Bawa la mbuni hufurahi; Lakini mabawa yake na manyoya yake, je! Yana huruma? 

Bawa la mbuni hufurahi; Lakini mabawa yake na manyoya yake, je! Yana huruma? 

SWALI: Nini maana ya haya maneno Mungu aliyomwambia Ayubu kuhusiana na  tabia za Mbuni?

Ayubu 39:13 Bawa la mbuni hufurahi; Lakini mabawa yake na manyoya yake, je! Yana huruma?  14 Kwani yeye huyaacha mayai yake juu ya nchi, Na kuyatia moto mchangani,  15 Na kusahau kwamba yumkini mguu kuyavunja, Au mnyama wa mwitu kuyakanyaga.  16 yeye huyafanyia ukali makinda yake, kana kwamba si yake; Ijapokuwa taabu yake ni ya bure, hana hofu;  17 Kwa sababu Mungu amemnyima akili, Wala hakumpa fahamu.  18 Wakati anapojiinua juu aende, Humdharau farasi na mwenye kumpanda. 


JIBU: Ukianzia kusoma mistari michache ya juu katika hiyo hiyo  sura  ya 39, Utaona Mungu anamweleza Ayubu baadhi ya wanyama ambao wanauwezo fulani mkubwa lakini hauwasidii kufanya mambo ya msingi, kwamfano mstari wa 5-8, anamtaja punda-milia, ni mnyama anayefanana na punda, ana nguvu na uwezo wa kukimbia zaidi hata ya punda, lakini je! Anamuuliza Ayubu unaweza kumkamata na kumfanya mtumwa wako akubebe mizigo? Au akulimie. Jibu ni la!

Mstari wa 9-12, anamtaja tena, Nyati, anamsifia nguvu zake, kwamba ni nyingi sana, lakini je utaweza kumfunga nira na kumwambia akulimie shamba lako kama ufanyavyo kwa ng’ombe? Jibu ni la kwasababu jambo hilo halipo ndani yake.

Na hapa kwenye mstari wa 13-18 Anamtaja tena Ndege mbuni na sifa zake. Anasema mabawa yake ni bora na mazuri, kiasi cha kuweza kuyatamia vema mayai ardhini zaidi ya ndege wengine wote duniani. Lakini kinyume chake ni kuwa mbuni ni ndege asiyejali mayai wala vifaranga vyake kuliko ndege wote unaowafahamu. Japokuwa anaouwezo mkubwa wa kuwashinda maadui zaidi ya ndege wote, lakini uwezo wake hautumii katika mambo yaliyo na faida. Mbuni anataga popote tu, hata kando ya njia,

hawezi kutafuta sehemu iliyo salama kama ndege wengine ambao huenda sehemu za maficho na kutaga huko ili watoto wao wawe salama pindi wazaliwapo lakini yeye hilo halijali, anataga popote apaonapo, matokeo yake ni aidha mayai yake kukanyagwa na wanyama wakubwa au kuibiwa na kenge au wanyama wengine wezi. Mbuni anaouwezo wa kutaga mpaka mayai 60 na kutamia yote yakatotolewa, lakini kwa tabia yake ya kutokujali anaweza kuambulia vifaranga viwili au vitatu tu. Anaweza kuyasahau mayai yake mchangani, jua au joto la mchangani likamsaidia kotolesha.

Na akishazaa, watoto wake awahudumii, kama wafanyavyo ndege wengine wadogo, ambao huakikisha wanazunguka huko na huko kutafuta vyakula vya watoto wao. Lakini bado maandiko haya yanaonyesha jinsi gani alivyomshapu kuliko hata farasi. Mwendo wa mbuni unauzidi mwendo wa farasi yoyote duniani. Kuonyesha jinsi alivyo mwepesi kujipigania lakini sio watoto wake.

Ni nini Mungu alikuwa anamwonyesha Ayubu ni kwamba, uwezo wa kufanya jambo Fulani sio tija ya mtu huyo kulitenda, kama Mungu hakumpa moyo huo. Wapo wenye mali nyingi, lakini hawana moyo wa kusaidia wanyonge, wapo wenye vipawa vizuri lakini hawezi kumwimbia Mungu. Nguvu zao ni bure hazina faida, wapo wenye uwezo wa kufundisha lakini hawewezi kujinyenyekeza chini ya makusudi ya Mungu watumiwe ili kuujenga ufalme wa Mungu, wanakuwa tu kama punda-milia wa nyikani.

Wapo wenye uwezo wa kulichunga kundi la Mungu lakini wanakuwa kama mbuni, nguvu zao, ukubwa wao hauwasaidii katika kujali kazi ya Mungu. Lakini Bwana akikupa moyo huo, basi utafanya hata kama utakuwa ni dhaifu, utafanya tu. Na hili ndio jambo ambalo tunapaswa tumwombe Bwana . ATUPE MOYO WA KUMTUMIKIA YEYE. Tusitazame kwamba mpaka tupate kitu Fulani ndio tuweze, mpaka tukasomee uchungaji ndio tuweze kuchunga, mpaka tupate pesa ndio tuweze kuisapoti kazi ya Mungu, Bwana atupe moyo huo tangu sasa wakati hatuna uwezo wowote. Kwani huo ndio utakaotusukuma kufanya makubwa.

Lakini pia yapo mambo matatu tunaweza kujifunza:

Jambo la kwanza ni sisi wenyewe, tusiwe kama mbuni ambao hatujali kuhudumia vinavyozalika ndani ya roho zetu. Kwa kutengeneza viota vyetu mahali salama,kinyume chake tunamwachia shetani azichukue mbegu zetu rohoni zinazopandwa, tunaziacha juu juu na matokeo yake ibilisi anakuja kuzila sawasawa tu na mfano wa mpanzi ambao Yesu aliutoa juu ya zile mbegu zilizoangukia njiani ndege wakazila. Ndivyo ilivyo maisha ya wengi, wanapolisikia Neno la Mungu badala walitunze na kulipalilia ndani yao  ili liwazalie matunda wao wanazembea tu, wanaishi kama wanavyotaka. Hivyo tunakuwa wapumbavu kama mbuni, kwa kutokuzalisha chochote.

Jambo la pili: Linahusu familia: Wazazi wasiowajali watoto wao, Ni wajibu kwa mzazi kuwatunza wanawe, kwa kuwahudumia kimwili na kiroho. Imekuwa rahisi leo hii wazazi kujali sana Elimu za watoto wao jambo ambalo ni zuri, lakini kuhusiana na maisha yao ya kiroho wamewaweka nyuma . Hiyo ni hatari kubwa sana, usipompa Mungu watoto wako awalee, shetani atakusaidia kuwaelea. Na matokeo yake utayaona baadaye watakapokuwa watu wazima. Kama mzazi jali sana maisha ya kiroho ya watoto wako, wapeleke Sunday school, wapeleke katika semina za watoto kanisani, wahubirie, wafundishe kuomba, kufunga, kuimba nyimbo za wokovu n.k.

Jambo la tatu: Ni kuhusu watumishi wa Mungu. Bwana hataki tuwe kama Mbuni katika eneo la kulichunga kundi lake. Tunachowaza ni kujijali sisi tu, lakini kuwafuatilia na kuwachunga kondoo wa Bwana tunaona uvivu. Tunasahau kuwa shetani huko nje! Anafanya kazi usiku na mchana kuwarudisha tena ulimwenguni. Hivyo ni angalizo kwetu sisi watumishi wa Mungu. Popote ulipo hakikisha unalilisha na kulichunga kundi la Mungu dhidi ya Yule mwovu. Tuwe na hekima za ‘chungu’

Bwana akubariki sana.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Hawa ndege katika Walawi 11:13-19 ndio ndege gani kwasasa?

NI NINI KINATOKA KINYWANI MWA MTOTO WAKO?

“Humfukuza punda wake asiye baba”, nini maana ya mstari huu? (Ayubu 24:3)

HUDUMA YA (ELIFAZI, SOFARI, NA BILDADI).

Kuvyaza ni nini katika biblia? (Ayubu 21:10).

KWANINI NI NUHU, AYUBU NA DANIELI?

Marijani ni nini katika biblia(Ayubu 28:18,Mithali 8:11)?

Santuri ni nini? (Danieli 3:5,10)

HUTATAMBUA LOLOTE, SIKU YA UNYAKUO IKIFIKA.

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments