KANUNI RAHISI YA KUPOKEA BARAKA MARA DUFU.

KANUNI RAHISI YA KUPOKEA BARAKA MARA DUFU.

Jina la Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo, Mkuu wa mbingu na nchi libarikiwe.

Kitabu pekee chenye mwongozo kamili wa maisha ni biblia takatifu, Mtu mmoja wa Mungu aliwahi kusema “endapo nikifungiwa katika chumba chenye giza, nikapewa mshumaa na biblia, basi ninaweza kueleza yote yanayoendelea nje katika ulimwengu”.

Hakika hiyo ni kweli kabisa..kwasababu biblia ndio kitabu pekee kinachoelezea uhalisia wa nyakati na majira tunayoishi, na mambo yajayo..

Leo napenda tujifunze kanuni moja rahisi ya kupokea baraka..Wengi wetu, tunategemea maombi tu, tunakuwa tunatumia nguvu nyingi katika kuomba ili kusudui tupokee baraka katika mwili, lakini ipo kanuni moja rahisi ya kupokea baraka.. Na kanuni hiyo Bwana Yesu aliisema katika Marko 4:24..

Marko 4:24 “Akawaambia, Angalieni msikialo; kipimo kile mpimacho NDICHO MTAKACHOPIMIWA, na TENA MTAZIDISHIWA”.

Hapo nataka tuyatazame hayo maneno miwili. 1)Kipimo mpimacho ndicho mtakachopimiwa. na 2) tena mtazidishiwa

Maana yake ni kwamba Kama utampimia mwingine kwa kumpa “sh.elfu moja”..basi Bwana atahakikisha anakurudishia kwa njia nyingine hiyo “elfu moja” uliyoitoa. (Huenda ikawa siku hiyo hiyo, au wakati mwingine ambao haupo mbali sana).

Lakini haiishii hapo tu kukurudishia hiyo elfu moja..bali anaendelea kwa kusema “na tena mtazidishiwa”.

Ikiwa na maana kuwa Bwana akishakurudishia kile ulichokitoa, sasa kinachofuata ni yeye kukulipa wema ulioufanya kwa “kwa kukuzidishia”.

Maana yake atakupa na kingine kingi zaidi ya hiyo elfu moja uliyoitoa,

Sasa ili tuelewe vizuri ni kiasi gani tutazidishiwa, hebu tuyatazame tena maneno ya Bwana Yesu katika Luka 6:38.

Luka 6:38 “Wapeni watu vitu, nanyi mtapewa; kipimo cha kujaa na kushindiliwa, na kusukwa-sukwa hata kumwagika, ndicho watu watakachowapa vifuani mwenu. Kwa kuwa kipimo kile kile mpimacho ndicho mtakachopimiwa”.

Hapa nataka tuugawanye tena mstari huu katika sehemu mbili.

1) Wapeni watu vitu nanyi mtapewa na 2) Kipimo cha kujaa na kushindiliwa na kusukwa-sukwa hata kumwagika, ndicho watu watakachowapa kifuani mwenu.

Maana yake tunapowapa watu, kipimo fulani labda elfu moja na sisi Bwana ataturudishia hichohicho kipimo cha sh elfu moja…lakini hataishia hapo, kwasababu akishaturudishia kipimo kile tulichokitoa, ndipo anaanza kutubariki kwa wema tulioufanya, sasa swali anatubariki vipi?..

Anatubariki kwa kutumia hao hao watu kutupa sisi vitu vifuani mwetu kwa kipimo cha kujaa na kushindiliwa, na kusukwa-sukwa hata kumwagika..Haleluyaa!!

Kwahiyo kama umetoa elfu moja kwa moyo mzuri na mwema Basi Bwana atakurudishia hiyo elfu moja yako, na atakuzidishia na nyingine nyingi kwa kiwango cha kujaa na hata kumwagika…(unaweza kutafakari jinsi zilizvyo nyingi fadhili zake)..huenda ikawa zaidi ya mamilioni..

Jifunze kuwa mtoaji, kama unataka kupata baraka maradufu.

Maran atha

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Ni rahisi zaidi ngamia kupenya tundu ya sindano.

Ni lini na wapi Ibrahimu aliioona siku ya Bwana akashangilia?.

JINSI YA KUMSIKIA MUNGU, NA KUPOKEA MAFUNUO AU JUMBE KUTOKA KWAKE.

JINSI YA KUPOKEA UPONYAJI, TUNAPOMWOMBA BWANA ATUGUSE MARA YA PILI.

Talanta ni nini katika biblia (Mathayo 25:14-30)

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
1 Comment
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Clementsangai
Clementsangai
1 year ago

Bwana Yesu asifiwe nikituma haya masomo kwenda katika e mail yangu kuwa pdf file mbona yana kataa.!?