MKUU WA UZIMA AKUWEKE HURU.

by Admin | 28 June 2020 08:46 am06

Bwana Yesu ndiye Mkuu wa Uzima (Matendo 3:15) Kwasababu alitabiriwa kuwa atakuwa Mkuu Zaidi ya wote..(Luka 1:15)..Na kwasababu hiyo basi Mungu alimpaka Mafuta ya Ukuu kuliko wote (Waebrania 1:9)..na uweza wa ajabu aliuweka juu yake….”Uweza wa kuwaweka huru waliofungwa na uteka wa shetani.(Luka 4:18).. Na kwa jina lake ametupa sisi wote tulio mwamini, mamlaka ya kuzitenda kazi zake zote…na utukufu ule aliokuwa nao ametupa sisi (Yohana 17:22)..Hivyo tuna nguvu kama za Simba zisizokuwa na mwisho, za kufanya makubwa kama aliyoyafanya Mkuu wa Uzima Yesu.

Kwasababu alisema..

Marko 16:17 “Na ishara hizi zitafuatana na hao waaminio; kwa jina langu watatoa pepo; watasema kwa lugha mpya;

18 watashika nyoka; hata wakinywa kitu cha kufisha, hakitawadhuru kabisa; wataweka mikono yao juu ya wagonjwa, nao watapata afya”.

Kwasababu hiyo basi mimi kama mmoja wa waliomwamini yeye, na kupewa mamlaka hayo…

Amini kuwa Ameyafanya hayo yote…Na yatakuwa kama ulivyoamini.

ZABURI 18: 1 “WEWE, BWANA, NGUVU ZANGU, NAKUPENDA SANA; BWANA NI JABALI LANGU, NA BOMA LANGU, NA MWOKOZI WANGU, MUNGU WANGU, MWAMBA WANGU NINAYEMKIMBILIA, NGAO YANGU, NA PEMBE YA WOKOVU WANGU, NA NGOME YANGU”

Maran atha!

Mada Nyinginezo:

MAOMBI YA VITA

YESU MPONYAJI.

KISIMA CHA MAJI YA UZIMA NI KILE KILE CHA ZAMANI.

USITOKE NJE YA HIFADHI YA MUNGU.

WAZAZI WA YOHANA NA YAKOBO.

Je! Bwana Yesu alibatiza akiwa hapa duniani?

VITA VYA IMANI NI VITA ENDELEVU.

Rudi Nyumbani:

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2020/06/28/mkuu-wa-uzima-akuweke-huru/