Nini maana ya kupwita-pwita? (Zaburi 38:10)

Nini maana ya kupwita-pwita? (Zaburi 38:10)

Jibu: Turejee,

Zaburi 38:10 “Moyo wangu unapwita-pwita, Nguvu zangu zimeniacha; Nuru ya macho yangu nayo imeniondoka”.

Kupwita-pwita maana yake, ni “kudunda kwa haraka”, hivyo hapo biblia iliposema “kuwa moyo wangu unapwita pwita”, maana yake ni kuwa “moyo wa mwandishi unaenda mbio” kutokana na mateso aliyokuwa anayapitia.

Mtu anayepitia katika hali ya mateso, kutoka kwa watu wabaya.. ni kawaida kuumia moyo, Tuwapo katika hali kama hiyo, biblia imetufundisha kuwa waombaji na kujinyenyekeza kwa Mungu ili Bwana aiponye mioyo yetu na kutuokoa na mikono ya watesi.

Zaburi 17:14 “Ee Bwana, kwa mkono wako uniokoe na watu, Watu wa dunia hii ambao fungu lao li katika maisha haya”.

Zaburi 59:1 “Ee Mungu wangu, uniponye na adui zangu, Uniinue juu yao wanaoshindana nami. 

2 Uniponye nao wafanyao maovu, Uniokoe na watu wa damu. 

3 Kwa maana wanaiotea nafsi yangu; Wenye nguvu wamenikusanyikia; Ee Bwana, si kwa kosa langu, Wala si kwa hatia yangu.

 4 Bila kosa langu huenda mbio, hujiweka tayari; Uamke uonane nami, na kutazama”.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa >> WHATSAPP-GROUP

Mada Nyinginezo:

Nitajuaje kuwa nimesamehewa dhambi zangu?

SALA YA UPONYAJI/MAOMBI YA UPONYAJI.

MWIMBIE BWANA ZABURI KATIKA NYAKATI ZA FURAHA.

BWANA UNIJULISHE MWISHO WANGU.

Mtima ni nini kibiblia?.

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments