Ni sahihi kwa mkristo kupokea fedha kutoka kwa mtu anayefanya kazi haramu?

Ni sahihi kwa mkristo kupokea fedha kutoka kwa mtu anayefanya kazi haramu?

Je! ni sahihi kwa mkristo kupokea fedha kutoka kwa mtu anayefanya kazi haramu kama za uuzaji wa dawa ya kulevya, wizi au bangi?

Jibu: Kama wewe ni mtu uliyeokoka, aidha mchungaji, au mwalimu, au muimbaji au mshirika wa kawaida, sio sahihi kupokea fedha zozote kutoka kwa mtu anayefanya kazi haramu kama za ujambazi au wizi, au uuzaji wa madawa ya kulevya, kwasababu kwa kufanya vile ni sawa na kushiriki zile kazi.

Kwasababu huwezi kupenda fedha za mtu mwovu, halafu ukachukia na kazi zake.. Huwezi kupenda boga halafu ukachukia ua lake.. Mpaka umekikibali kitu maana yake tayari umekikubali na chanzo chake..

Hivyo kama utapokea fedha kutoka kwa mtu anayeuza madawa ya kulevya, au jambazi, tayari moja kwa moja umehakikia chanzo chake na kukikubali!, lakini kama umekikataa chanzo chake pia huwezi kukubali matunda ya chanzo hicho, Kama Bwana Yesu alivyosema katika…

Luka 6:43 “Kwa maana hakuna mti mzuri uzaao matunda mabaya, wala mti mbaya uzaao matunda mazuri;

44  kwa kuwa kila mti hutambulikana kwa matunda yake; maana, katika miiba hawachumi tini, wala katika michongoma hawachumi zabibu”

Kwahiyo kibiblia sio sahihi kwa mtu aliyeokoka kupokea fedha kutoka kwa mtu anayefanya kazi haramu, aidha kwa lengo la kuendeleza huduma, au kwa lengo la kujiendeleza yeye mwenyewe. Ni sharti kwanza mtu huyo ageuzwe njia zake kwa kumpokea Yesu kikamilifu na kubadili kazi yake hiyo kwa kufanya kazi halali, ndipo fedha zake ziwe safi. (Hapo atakuwa ameufanya mti wake kuwa mzuri na matunda yake kuwa mazuri)

Na sio tu kupokea, vilevile watu hao wafanyao kazi haramu kibiblia hawaruhusiwi kuzipeleka fedha zao kama sadaka au zaka katika nyumba ya Mungu, kwani ni machukizo makubwa sana..

 Mithali 15:8 “Sadaka ya mtu mbaya ni chukizo kwa Bwana; Bali maombi ya mtu mnyofu ni furaha yake”.

Soma pia Kumbukumbu 23:18 na Mithali 21:27.

Kwahiyo ni lazima kuvifanya vyanzo vyetu kuwa safi, ndipo na matunda ya vyanzo hivyo yawe safi, lakini kama vyanzo ni vichafu hata matunda yake yatakuwa machafu tu, kwa anayetoa na anayepokea. Ndio maana asilimia kubwa ya wanaopokea fedha kutoka kwa watu wanaofanya biashara haramu, zile fedha wanazozipokea ni lazima zitakuja kuwaletea madhara kwa namna moja au nyingine, kwasababu zinakuja na roho na maagizo ya ibilisi nyuma yake.

Bwana atusaidie.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Mwana haramu ni nani kibiblia? (Kumbukumbu 23:2).

Nini maana ya “kila tendo lisilotoka katika imani ni dhambi?”

KANUNI RAHISI YA KUPOKEA BARAKA MARA DUFU.

JINSI YA KUMSIKIA MUNGU, NA KUPOKEA MAFUNUO AU JUMBE KUTOKA KWAKE.

Atakapokuja Mwana wa Adamu, je! Ataiona imani duniani? Maana yake nini?

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
2 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Loanyuni Tarakwa
Loanyuni Tarakwa
1 year ago

Je, mchungaji kuwaombea watu wanaobeti ili washinde ni sahihi..?!

NEEMA ALICE
NEEMA ALICE
1 year ago

MUNGU akubariki sana mtumishi wa Mungu Kwa neno hili lakini je Kwa mfano yule anayepokea fedha Kwa mtu anayefanya kazi ya haramu na pengine hajui kazi ya mwenye analeta pesa itakuwa naye amo dhambini? Naomba jibu