MWANAMKE ABIGAILI ANAFUNZO GANI KWA WANAWAKE?

MWANAMKE ABIGAILI ANAFUNZO GANI KWA WANAWAKE?

Abigaili.

Huu ni mwendelezo wa mafundisho maalumu yahusuyo wanawake.

Na Leo tutaisikia sauti ya Mungu iliyokuwa nyuma maisha ya huyu mama aliyeitwa Abigaili.

Abigaili ni mwanamke aliyeolewa na mwanaume ambaye halikuwa chaguo la Mungu kwake, ijapokuwa mwanaume huyo alikuwa tajiri, hatujui ni nini kilimsukuma Abigaili katika ujana wake kukubali kuolewa na mwanaume yule, labda pengine Nabali hakuanza vile, alikuja kubadilika baadaye, au pengine wazazi wake walimshurutisha aolewe naye kwasababu ya utajiri aliokuwa nao.

Lakini mwanaume huyo halikuwa chaguo sahihi la Abigaili Kutoka Kwa Mungu, kwani Nabali hakuwajali watu wa chini kabisa, Wala hakuwa mtu wa kurudisha fadhila. Utakumbuka wakati ambapo Daudi anakimbizwa na Sauli, akiwa kule  maporini, alikutana na kundi kubwa la mifugo wa huyu Nabali, hivyo Daudi alichofanya ni kuwapa hifadhi watumwa wake, kuwahakikishia ulinzi, dhidi ya wavamizi wa mifugo ya wachungaji,kwasababu Nabali alikuwa na mifugo mingi sana na kipindi ambacho wanakwenda kuwakata manyoya kondoo wao, waporaji wenye silaha Huwa wanawavamia sana wafugaji..hivyo walidumu na Daudi Kwa muda wote huo mpaka walipomaliza shughuli zao.

Lakini siku moja Daudi alipungukiwa chakula yeye na jeshi lake hivyo wakaona mtu wa karibu atakayeweza kuwasaidia ni huyu Nabali. Ndipo Daudi akatuma wajumbe kwake kumuomba chochote alichonacho awasaidie.Lakini badala ya kupokea fadhili akapokea matusi. Ndipo Daudi akakasirika sana akataka kwenda kumuua Lakini mke wake alipopata habari akafanya kinyume chake akaaanda vyakula na kumpelekea Daudi, ndipo hasira yake ikageuka.

Embu tukisome kisa hichi Kwa ufupi;

1 Samweli 25:9-38

[9]Basi walipofika vijana wake Daudi, wakamwambia Nabali sawasawa na maneno hayo yote kwa jina la Daudi, kisha wakanyamaza.

[10]Naye Nabali akawajibu wale watumishi wa Daudi, akasema, Huyu Daudi ni nani? Na mwana wa Yese ni nani? Siku hizi kuna watumwa wengi wanaomtoroka kila mtu bwana wake!

[11]Basi mimi je! Nitwae mkate wangu, na maji yangu, na machinjo yangu niliyowachinjia hao watu wangu wakatao manyoya kondoo zangu, na kuwapa watu ambao siwajui wametoka wapi?

[12]Basi vijana wake Daudi wakageuka, wakaenda zao, wakarudi, nao wakaja wakamwambia sawasawa na maneno hayo yote.

[13]Kisha Daudi akawaambia watu wake, Haya! Jifungeni kila mtu upanga wake. Nao wakajifunga kila mtu upanga wake; Daudi naye akajifunga upanga wake; nao wakapanda nyuma yake Daudi, wapata kama watu mia nne; na watu mia mbili wakakaa na vyombo vyao.

[14]Lakini kijana mmojawapo alimpasha habari Abigaili, mkewe Nabali, kasema, Tazama, Daudi alituma wajumbe kutoka nyikani waje ili kumsalimu bwana wetu, naye akawatukana.

[15]Walakini watu hawa walitutendea mema sana, wala hatukupata dhara, wala sisi hatukupotewa na kitu cho chote, wakati wote tulipofuatana nao, tulipokuwako mavueni;

[16]watu hao walikuwa boma kwetu usiku na mchana, wakati wote tulipokuwa nao tukiwachunga kondoo.

[17]Basi sasa ujue na kufikiri utakayotenda; kwa sababu yamekusudiwa mabaya juu ya bwana wetu, na juu ya nyumba yake yote; kwa kuwa yeye ni mtu asiyefaa kabisa, hata mtu hawezi kusema naye.

[18]Ndipo Abigaili akafanya haraka, akatwaa mikate mia mbili, na viriba viwili vya divai, na kondoo watano waliofanyizwa tayari, na vipimo vitano vya bisi, na vishada mia vya zabibu, na mikate ya tini mia mbili; akavipakia vitu hivi juu ya punda.

[19]Akawaambia vijana wake, Haya! Tangulieni mbele yangu; angalieni, mimi nawafuata. Ila hakumwambia mumewe, Nabali.

[20]Ikawa, alipokuwa amepanda punda wake, na kutelemka penye sitara ya mlima, tazama, Daudi na watu wake walikuwa wakishuka kumkabili; naye akawakuta.

[21]Basi Daudi alikuwa amesema, Hakika ni bure nilivyokuwa nikilinda nyikani yote aliyo nayo mtu huyu, asipotewe na kitu cho chote cha mali yake yote; naye amenilipa mabaya badala ya mema.

[22]Mungu naye awafanyie hivyo adui za Daudi, na kuzidi, nikimwachia katika wote walio wake hata mtoto mume mmoja, kutakapopambazuka asubuhi.

[23]Ndipo hapo Abigaili alipomwona Daudi, alifanya haraka kushuka juu ya punda wake, akamwangukia Daudi kifulifuli, akainama mpaka nchi.

[24]Akamwangukia miguuni pake, akasema, Juu yangu, bwana wangu, juu yangu mimi na uwe uovu; tafadhali mjakazi wako na anene masikioni mwako, nawe uyasikilize maneno ya mjakazi wako.

[25]Nakusihi, bwana wangu, wewe usimwangalie huyu mtu asiyefaa, yaani, Nabali; kwa maana kama lilivyo jina lake ndivyo alivyo yeye; jina lake ndilo Nabali, na upumbavu anao; lakini mimi, mjakazi wako, sikuwaona hao vijana wa bwana wangu aliowatuma.

[26]Basi sasa, bwana wangu, aishivyo BWANA, na iishivyo nafsi yako, kwa kuwa BWANA amekuzuia usimwage damu, tena usijilipize kisasi mkono wako mwenyewe, basi sasa adui zako, na hao wamtakiao bwana wangu mabaya, wawe kama Nabali.

[27]Na sasa zawadi hii, mjakazi wako aliyomletea bwana wangu, na wapewe vijana wamfuatao bwana wangu.

[28]Nakuomba ulisamehe kosa lake mjakazi wako, kwa kuwa hakika BWANA atamfanyia bwana wangu nyumba iliyo imara, kwa sababu bwana wangu anavipiga vita vya BWANA; tena uovu hautaonekana ndani yako siku zako zote.

[29]Na hata ijapokuwa binadamu angeinuka akuwinde, na kuitafuta nafsi yako, hiyo nafsi ya bwana wangu itafungwa katika furushi ya uhai pamoja na BWANA, Mungu wako; na nafsi za adui zako ndizo atakazozitupa nje, kama kutoka kati ya teo.

[30]Tena itakuwa, hapo BWANA atakapokuwa amemtendea bwana wangu sawasawa na mema yote aliyoyanena juu yako, na kukutawaza juu ya Israeli;

[31]hili halitakuwa kwazo, wala chukizo la moyoni kwa bwana wangu, ama ya kuwa umemwaga damu bure, ama ya kuwa bwana wangu amejilipiza kisasi mwenyewe; tena hapo BWANA atakapokuwa amemtendea bwana wangu mema, ndipo umkumbuke mjakazi wako.

[32]Naye Daudi akamwambia Abigaili, Na ahimidiwe BWANA, Mungu wa Israeli, ambaye amekuleta hivi leo kunilaki;

[33]na ibarikiwe busara yako, na ubarikiwe wewe, uliyenizuia hivi leo nisimwage damu, wala kujilipiza kisasi kwa mkono wangu mwenyewe.

[34]Kwa kuwa ni kweli, aishivyo BWANA, Mungu wa Israeli, aliyenizuia nisikudhuru, kwamba hungefanya haraka kuja kunilaki, hakika huyu Nabali asingaliachiwa hata mtoto mume mmoja, kutakapopambazuka asubuhi.

[35]Basi Daudi akapokea mkononi mwake vitu vile alivyomletea; akamwambia, Haya! Kwea kwa amani kwenda nyumbani kwako; tazama, nimeisikiliza sauti yako, nami nimeukubali uso wako.

[36]Kisha Abigaili alimjia Nabali; na tazama, alikuwa amefanya karamu nyumbani mwake, kama karamu ya kifalme; na moyo wake huyo Nabali ukafurahiwa ndani yake, kwa maana amelewa kabisa. Kwa sababu hiyo hakumwambia neno, dogo wala kubwa, hata kulipopambazuka.

[37]Ikawa asubuhi, divai ilipokuwa imemtoka Nabali, mkewe alimwambia mambo hayo, na moyo wake ukafa ndani yake, akawa kama jiwe.

[38]Tena ikawa, yapata siku kumi baadaye, BWANA alimpiga huyo Nabali, hata akafa.

Ni nini mwanawake wanapaswa wajifunze kuhusiana na maisha ya Abigaili.

  1. Mwanaume Bora si yule mwenye Mali:

Kundi kubwa la wanawake wengi wa sasa wanaotaka kuolewa kigezo wanachokitazama Kwa wanaume ni Mali, wanasahau kuwa hata shetani hutoa Mali. Nabali alimsumbua sana Abigaili katika maisha yake ya ukamilifu, na kama asingekuwa na bidii katika busara yake angeshauliwa mbali na Daudi pamoja na Mali zao. Kufunua kuwa Kristo kama mfalme wetu, Huwa anaziadhibu familia Kwa makosa ya wanandoa wasiowajibika kiroho. Haijalishi wingi wa Mali walizonazo. Wewe kama mwanamke unayekaribia kuolewa kumbuka mwanaume anayemcha Mungu ndio chaguo sahihi kwako, na si vinginevyo.

  1. Pili Abigaili analiwakilisha kundi la wanawake ambao, wameshaingia katika ndoa za watu wasiosahihi.

Wanawake wengi wapo kwenye ndoa, lakini baadaye sana ndio wanakuja kugundua kuwa waume walionao hawakuwa Kutoka Kwa Bwana. Wengine ni wazinzi, wengine ni walevi kama Nabali, wengine hawajali kazi za Mungu Wala Roho zao wenyewe, wengine majambazi, wengine wanawatesa n.k.

Lakini utaona busara ya Abigaili haikuwa kwenda kutafuta mwanaume mwingine aolewe naye, kisa mume wake ni mpumbavu, ila aliendelea kudumu katika haki na ukamilifu, aliendelea kumwombea rehema mume wake hata Kwa maadui zake. Ijapokuwa alikuwa mjinga, lakini hakujaribu kujitenga na mumewe, alimwachia Mungu amfanyie wepesi. Na tunaona Mungu mwenyewe ndio alikuja kushughulika na Nabali akamuua, Kisha Abigaili akawa mke wa Mfalme Daudi. Pumziko la ndoa yake likaja.

Hata sasa wewe kama mwanamke ambaye upo katika ndoa chungu. Huitaji kuizira ndoa hiyo, badala yake omba rehema, na wokovu Kwa mume wako kwa Yesu. Naye ataugeuza moyo wake. Bwana hatatumia njia ya kumuua, lakini ataua uovu na ubaya ulio ndani yake. Na atakuwa tu mume Bora, lakini  usichoke kuomba ukasema nimeomba sana sijaona mabadiliko.yoyote… wewe endelea kuomba hata kama itapita miaka 20, ujue Mungu anaona na kusikia maombi Yako tu, atatenda jambo. Huyo atakuwa mume Bora zaidi ya unavyodhani, usipozimia moyo.Hivyo iga busara ya Abigaili.

Anza sasa kuijenga ndoa Yako. Bwana akubariki.

Shalom.

Je! Umeokoka? Je unafahamu kuwa hizi ni nyakati za mwisho na Mlango wa neema unakaribia kufungwa? Unasubiri nini usiokoke? Itakufaidia nini uupate ulimwengu wote halafu upate hasara ya nafsi Yako? Ikiwa upo tayari kumkabidhi Leo Bwana Yesu maisha Yako. Basi wasiliana nasi Kwa namba zetu hizi Kwa ajili ya mwongozo huo Bure.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

MASOMO MAALUMU KWA WANAWAKE.

NI KITU GANI TUNAJIFUNZA KWA RISPA, BINTI AYA?

Je! kuna mwanamke mwingine aliyempaka Bwana marhamu (manukato) zaidi ya Mariamu ndugu yake Lazaro?

Maneno ya mchongezi ni kama vitoweo; Nayo hushukia pande za ndani za tumbo

Na ulimi laini huvunja mfupa.(Mithali 25:15)

Kwanini Yesu Kristo ni mwana wa Adamu?

MISTARI YA BIBLIA YA FARAJA.

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
1 Comment
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Tumaini
Tumaini
10 months ago

Naomba niombewe nina allergy inayonisumbua muda mrefu sana sipati hasta Raha nikianza kuwashwa mwili unavimba. Nimeokoka Mungu akubariki Kwa mafundisho