TUNA JUKUMU LA KWENDA KUTEKA MATEKA.

TUNA JUKUMU LA KWENDA KUTEKA MATEKA.

Shalom, mtu wa Mungu..karibu tuyatafakari maandiko pamoja,

Biblia inasema…

2Wakorintho 10:3 “Maana ingawa tunaenenda katika mwili, hatufanyi vita kwa jinsi ya mwili;

4 (maana silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome;)”

Kazi ya kwenda kuvua watu inafananishwa na shughuli za wanajeshi vitani…Wanajeshi wanapotaka kushambulia mahali huwa hawampi adui taarifa…na wanafanya hivyo, wanashtukiza tu…na wakisha angamiza wote wanateka mateka na kuchukua nyara vitu vyao..

Na katika kazi ya uvuvi wa watu ni hivyo hivyo…Hatupaswi kuingia mkataba na adui, wala kushauriana naye…tunachopaswa kufanya ni kila mara kuvamia kambi ya adui na kuteka mateka..

Unaposikia msukumo wa kuhubiri, sio suala la kusema hapa panafaa au hapafai..unachopaswa kufanya ni unavamia!…kwasababu katikati ya kambi ya Adui kuna mateka…na mateka unawaweka huru kwa kuwavamia..Ingawa vita utakutana navyo hiyo ni kawaida hata kambi ya adui akivamiwa ghafla ni lazima ijibu mashambulizi kidogo hata kama inajua itakwenda kushindwa..

Ukiwa shuleni, hata mwanya mdogo unaoupata, usipoteze muda…hubiri Habari njema, ukiona mgonjwa mahali mwanya huo ulioupata mnyang’anye shetani hilo teka…Mwombee apone na mhubirie, Ukikutana na mtu mwenye mapepo..itumie hiyo fursa vizuri, ya kuyakemea hayo mapepo yamwondoke na kumweka huru huyo mtu, na kisha Mweleze Habari za Yesu…

Usitazame huyu ni mkubwa kuliko mimi hawezi kunisikiliza, huyu ana elimu kuliko mimi, huyu ana heshima kuliko mimi, anavaa vizuri kuliko mimi, ni mwalimu wangu, ni kiongozi wangu, au nimekutana naye tu siku ya kwanza usiyaangalie hayo hata kidogo.. Kwasababu silaha ulizo nazo zina NGUVU! Kuifanya kila Fikra imtii Kristo. Wapo maprofesa waliobadilishwa fikra zao wakamtii Kristo na watu ambao hawajasoma hata darasa moja..Wapo maraisi waliowekwa huru na injili ya watu ambao hawajasoma hata darasa moja. Wapo waliokuwepo sugu lakini leo hii ni watumishi wa Mungu. Kwahiyo vaa silaha na ingia kazini..

Nguvu ile ile iliyokubadilisha wewe ndiyo hiyo hiyo itakayowabadilisha na wengine..wewe mpaka umemtii Kristo ni kwasababu Kristo alimtumia Mtumishi wake kuja kumnyang’anya shetani wewe ambaye ulikuwa mtumwa wake…Na baada ya kumpokonya shetani ndipo akakufanya wewe kuwa TEKA lake. Na hakuishia hapo akakupa na wewe Kipawa (yaani karama)..ambayo ni silaha na kazi yake mojawapo ni kwenda na wewe kuteka mateka mengine na kuyaleta kwa Kristo.

Waefeso 4:7 “Lakini kila mmoja wetu alipewa neema kwa kadiri ya kipimo cha kipawa chake Kristo.

8 Hivyo husema, Alipopaa juu aliteka mateka, Akawapa wanadamu vipawa”.

Hivyo kama umempa Kristo Maisha yako…ni jukumu lako kwenda kuteka mateka…kwasababu tayari silaha unayo…kama ni mtaani ingia anza kuhubiri, na utaona matokeo, kama ni shuleni ni hivyo hivyo, kama ni kusafiri huko na huko fanya hivyo kwa nguvu zote kwa karama Mungu aliyoiweka ndani yako, kama ni katika mahospitali na magereza..usikawie kawie..Nenda kwasababu Mungu atakuwa Pamoja nawe siku zote kukuongoza… yakumbuke haya maneno ya Yesu mwenyewe Bwana wetu aliyoyasema..

Mathayo 28:18 “Yesu akaja kwao, akasema nao, akawaambia, Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani.

19 Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu;

20 na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi; NA TAZAMA, MIMI NIPO PAMOJA NANYI SIKU ZOTE, HATA UKAMILIFU WA DAHARI”

Atakuwa Pamoja na wewe hata ukamilifu wa dahari!…dahari maana yake ni nyakati/wakati….Hivyo hapo maana yake ni kwamba ameahidi kuwa “Pamoja nasi mpaka mwisho wa nyakati”…Lakini hiyo ni kama tutaondoka na kwenda kuwafanya mataifa yote kuwa wanafunzi…na kuwafanya kuwa mateka wa Kristo.

Bwana atusaidie kumuamini..

Kumbuka pia katika kwenda kuhubiri kuwa mwaminifu na kuwa na nia ya Kristo, sio nia ya kuwa maarufu au kutafuta fedha, bali ya kutafuta roho za watu…huku ukijua kuwa una thawabu yako mbinguni na Kristo anakuja upesi..

Ufunuo 22:12 “Tazama, naja upesi, na ujira wangu u pamoja nami, kumlipa kila mtu kama kazi yake ilivyo.

13 Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho, wa kwanza na wa mwisho”.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

MKUU WA UZIMA AKUWEKE HURU.

Kuungama ni nini?

UTASIMAMA PEKE YAKO SIKU ILE.

Katika biblia Neno “Mshenzi” linatajwa.Kwanini liwekwe?

KUTAKUWA NA MATETEMEKO YA NCHI, NJAA NA TAUNI.

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!

USIPUNGUZE MAOMBI.

Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments