Ebenezeri/ Ebeneza maana yake ni nini?

Ebenezeri/ Ebeneza maana yake ni nini?

Maana ya Neno Ebenezeri ni jiwe la msaada.

Wakati ule Israeli wanamlilia Bwana awarudie, Wafilisti walipata taarifa wakakusanyika pamoja ili wawaangamize, Israeli walivyoona hivyo wakaogopa sana, wakamsihi Samweli awalilie kwa Bwana ili wasaidiwe kwasababu wanakwenda kuangamia. Na Mungu akasikia kilio chao, akawatetea, kwa kutoa ngurumo kubwa sana, zilizowadhoofisha wafilisti, hivyo wakapigwa na kuharibiwa, mpaka miji ambayo wafilisti walikuwa wameiteka ikarudishwa yote kwa Israeli. Ndipo Samweli akachukua jiwe kubwa akalisimamisha Kati ya Mispa na Sheni, akaliita Ebenezeri, akasema hata sasa Bwana ametusaidia.

1Samweli 7:12 Ndipo Samweli akatwaa jiwe, na kulisimamisha kati ya Mispa na Sheni, akaliita jina lake Eben-ezeri, akisema, Hata sasa Bwana ametusaidia.

Lakini la kujiuliza kwanini Samweli anyanyue jiwe, na sio kitu kingine labda nguzo au bendera? Na pia alikuwa na maana gani kusema “Hata sasa Bwana ametusaidia”? Na sio maneno mengine?

JIBU: Alinyanyua jiwe kwasababu alipata ufunuo wa aliyemsaidia, na huyo si mwingine zaidi ya  Kristo ambaye ndio jiwe letu (Warumi 9:33). Alitambua ni yeye ndiye aliyewapigania vita kwa kunguruma, Kwasababu ndiye simba wa Yuda.

Lakini pia kwanini aseme “Hata sasa Bwana ametusaidia” ni kwasababu alitambua kuwa Mungu ni msaada wao sikuzote, hadi ule wakati walioufikia bado alikuwa ni msaada wao, ndio maana akasema “Hata sasa Bwana ametusaidia”, yaani sio tu jana, au zamani bali hata sasa Bwana yupo pamoja nasi.

Ikiwa na maana kuwa hata na sisi tukiwa ndani ya Kristo wakati wote atatulinda,  sio jana tu peke yake, hadi leo na hata kesho. Ni furaha iliyoje kuwekwa chini ya huu mwamba Yesu Kristo?

Je! Kristo ni jiwe lako? Je! Ni Ebenezeri wako? Kama sio, embu mkaribishe leo maishani mwako akuokoe, upate uzima wa milele. Akulinde mbali na Yule mwovu. Ikiwa upo tayari kutubu na kumpokea Yesu basi fungua hapa kwa msaada wa sala ya Toba >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

CHAGUA NI JIWE LIPI LITAKALO KUFAA KWA UJENZI.

BASI, IWENI NA HURUMA, KAMA BABA YENU ALIVYO NA HURUMA

LIONDOE JIWE.

Usimwache rafiki yako mwenyewe, wala rafiki ya baba yako.

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments