Uishi kwa furaha pamoja na mke umpendaye, siku zote

Uishi kwa furaha pamoja na mke umpendaye, siku zote

SWALI: Naomba kufahamu maana ya hivi vifungu katika maandiko

Mhubiri 9:7-10

[7]Wewe enenda zako, ule chakula chako kwa furaha, unywe mvinyo yako kwa moyo wa kuchangamka; kwa kuwa Mungu amekwisha kuzikubali kazi zako.

[8]Mavazi yako na yawe meupe sikuzote; wala kichwa chako kisikose marhamu.

[9]Uishi kwa furaha pamoja na mke umpendaye, siku zote za maisha yako ya ubatili, ulizopewa chini ya jua; siku zote za ubatili wako, kwa maana huo ni sehemu yako ya maisha; na katika taabu zako ulizozitaabika chini ya jua.

[10]Lo lote mkono wako utakalolipata kulifanya, ulifanye kwa nguvu zako; kwa kuwa hakuna kazi, wala shauri, wala maarifa, wala hekima, huko kuzimu uendako wewe.

JIBU: Kitabu Cha mhubiri ni kitabu kinachoelezea uhalisi wa maisha, mambo mazuri lakini pia mambo mabaya yaliyopo duniani mwanadamu anayoyasumbukia, yasiyokuwa na faida. Pamoja na siri nyingi mwanadamu asizoweza kuzivumbua, isipokuwa Mungu tu peke yake

Kwamfano anasema Dunia imejaa uchovu usioneneka, mambo yote ni ubatili kwasababu hakuna jipya chini ya jua mwisho wa siku tutayaacha yote hapa duniani.(Mhubiri 1:8)

Lakini pia pamoja na hayo hatupaswi kuyakinai maisha, kwani pia Yana mambo mazuri ambayo mwanadamu anaweza kuyafurahia endapo ataishi katika kumcha Mungu, 

Ndipo hapo anasema.ule chakula chako, uvae mavazi meupe, uishi Kwa furaha pamoja na mke umpendaye siku zote za maisha Yako, ufurahie matunda ya kazi uliyoifanya maadamu tayari Mungu ameshakuridhia…yaani tayari upo ndani ya Kristo.

Hivyo Kama Mahali Mungu alipokuweka panastahili kufurahi basi furahi tu, kwasababu ni Mungu kakubariki, huku ukiwa ndani ya Bwana, kama ni mke Bwana kakupa mfurahie, kama ni mavazi mazuri vaa..Kwani mambo hayo ni ya hapa hapa tu duniani, Bwana ametukirimia,.Hatutakwenda nayo kule ng’ambo.

Sehemu nyingine anasema.

Mhubiri 8:15

[15]Kisha nikaisifu furaha, kwa sababu mwanadamu hana neno lo lote lililo jema chini ya jua, kuliko kula, na kunywa, na kucheka; na yakuwa hilo likae naye katika amali yake, siku zote za maisha yake alizompa Mungu chini ya jua.

Hivyo mhubiri anatuambia tuhakikishe kwanza Bwana ameziridhia njia zetu. Kisha furaha ya maisha ifuate baada ya hapo, Ndio kiini cha hivyo vifungu. lakini ikiwa tutafurahia maisha, lakini Mungu yupo nyuma, hiyo inageuka na kuwa anasa na tujue mwisho wetu utakuwa ni upotevu.

Zaidi sana sehemu nyingine anasema heri, “Heri konzi moja pamoja na utulivu, Kuliko konzi mbili pamoja na taabu; na kujilisha upepo” Mhubiri 4:6  Maana yake ni kwamba ikiwa umejaliwa kimoja, lakini upo katika amani ni bora kuliko kuwa na vingi lakini katika masumbufu.

Bwana atusaidie, tuishi kwa hekima katika dunia yake aliyotupa. Pastahilipo furaha tufurahi, pastahilipo kujizuia tujizuie kwelikweli. Mambo yote yawe katika uwiano ndani ya Kristo.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

JE! NINAWEZA KUPOTEZA FURAHA YA WOKOVU?

Mithali 24:17 inamaana gani kusema Tengeneza kazi yako huko nje?

Furaha ni nini?

Mithali 14:4 ‘Zizi ni safi ambapo hapana ngombe;

IFAHAMU HUZUNI NA FURAHA YA MALAIKA.

“Humfukuza punda wake asiye baba”, nini maana ya mstari huu? (Ayubu 24:3)

Nini maana ya “mtakayoyafunga duniani, yatakuwa yamefungwa mbinguni”?

NINI MAANA YA KUWA MKRISTO?

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments