WALIKUWA WAMECHOKA NA KUTAWANYIKA KAMA KONDOO WASIO NA MCHUNGAJI.

WALIKUWA WAMECHOKA NA KUTAWANYIKA KAMA KONDOO WASIO NA MCHUNGAJI.

Nakusalimu katika jina la mwokozi wetu Yesu Kristo.  Nakukaribisha tena tuzidi kuyatafakari maandiko.

Moja ya mambo ambayo, yalimuhuzunisha sana Bwana Yesu ni pale alipowatazama watu wake na kuwaona wanafanana  na kundi la kondoo wafugwao waliopoteza tumaini kabisa na kutawanyika, kila mmoja mahali pake anapopajua yeye..Ina huzunisha sana..

Embu Tusome; kwa utulivu habari hiyo; 

Mathayo 9:35-36

[35]Naye Yesu alikuwa akizunguka katika miji yote na vijiji, akifundisha katika masinagogi yao, na kuihubiri habari njema ya ufalme, na kuponya magonjwa yote na udhaifu wa kila aina.

[36]Na alipowaona makutano, aliwahurumia, kwa sababu walikuwa WAMECHOKA na KUTAWANYIKA kama kondoo wasio na mchungaji.

Hapo biblia inasema walikuwa WAMECHOKA..na KUTAWANYIKA.

Kuchoka kunakozumgumziwa hapo, sio tu kule kwa kutembea umbali mrefu, katika kutafuta  chakula / maji…hiyo ni sehemu ya kwanza..Bali kuchoka kunakolengwa hapo hasaa kunakuja kutokana na kukandamizwa, kujeruhiwa, na kufukuzwa, kutishwa..pamoja na hofu na wasiwasi wa mashaka ya kuraruliwa na mbwa mwitu wakali.

Hii ndio hali halisi yasasa.. Watu wa Mungu WAMECHOKA. Sio kidogo bali wamechoka kwelikweli, Kutokana na kudanyanywa, kuumizwa na watumishi wa uongo, wameharibiwa, wametawanywa.., manabii wa uongo wamechukuliwa fedha zao wakiwaahidia kubarikiwa na kufunguliwa, lakini mwisho wa siku wanajikuta wapo katika matatizo zaidi, wanahangaika huku na kule kutafuta msaada wa kumkaribia Mungu, lakini hawauoni,

 badala wapewe tiba ya Neno la Mungu wanapewa maji ya upako, wanafika makanisani badala wahubiriwe Yesu, wanahubiriwa bikira Mariamu na watakatifu wa kale, na sala za wafu, badala wahubiriwe neema iliyo katika Kristo Yesu, wanahubiriwa siri zilizo ndani ya wachawi.

Imefikia hatua watu wamekata tamaa kabisa, kila mmoja anaona ni heri, asiamini kanisa lolote, ajisalie tu peke yake nyumbani..kuliko kwenda na kusikiliza madanganyo. Ni ni mbaya sana..

Ndio jambo ambalo Bwana Yesu analiona sasa hivi ulimwenguni..na kulihurumia kundi lake  jinsi lilivyotawanyika…na kuonewa sana..

Ikiwa wewe ni mhubiri, halafu hutimizi wajibu wako wa kuwaongoza watu katika njia sahihi..ujue kuwa utawajibishwa siku ile mbele za Bwana.

Kama tunaigeuza  kazi ya Mungu biashara, hatujali maisha ya kiroho ya watu wa Mungu, hata wakija watakavyo kanisani tunaona ni sawa, …tufahamu kuwa tutawajibishwa na Bwana siku ile.

Yeremia 23:1-4

[1]Ole wao wachungaji, wanaoharibu kondoo za malisho yangu na kuwatawanya! Asema BWANA.

[2]Kwa sababu hiyo BWANA, Mungu wa Israeli, asema hivi, juu ya wachungaji wanaowalisha watu wangu, Mmetawanya kundi langu, na kuwafukuza, wala hamkwenda kuwatazama; angalieni, nitawapatiliza uovu wa matendo yenu, asema BWANA.

[3]Nami nitakusanya mabaki ya kundi langu, katika nchi zile zote nilizowafukuza, nami nitawaleta tena mazizini mwao; nao watazaa na kuongezeka.

[4]Nami nitaweka juu yao wachungaji watakaowalisha; wala hawataona hofu tena, wala kufadhaika, wala hatapotea hata mmoja wao, asema BWANA.

Tujiulize, sisi tunaosema tumeitwa kumtumikia Bwana.. Ni utumishi gani tunaoufanya? Tunadhani watu wa Mungu watapotezwa sikuzote?

Mungu anajua kuwakusanya watu wake. Na atawanyanyulia watumishi waaminifu. Sawasawa na Neno lake. Lakini sisi wengine tutawajibishwa.

Bwana atusaidie.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Gongo na Fimbo ni nini? Na vinawezaje kumfariji mtu? (Zaburi 23:4).

JE! UNAMPENDA BWANA?

USIYADHARAU MARUDIA YA BWANA.

“Nitampiga mchungaji na kondoo wa kundi watatawanyika”,Maana yake nini?

NI LIPI KATI YA MAKUNDI HAYA, WEWE UPO?

HUTATAMBUA LOLOTE, SIKU YA UNYAKUO IKIFIKA.

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
2 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Anonymous
Anonymous
7 months ago

mugu akubaliki amen

Emmanuel Kitengule
Emmanuel Kitengule
1 year ago

Bwana akubariki sana mwalimu kwa ujumbe uletao uzima.