Kuungama ni nini?

Kuungama ni nini?

SWALI: Kuungama maana yake ni nini?

JIBU: Maana ya kuungama ni “kukiri jambo kwa wazi” kukubali….Kwamfano mtu anayetubu kwa kuzikiri dhambi zake kwa wazi kwamba yeye ni mwenye dhambi mbele za Mungu, mtu huyo ni “ameungama dhambi zake”

1Yohana 1:9 “Tukiziungama dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu na wa haki hata atuondolee dhambi zetu, na kutusafisha na udhalimu wote”.

Mathayo 3:5 Ndipo walipomwendea Yerusalemu, na Uyahudi wote, na nchi zote za kandokando ya Yordani;

6 naye akawabatiza katika mto wa Yordani, huku wakiziungama dhambi zao”.

Kadhalika kuikiri imani mbele za watu ni “kuiungama imani”..na kuukiri uongo ni kuungama uongo!

Bwana wetu Yesu Kristo alipopelekwa mbele ya Pontio Pilato, na Pilato alipomwuliza je wewe ndiwe Kristo?..Alikiri (aliungama) wazi kuwa yeye ndiye!

Luka 23:3 “Pilato akamwuliza, akisema, Wewe ndiwe mfalme wa Wayahudi? Akajibu akamwambia, Wewe wasema”…..

Neno “wewe wasema” maana yake ni “kama ulivyosema”..Kwahiyo Kristo alikiri kwa wazi pasipo hofu mbele ya Pilato kwamba yeye ndiye Kristo!..Hivyo aliungawama Imani yake kwa wazi.

1Timotheo 6:13 “Nakuagiza mbele za Mungu anayevihifadhi hai vitu vyote, na mbele za Kristo Yesu, ALIYEYAUNGAMA MAUNGAMO MAZURI yale mbele ya Pontio Pilato,

14 kwamba uilinde amri hii pasipo mawaa, pasipo lawama, hata kufunuliwa kwake Bwana wetu Yesu Kristo”

Kadhalika na sisi kama hatujatubu mbele za Mungu…tunapaswa tuziungame dhambi zetu kwanza, (maana yake tuzikiri kwa dhati kwamba sisi ni wenye dhambi, tusipokiri na kukubali kwamba sisi ni wakosaji mbele zake kamwe hatuwezi kupata msamaha kutoka kwake!)..kisha tumwombe Mungu rehema naye atatusamehe…Na tukiishaziungaa dhambi zetu na kuipokea Imani kwa kumwamini mwanawe mpendwa Yesu Kristo tunapaswa kila siku TUUNGAME MAUNGAMO YA IMANI YETU!…maana yake tuikiri Imani ya kikristo kila mahali tuendapo, na popote pale tusimamishwapo pasipo hofu wala kujali ni nani yupo mbele yetu!..kama Bwana wetu Yesu alivyoungama..

1Timotheo 6:12 “Piga vita vile vizuri vya imani; shika uzima ule wa milele ulioitiwa, UKAUNGAMA MAUNGAMO MAZURI MBELE YA MASHAHIDI WENGI”.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

NI NANI ATAKAYETUTENGA NA UPENDO WA KRISTO?

YONA: Mlango wa 4

Je ni sahihi kumtenga mtu anapofanya dhambi kanisani?

TOFAUTI KATI YA HEKALU, SINAGOGI NA KANISA NI IPI?

Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments