika hatari kubwa sana ya kuangamizwa na Mungu.

Ni sawa na mtu anayekimbilia kufanya biashara ambayo hajaifanyia utafiti kujua changamoto zake.faida zake na hasara zake..

Leo tutatazama ni kwa namna gani.

Ndugu usipumbazwe hata kidogo kuona Mungu anasema nawe..anakuonyesha maono makubwa..anakusifia..anakutokea..anakutuma ukawahubirie watu injili.. Usipumbazwe kabisa na jambo hilo. Kama maagizo yaliyopo katika Neno lake huyatii..Kufa unaweza tu kufa.

Jambo kama hilo tutaliona kwa Musa. Kila mtu anafahamu kuwa alitokewa na Mungu mwenyewe katika mwali wa moto. Mungu akampa ishara kubwa..akamtuma aende Misri kwenda kuwaokoa mamilioni ya watu..Lakini cha ajabu tunashangaa Mungu alitaka kumuua njiani..

Yaani kama sio mke wake Sipora,kumsaidia habari ya Musa ingekuwa imeishia pale na maono yake na wito wake.

Kutoka 4:21-25

[21]BWANA akamwambia Musa, Hapo utakaporudi Misri, angalia ukazifanye mbele ya Farao zile ajabu zote nilizozitia mkononi mwako; lakini nitaufanya mgumu moyo wake, naye hatawapa ruhusa hao watu waende zao.

[22]Nawe umwambie Farao, BWANA asema hivi, Israeli ni mwanangu mimi, mzaliwa wa kwanza wangu;

[23]nami nimekuambia, Mpe mwanangu ruhusa aende, ili apate kunitumikia, nawe umekataa kumpa ruhusa aende; angalia basi, mimi nitamwua mwanao, mzaliwa wa kwanza wako.

[24]Ilikuwa walipokuwa njiani mahali pa kulala, BWANA akakutana naye akataka kumwua.

[25]Ndipo Sipora akashika jiwe gumu na kuikata govi ya zunga la mwanawe, na kuibwaga miguuni pake akasema. Hakika wewe u bwana arusi wa damu kwangu mimi.

Sasa ni kwanini Mungu alitaka kumuua ni kwasababu alipuuzia maagizo ya msingi ya kuwatahiri watoto wake..Mambo ambayo Mungu alikuwa ameshawaagiza  wana wa Israeli wote wafanye hivyo kulithibitisha agano lake..Lakini yeye hakuona umuhimu huo..kisa tu Mungu amemtokea..amemtuma kama nabii mkuu Misri..hivyo hakuna sababu ya kuhangaika na yale mengine..

Ni wangapi leo hii wamepatwa na kiburi cha kukataa maagizo ya Mungu kama vile ubatizo sahihi wa maji..kwa kisingizio kuwa Mungu anazungumza na wao..Mungu kawatokea..Mungu kawaagiza waende kutumika..ubatizo hauna maana yoyote ukishamkiri tu Kristo inatosha..Wewe si zaidi sana ya nabii  Musa..Mungu hashindwi kukuua.

Unaweza kusema ni Musa tu peke yake yalimkuta haya..Yupo nabii mwingine huko mbeleni anaitwa Balaamu.. Yeye naye alitokewa na Mungu katika safari yake ya kwenda kuwalaani Israeli.

Mara ya kwanza Mungu akamuonya lakini hakusikia.. Akataka zaidi kufanya hivyo..baadaye Mungu akamruhusu na akamuhakikishia kuwa atakuwa pamoja naye..Lakini njiani Mungu alikuwa ameshamweka malaika wake tayari amuue. Kama si yule Punda kumsaidia habari yake ingekuwa naye imeisha pale…

Ni kwanini sasa iwe vile ni kwasababu alipuuzia maagizo ya awali ya Mungu “..amlaaniye Israeli na yeye atalaaniwa”(Mwanzo 12:3)..hivyo yeye akataka kulipindua hilo Neno kwa maono yake..au mitazamo yake mwenyewe. Akawa katika hatihati ya kufa..

Hesabu 22:12-13

[12]Mungu akamwambia Balaamu, Usiende pamoja nao; wala usiwalaani watu hawa, maana wamebarikiwa.

[13]Balaamu akaondoka asubuhi akawaambia wakuu wa Balaki, Enendeni zenu hata nchi yenu; kwa maana BWANA amekataa kunipa ruhusa niende pamoja nanyi….

Lakini baada ya kushurutishwa sana na wale wakuu wa Balaki..utaona alijifanya tena kwenda kumuuliza Mungu..hichi ndio kitu alichoambiwa mara ya pili

Hesabu 22:20-22

[20]Mungu akamjia Balaamu usiku, akamwambia, Kwa kuwa watu hawa wamekuja kukuita, enenda pamoja nao; lakini neno lile nitakalokuambia ndilo utakalolitenda, basi.

[21]Balaamu akaondoka asubuhi, akatandika punda wake, akaenda pamoja na wakuu wa Moabu.

[22]Hasira ya Mungu ikawaka kwa sababu alikwenda; malaika wa BWANA akajiweka njiani, ili kumpinga. Basi alikuwa amepanda punda wake, na watumishi wake wawili walikuwa pamoja naye.

Ndugu..tuzifahamu tabia za Mungu..wapo watu wengi wameonyeshwa mambo makubwa sana katika wito wao. Lakini unashangaa hakuna hata moja limetimia..hadi siku anakufa..Ni kwanini?

Nikwasababu alikwenda pasipo kujua kanuni za Mungu. Tuishi kwa Neno la Mungu na sio kwa ndoto au sauti au maono. Haijalishi wito huo utakuwa mkubwa kiasi gani..hauwezi kuzidi Neno lake.. Neno linasema mwanamke hana nafasi ya kufundisha kanisani (palipo na mchanganyiko wa wanaume na wanawake) 1Timotheo 2:12..Lakini mwingine atasema Mungu kaniita kuwa Mchungaji..kanitokea kabisa na kunitia mafuta..

Mama kuwa makini..kasome biblia yako kwanza umwelewe Mungu ndipo ukatumike..

Hivyo ili tuwe salama.. kabla ya kuitii sauti yoyote ya nje..Tuitii kwanza Sauti ya Mungu iliyo katika Neno lake.  Ndio hayo mengine yafuate.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp ya kila siku basi jiunge kwa kubofya hapa >>> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

USIPOTEZWE NA MANENO YA MANABII WA UONGO.

JE UNAIFANYA KAZI YA MUNGU?

MAJARIBU MATATU YA YESU KRISTO

TAFUTA MSAMAHA HALISI, NA SI MSAMAHA TU!

UTAWALA WA MIAKA 1000.

Nini maana ya “wazimu” katika biblia?

JINSI PAULO ALIVYOPAMBANA NA UJINGA WA ROHONI.

PINDO LA VAZI LAKE SASA LIMEREFUSHWA.

Rudi nyumbani

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2021/11/27/wito-wa-mungu-hauvuki-neno-lake/