Mtiririko wa vitabu vya biblia kwanini upo vile?

by Admin | 23 April 2023 08:46 pm04

SWALI: Kwanini vitabu vya biblia vipo katika mtiririko ule, na sio kinyume chake?

Ni vema kufahamu kuwa mtiririko wa kibiblia wa agano la kale na agano jipya, haukuwekwa na Mungu, kwamba kianze kitabu hiki kifuate hiki, kianze cha Mwanzo kisha kifuate cha Kutoka. Hapana bali ni utaratibu uliowekwa na wanadamu, ambao kimsingi unamaudhui mazuri, na uligawanya hivyo ili kumsaidia msomaji kufahamu vizuri, kuliko vingeorodheshwa  tu kila kimoja eneo lake, ingewia ngumu kwa msomaji anayependa kujifunza Biblia kuelewa kiwepesi.

Mtiririko ambao sisi tunaoutumia ni tofauti na mtiririko ambao Wayahudi wanautumia kwa vitabu vya agano la kale.

Kwa mfano mtiririko wetu (Ambao unajulikana kama mtiririko wa kiprotestanti), una vitabu 39 vya Agano la kale. Lakini mtitiriko wa Kiyahudi, una vitabu 24 kwa agano hilo hilo la kale,.

Vitabu vyetu ni kama vifuatavyo

Vitabu vya Sheria

  1. Mwanzo
  2. Kutoka
  3. Mambo ya Walawi
  4. Hesabu
  5. Kumbukumbu la Torati

Vitabu vya Historia

Vitabu vya Mashairi

  1. Ayubu
  2. Zaburi
  3. Mithali
  4. Mhubiri
  5. Wimbo ulio bora

Vitabu vya Manabii (Wakubwa)

Vitabu vya manabii (Wadogo)

Lakini utajiuliza kwanini biblia ya kiyahudi iwe na vitabu 24 na sio 39? Je vingine vimeondolewa? Jibu ni hapana, bali baadhi yao vilijumuishwa kama ni kitabu kimoja kwamfano.

> Vitabu viwili vya wafalme kwao ni kitabu kimoja.

> Vitabu viwili vya Mambo ya Nyakati kwao ni kitabu kimoja.

> Vitabu viwili vya Samweli kwao ni kitabu kimoja.

> Ezra na Nehemia vimeweka kama kitabu kimoja.

> Vitabu 12 vya Manabii wadogo kwao ni  kitabu kimoja.

Jumla yake ni vitabu 24 Badala ya 39.

Hivyo tukirudi katika biblia yetu, yenye vitabu 39 kwa agano la kale, Orodha ile haijawekwa kulingana na vipindi vilipoandikwa, bali kulingana na ‘asili ya vitabu’. Ndio hapo utaona hiyo migawanyo mikuu mitano (Yaani vitabu vya Sheria, vya historia, vya mashairi, vya Manabii wakubwa na wale wadogo).

Kutaja manabii wakubwa haimaanishi kuwa walikuwa na vyeo vya juu au walikuwa na nguvu zaidi ya wale wengine hapana, bali ni kutokana na wingi wa uandishi wao, yaani waliokuwa na uandishi mwingi waliwekwa katika kundi hilo la manabii wakubwa.

Tukirudi katika agano jipya.

Vipo vitabu 27, na vyenyewe pia havijaandikwa kulingana na wakati wa uandishi, japo havipishani sana na wakati wa uandishi.

Huu ndio mgawanyo wake.

Vitabu vya Injili

  1. Mathayo
  2. Marko
  3. Luka
  4. Yohana

Kitabu cha Historia

Nyaraka za Paulo

Nyaraka kwa wote

  1. Waebrania
  2. Yakobo
  3. 1Petro
  4. 2Petro
  5. 1Yohana
  6. 2Yohana
  7. 3Yohana
  8. Yuda

Unabii

Halikadhalika Nyaraka za Mtume Paulo ziliorodheshwa katika mpangilio ule kutoka na  urefu wa uandishi na sio umuhimu wa nyaraka Fulani zaidi ya nyingine, kwamfano utaona kitabu cha kwanza kwa urefu cha Mtume Paulo ni Warumi na ndio kilichowekwa cha kwanza. Vilevile kirefu zaidi ya vyote alivyoviandika kwa Watu, ni cha Timotheo ndicho kilichopangiliwa cha kwanza.

Lakini pamoja na kwamba havikuweka katika mpangalio wa nyakati za uandishi bado zinamtiririko mzuri unaelekeana na historia, kuanzia kitabu cha Mwanzo mpaka ufunuo.  Japo pia katika usomaji haimaanishi ufuate mtiririko huo, bali unaweza kuanza vyovyote upendavyo kwa jinsi Roho Mtakatifu atakavyokuongoza.Kwasababu hakuna sehemu yoyote katika maandiko tumewekewa mtiririko huo.

Pia zipo biblia nyingine mfano ile ya Kikatoliki yenye vitabu 73, ambayo kimsingi haijavuviwa na Roho wa Mungu kwani kuna baadhi ya vitabu vimeongezwa ambayo hukinzana na mafundisho ya msingi ya imani, na hivyo hatupaswi kuifuata. Biblia yetu ina vitabu 66 tu. Kama vilivyoorodheshwa hapo juu. Zaidi ya hivyo hutoka kwa Yule mwovu.

Bwana akubariki sana.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Tofauti kati ya maandiko na Neno ni ipi?

TABIA YA WAZI INAYOWATOFAUTISHA MANABII WA UONGO NA WALE WA UKWELI.

HISTORIA YA BIBLIA YA KING JAMES, INA FUNZO GANI KWETU?

Vitabu vya Deuterokanoni ni vya kiMungu?

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 1

FAHAMU MAISHA YA YESU KABLA YA HUDUMA.

Mimbari ni nini? Je tofauti kati ya Mimbari na madhabahu ni ipi?

Rudi nyumbani

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2023/04/23/mtiririko-wa-vitabu-vya-biblia-kwanini-upo-vile/