Uadilifu ni nini kibiblia?

Uadilifu ni nini kibiblia?

Uadilifu ni neno pana linalomaanisha, nidhamu, utu, auminifu, yaani kutenda kile ambacho jamii husika inataka wewe ukitende.

Kibiblia uadilifu ni utiifu katika sheria ya Mungu. Vilevile uaminifu na nidhamu katika mambo yote ya ki-Mungu.  Mtu wa namna hiyo anaitwa mwadilifu, au mcha Mungu.

Kwamfano watu ambao walikuwa waadilifu katika biblia ni kama Yusufu, Ayubu, Danieli pamoja na wengine, ambao waliweza kutembea katika sheria za Mungu bila lawama yoyote.

Baadhi ya vifungu ambavyo utakutana na Neno hilo ni hivi;

2Nyakati 26:3 Uzia alikuwa na umri wa miaka kumi na sita alipoanza kutawala; akatawala huko Yerusalemu miaka hamsini na miwili; na jina la mamaye aliitwa Yekolia wa Yerusalemu.  4 Akafanya yaliyo ya adili machoni pa Bwana, sawasawa na yote aliyoyafanya Amazia babaye

Zaburi 64: 10 “Mwenye haki atamfurahia Bwana na kumkimbilia, Na wote wenye moyo wa adili watajisifu”

Zaburi 112: 2 Wazao wake watakuwa hodari duniani; Kizazi cha wenye adili kitabarikiwa.  3 Nyumbani mwake mna utajiri na mali, Na haki yake yakaa milele.  4 Nuru huwazukia wenye adili gizani; Ana fadhili na huruma na haki

Soma pia 2Nyakati 27:2,29:2 Zaburi 140:13.

Lakini cha kujua kuhusu tabia hii, ni kwamba Bwana Yesu alisema ni wajibu pia wa kila kiongozi wa kiroho/ Mhubiri kufundisha mafundisho ya adili, zaidi ya mafundisho ya utoaji.

Luka 11:42  Lakini, ole wenu, Mafarisayo, kwa kuwa mwatoa zaka za mnanaa na mchicha na kila mboga, na huku mwaacha mambo ya adili, na upendo wa Mungu; iliwapasa kuyafanya hayo ya kwanza, bila kuyaacha hayo ya pili.

Mafundisho ya adili, ni kama vile, utakatifu, auminifu, haki, utu wema, amani, umoja na kiasi, uvumilivu, fadhili, upole, unyenyekevu. na yote yanayofanana na hayo. Kwasababu ndicho Bwana anataka kukiona ndani ya mioyo ya watu wake, wawe waadilifu kama yeye alivyo mwadilifu (Zaburi 25:8).

Je! Wewe ni mwadilifu? Kumbuka huwezi kuwa hivyo kama upo nje ya Kristo. Yeye ndio pekee anayeweza kukupa nguvu ya kutenda mema. Hivyo ili uitwe mwadilifu sharti kwanza umpokee Yesu akuokoe, akusamehe dhambi zako. Ndipo Bwana akupe nguvu ya kumcha yeye.

Ikiwa upo tayari leo kuokoka, basi fungua hapa kwa mwongozo wa Sala ya Toba. >> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

IMANI YENYE MATENDO;

NINI TOFAUTI KATI YA MATENDO YA SHERIA NA MATENDO YA IMANI?

JE KUHUDUMU KWA NYIMBO ZA INJILI KUKOJE?

MWIMBIE BWANA ZABURI KATIKA NYAKATI ZA FURAHA.

NYAKATI SABA ZA KANISA NA WAJUMBE WAKE.

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments