JINSI DHAMBI INAVYOMGHARIMU MTU SANA.

JINSI DHAMBI INAVYOMGHARIMU MTU SANA.

Mwanzo 47:9 “Yakobo akamjibu Farao, Siku za miaka ya kusafiri kwangu ni mia na thelathini; siku za miaka ya maisha yangu zimekuwa chache, TENA ZA TAABU, wala hazikufikilia siku za miaka ya maisha ya baba zangu katika siku za kusafiri kwao.”

Hakuna dhambi isiyokuwa na gharama. Unaweza ukajiuliza ni kwanini Yakobo alimwambia Farao siku zake za kusafiri duniani zimekuwa ni za taabu, zisizoweza kufananishwa na za baba zake..?..

Ni kwasababu ya ujanja alioufanya wa kumdanganya baba yake na kuchukua mbaraka wa ndugu yake, Japo ni kweli ndani yake kulikuwa na mpango wa Mungu uliobeba ujumbe uliomhusu Mesia, lakini kitendo alichokifanya bado kilikuwa ni uovu..Na hiyo haikuzuia kutumikia adhabu ya uovu wake.

Na ndio maana utaona Yakobo baada ya kufanya kitendo kile alikimbilia kwa mjomba wake, hata yule mama yake aliyependana naye na kupatana kutenda uovu, ndio ikawa mwisho wa kuonana kwao tena mpaka mwisho wa miaka 20 mbeleni, kuonyesha kuwa upendo wowote wenye makubaliano yasiyo makamilifu huwa haudumu..

Na alipofika kwa mjomba yake Labani, na kukaa huko, akimtumikia kwa ajili ya Raheli mke wake, kwa miaka saba, akidhani sasa ndio anakwenda kumpata Raheli, kumbe mjomba yake Labani akamfanyia hila kama ile ile aliyomfanyia ndugu yake Esau, matokeo yake akapewa dada yake Lea ndio awe mke wake badala ya Raheli, hivyo Labani akamwambia akimtaka na Raheli pia ni lazima amtumie miaka saba mingine..

Akaendelea kuwa mtumishi kwa muda mrefu mingine, mpaka wakati anaondoka, Na kwenda kule Kaanani nchi ya baba yake. Huko nako Watoto wake wawili Simeoni na Lawi, wakamfanyia hila kwa kudanganya, mpaka wakaenda kuwauwa watu wasiokuwa na hatia (Mwanzo 34),

Kama hiyo haitoshi, mwanawe wa kwanza Reubeni, akamzunguka baba yake, naye pia akamfanyia hila akaenda kulala na mke wake.

Tena Zaidi ya hayo, Watoto wake wakamfanyia hila kubwa Zaidi, kumdanganya kuwa mtoto wake Yusufu ampendaye ameliwa na mnyama mkali porini..Ikimfanya alie sana na kuomboleza kwa uchungu mwingi..

Kwahiyo unaweza kuona Maisha ya Yakobo, yalikuwa ni ya kudanganywa danganywa tu, na kufanyiwa hila kila kukicha, tofauti na ilivyokuwa kwa Ibrahimu na Isaka..

Kwasababu biblia inasema…

Mathayo 7:2 “Kwa kuwa hukumu ile mhukumuyo, ndiyo mtakayohukumiwa; na kipimo kile mpimiacho, ndicho mtakachopimiwa”.

Na ndio maana utaona anakiri kabisa Maisha yake yalikuwa ni ya taabu,..Lakini mwishoni kabisa Mungu alikuja kumpa faraja, kupitia mwanawe Yusufu.

Sasa huyo alikuwa ni Yakobo, mtu aliyebarikiwa na Mungu, lakini hakuachwa bila adhabu ya muda mrefu hapa duniani. Tujiulize sisi ambao tunaoendelea kuishi katika Maisha ya dhambi, Maisha yetu sikuzote ni ya dhuluma, tutawezaje kupona tusipouthamini wokovu mkuu namna hii?

Mithali 11:31 “Tazama, mwenye haki atalipwa duniani; Basi mwovu na mkosaji si mara nyingi Zaidi”

Adhabu hizi za mwilini zinafunua zile za rohoni..Wapo wanaodhani ukifa tu, ndio umekufa hakuna adhabu baada ya hapa…Adhabu ipo kwa wakosaji wote. Lakini Neema ya Mungu pia ipo kutukinga na adhabu hizo.

Na neema yenyewe ni kupitia YESU KRISTO. Tukimkabidhi Maisha yetu atatusamehe na kutugeuza na kutufanya kuwa wapya tena. Atafuta hata deni la dhambi na adhabu tulizostahili kuzipokea katika utoaji mimba wetu, katika uuaji wetu, katika rushwa zetu, katika uongo wetu, katika wizi wetu, katika uzinzi wetu, katika utapeli wetu n.k. Na hiyo ndio faida ya agano hili jipya la neema lililo katika damu ya YESU.

Hivyo kimbilia leo msalabani ikiwa bado hujaaokoka, tubu dhambi zako, ukabatizwe, usamehewe dhambi zako kisha upokee Roho Mtakatifu, atakaye kuwa na wewe hadi siku ile ya mwisho ya Unyakuo.

Bwana akubariki sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!

KWANINI UNAPASWA UJIWEKE TAYARI SASA, KABLA YA ULE WAKATI KUFIKA?.

USIJITAFUTIE KULAMBWA NA MBWA KWA DHAMBI YA KUTAMANI.

MAONO YA NABII AMOSI.

Je Mtu anaweza kusema uongo, Na Mungu akambariki?

MKUMBUKE MKE WA LUTU.

MPINGA-KRISTO

Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments