WANNE WALIO WAONGO.

WANNE WALIO WAONGO.

Biblia imetuonya imetutahadharisha vitu vitatu vilivyo na udanganyifu kuliko vitu vyote.

1.MOYO

Moyo wa mtu ndio kitu kilicho kidanganyifu kuliko vyote..

Yeremia 17:9 “Moyo huwa mdanganyifu kuliko vitu vyote, una ugonjwa wa kufisha; nani awezaye kuujua?”

Hakukuwa na shetani mwingine mbinguni aliyemdanganya shetani, bali kilichomdanganya shetani ni moyo wake mwenyewe… Moyo wake ulimtuma kuamini kuwa anaweza kuwa kama Mungu. Na hivyo akaufuata moyo wake na mwisho akaangukia upotevuni.

Na mioyo yetu sisi wanadamu ni midanganyifu sana, na mara nyingi inatuongoza pabaya…Mithali 16:2 “Njia zote za mtu ni safi machoni pake mwenyewe…” Na maandiko yanatufundisha kulinda mioyo yetu kuliko vyote tulindavyo, kwasababu huko ndiko zinakotoka chemchemi za uzima (Mithali 4:23).

Na tunailinda kwa kuangalia yale tunayoyasikia au tunayojifunza, na biblia ndio kitabu pekee cha kutusaidia kupima mambo yote.

2. DHAMBI.

Dhambi ni adui wa pili wa kumwongopa kuliko “shetani”. Na dhambi siku zote inadanganya, (inavutia kwa nje lakini mwisho wake ni Mauti, Warumi 6:23). Ulevi unaonekana kama unavutia lakini mwisho wake ni Mauti, Anasa zinaonekana kama zinavutia, lakini mwisho wake ni Mauti, Vivyo hivyo na Zinaa, na usengenyaji, na wizi, na rushwa n.k Vyote hivyo vinavutia kwa nje lakini ndani yake ni Mauti.

Waebrania 3:13 “Lakini mwonyane kila siku, maadamu iitwapo leo; ili mmoja wenu asifanywe mgumu kwa UDANGANYIFU WA DHAMBI”.

3. SHETANI.

Maandiko yanasema wazi kuwa shetani ni baba wa Uongo.

Shetani atakuambia kuabudu sanamu si dhambi, kunywa pombe si dhambi, kuupenda ulimwengu si dhambi, kujiburudisha kwa anasa si dhambi n.k  Na kumbe anasema Uongo, kwasababu yeye ni baba wa huo, ndivyo alivyomdanganya Hawa na ndivyo anavyoendelea kudanganya watu mpaka leo.

Yohana 8:44 “Ninyi ni wa baba yenu, Ibilisi, na tamaa za baba yenu ndizo mpendazo kuzitenda. Yeye alikuwa mwuaji tangu mwanzo; wala hakusimama katika kweli, kwa kuwa hamna hiyo kweli ndani yake. Asemapo uongo, husema yaliyo yake mwenyewe; kwa sababu yeye ni mwongo, na baba wa huo”

4. MALI

Maandiko pia yanasema kuwa Mali zinadanganya!.. Mali zinasema ukizipata utaheshimika, ukizipata utapendwa, ukizipata utaishi vizuri.. jambo ambalo si kweli, Kristo pekee ndiye ukimpata mambo yote, yatakuwa sawa hata pasipo hizo mali… Kama alisema “mtu hataishi kwa mkate tu, bali Neno la Mungu”…si zaidi Mali???.

Lakini Mali zenyewe zinatuhubiria kinyume chake kuwa pasipo hizo, maisha yetu hayawezi kwenda au yatakuwa ya shida, maisha yetu yatakuwa ya tabu na mateso…

kwahiyo kama hatutaongeza umakini katika kumjua Mungu na uweza wake tutadanganyika na udanganyifu huo ambao Mali zinauhubiri.. tutajikuta tunatumia muda mwingi kuzisaka na kutumia muda mchache kumtafuta Mungu.. na hivyo kupotea..

Mathayo 13:22  “Naye aliyepandwa penye miiba, huyo ndiye alisikiaye lile neno; na shughuli za dunia, na UDANGANYIFU WA MALI hulisonga lile neno; likawa halizai”.

Mali zisikudanganye na kukupotezea muda wako mwingi, Mali zisikuambie kuwa usipoenda kuzisaka siku ya jumapili utakufa njaa!!, mali zisikudanganye kuwa usipotumia usipotumia muda mwingi kuzisaka basi zitakukimbia!!..  Jihadhari na udanganyifu huo.

Bwana atubariki na kutusaidia.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

MBINGUNI YUPO NANI SASA?

Kwanini Paulo aungane na wale watu wanne wenye nadhiri?

Heri walio maskini wa roho; Maana ufalme wa mbinguni ni wao.

KWA WALE WALIO NJE “YOTE” HUFANYWA KWA MIFANO.

Sadaka ya Moyo ipoje? (Walawi 22:21).

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
1 Comment
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
JEAN MARIE BITA
JEAN MARIE BITA
1 year ago

amen