Babewatoto ni nani katika biblia?(Isaya 34:14).

Babewatoto ni nani katika biblia?(Isaya 34:14).

Babewatoto ni jina lingine la mapepo yanayotembea usiku (yenye mfano wa ndege wa angani).

Hawa wametajwa mara moja tu katika biblia..

Isaya 34:14 “Na hayawani wa nyikani watakutana na mbwa-mwitu, na beberu anamwita mwenziwe; naam, babewatoto anakaa huko na kujipatia raha”.

Bwana alitoa unabii juu watu wote wa ulimwengu waliomwacha yeye, kuwa makao yao yatakuwa ni makao ya hayawani wa porini na ya mapepo hayo (Babewatoto).

Utaona unabii kama huo Bwana aliutoa pia kwa Babeli kwamba utaanguka na makao yake yatakuwa ukiwa na hayawani wa mwituni watakaa huko na MAJINI yatacheza huko.

Jambo ambalo lilikuja kutimia kama lilivyo..ulipofika wakati wa unabii huo kutimia, Babeli ilikuja kuanguka na mahali pale ambapo palisifika kwa uzuri na bustani zinazoelea leo hii tunapozungumza ni jangwa, hayawani wa porini wanapita na majini wanakaa huko.

Isaya 13:19 “Na Babeli, huo utukufu wa falme, uzuri wa kiburi cha Wakaldayo, utakuwa kama Sodoma na Gomora hapo Mungu alipoiangamiza.

20 Hautakaliwa na watu tena kabisa, wala watu hawatakaa ndani yake tangu kizazi hata kizazi. Mwarabu hatapiga hema yake huko, wala wachungaji hawatalaza makundi yao huko.

21 Lakini huko watalala hayawani wakali wa nyikani; na nyumba zao zitajaa bundi; mbuni watakaa huko; na MAJINI watacheza huko”.

MAJINI yanayozungumziwa hapo ni mapepo yenye maumbile kama ya Mbuzi-mwitu.

Hiyo ikifunua kuwa tukimwacha Mungu haijalishi tulikuwa tumestawi kiasi gani, Bwana ataushusha utukufu wetu na makao yetu yatakuwa ni makao ya majini (mapepo) na babewatoto.
Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:

Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au

Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

MAJINI WAZURI WAPO?

AINA ZA MAJINI, MAJINA YAO, KAZI ZAO, NA TIBA ZAKE.

IMESALIA RAHA YA SABATO KWA WATU WA MUNGU.

MISTARI YA BIBLIA KUHUSU WATOTO.

Makao ambayo Yesu alikwenda kutuandalia ni yapi?

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments