Je ni sahihi kumtenga mtu anapofanya dhambi kanisani?

Je ni sahihi kumtenga mtu anapofanya dhambi kanisani?

JIBU: Yapo makundi mawili kanisani..kundi la kwanza ni lile ambalo linahusisha washirika, ambalo ndani yake kuna wachungaji, waalimu, wainjilisti, mashemasi na waumini na wengineo…Kundi lote hili linahusisha washirika ambao tayari wameshamwamini Yesu Kristo, na kubatizwa na kupokea Roho Mtakatifu…hali kadhalika wameshajifunza Neno vya kutosha na kukolea katika maarifa ya ki-Mungu…hata kufikia kiasi cha kuweza kuwaelekeza na kuwaelekeza wengine katika njia ya wokovu.

Na kundi la pili ni lile la watu waliookoka karibuni, au walioingia katika Imani kipindi cha hivi karibuni..Wengi wa hawa unakuta ni wachanga kiimani, na mara nyingi wanakuwa ni wageni…Hivyo wanakuwa bado wanahitaji msaada katika kujifunza Imani na uweza wa Mungu..Na kwasababu wametoka katika ulimwengu bado kuna tabia baadhi baadhi wanakuwa hawajaziacha kutokana na kwamba pengine hawajajua Neno la Mungu linasemaje kuhusu mambo hayo wanayoyafanya.

Sasa katika lile kundi la kwanza ambalo linahusisha washirika ambao tayari wameshaijua kweli ya Mungu kwa utimilifu mkubwa…wameshajua na kufundishwa uasherati ni dhambi, wizi ni dhambi, ulevi ni dhambi n.k…Wakakengeuka na kurudia matapishi na kufanya mojawapo ya dhambi hizo ambazo tayari walishajifunza kuwa ni machukizo kwa Mungu…Mtu wa Namna hiyo kimaandiko ANAPASWA ATENGWE!!…Na endapo asipotengwa wale ambao wanapaswa wamtenge watakuwa WANAFANYA DHAMBI MBELE ZA MUNGU!!…Hivyo ni agizo la Mungu kwamba ni lazima atengwe…

Na kutengwa huko kunahusisha, yeye kutoonekana maeneo au mazingira ya kanisa kwa kipindi kirefu…Na washirika wengine hawatakiwi hata kumsalimia wala kushirikiana naye kwa lolote lile, hata hata kama atatubu…atakaa mwenyewe kwa kipindi chote hicho…mpaka wakati ambao Kanisa litasikia amani ya Roho kumrudisha…na wakati huo wa kutengwa huku akiwa katika hali ya toba na maombolezo, Mungu atakuwa anamrudi kwa aliyoyafanya. Hivyo hakuna raha yoyote katika kutengwa, kama kweli ni mtoto wa Mungu. Kwasababu asipotolewa katika kanisa, watu wote wataiga na hawatamwogopa Mungu..Hivyo ili kuzuia hilo, biblia imeruhusu kumwondoa mtu huyo ili kanisa zima lisiharibike…

Utauliza ni wapi maandiko yanasema hivyo?

1Wakorintho 5:1 “Yakini habari imeenea ya kuwa kwenu kuna zinaa, na zinaa ya namna isiyokuwako hata katika Mataifa, kwamba mtu awe na mke wa babaye.

2 Nanyi mwajivuna, wala hamkusikitika, ili kwamba aondolewe miongoni mwenu huyo aliyetenda jambo hilo.

3 Kwa maana kweli, nisipokuwapo kwa mwili, lakini nikiwapo kwa roho, mimi mwenyewe nimekwisha kumhukumu yeye aliyetenda jambo hilo, kana kwamba nikiwapo.

4 Katika jina la Bwana wetu Yesu, ninyi mkiwa mmekusanyika pamoja na roho yangu, pamoja na uweza wa Bwana wetu Yesu;

5 kumtolea Shetani mtu huyo, ili mwili uadhibiwe, ili na roho iokolewe katika siku ya Bwana Yesu.

6 Kujisifu kwenu si kuzuri. Hamjui kwamba chachu kidogo hulichachusha donge zima

9 Naliwaandikia katika waraka wangu, kwamba msichangamane na wazinzi.

10 Sisemi msichangamane kabisa na wazinzi wa dunia hii, au na wenye kutamani, au na wanyang’anyi, au na wenye kuabudu sanamu; maana hapo ingewalazimu kutoka katika dunia.

11 Lakini, mambo yalivyo, naliwaandikia kwamba msichangamane na mtu aitwaye ndugu, akiwa ni mzinzi au mwenye kutamani au mwenye kuabudu sanamu au mtukanaji au mlevi au mnyang’anyi; mtu wa namna hii msikubali hata kula naye.

12 Maana yanihusu nini kuwahukumu wale walio nje? Ninyi hamwahukumu hao walio ndani?

13 Lakini hao walio nje Mungu atawahukumu. Ninyi mwondoeni yule mbaya miongoni mwenu.”

Soma pia..

2Wathesalonike 3:14 “Na ikiwa mtu awaye yote halishiki neno letu la waraka huu, jihadharini na mtu huyo, wala msizungumze naye, apate kutahayari; 15 lakini msimhesabu kuwa adui, bali mwonyeni kama ndugu”.

Hivyo kuna hatari sana ya kufanya dhambi za makusudi baada ya kuujua ukweli..Tunakuwa tunakabidhiwa shetani ashughulike na sisi, Hivyo tujihakiki na Bwana atuepushe na hayo yote.

Maran atha!

Mada Nyinginezo:

Je! mtu aliyeokoka anaruhusiwa kumiliki Lodge ambayo ina Bar ndani yake?

Mahuru ndio nini?

Kwanini Mungu alisema hakuna mtu awazaye kuuona uso wake akaishi?

Je Mtu anaweza kusema uongo, Na Mungu akambariki?

Nini maana ya mstari huu: (Mtu ambarikiye mwenzake kwa sauti kuu asubuhi na mapema; Itahesabiwa kuwa ni laana kwake.Mithali 27:14 )?

Maana ya huu mstari ni ipi? Mithali 14:4 ‘Zizi ni safi ambapo hapana ngombe;bali nguvu za ngombe zaleta faida nyingi’.

Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments