Title July 2022

Paulo alikuwa anamaanisha nini kusema “Mnatenda vema kuvumiliana naye” (2Wakorintho 11:4).

Jibu: Tusome,

2Wakorintho 11:4 “Maana yeye ajaye akihubiri Yesu mwingine ambaye sisi hatukumhubiri, au mkipokea roho nyingine msiyoipokea, au injili nyingine msiyoikubali, MNATENDA VEMA KUVUMILIANA NAYE!”

Ukiisoma sentensi hiyo kwa haraka ni rahisi kutafsiri kuwa Paulo anawafundisha watu kuwavumilia watu wanaohubiri injili nyingine, au kumhubiri Yesu Mwingine..Lakini sivyo, bali ni kinyume chake!.. alikuwa anawashangaa kwanini wanawavumilia hao wanaohubiri injili nyingine!.

Sasa sentensi hiyo ili ieleweke vizuri tunaweza kuiweka hivi .. “Maana yeye ajaye akihubiri Yesu mwingine ambaye sisi hatukumhubiri, au mkipokea roho nyingine msiyoipokea, au injili nyingine msiyoikubali, MNAVUMILIANA NAYE VIZURI SANA”..

Hivyo Neno “Kutenda vema” hapo jinsi lilivyotumika, limemaanisha “kufanya vizuri”..kwamfano badala ya kusema “mtu yule anaimba vizuri” pia ni sawa na kusema “mtu yule anatenda vema kuimba”.

Paulo alikuwa anawaonya hawa Wakorintho, kwa kuyavumilia mafundisho ya kipepo, na injili za kuzimu.. Kwamba hawapaswi kuyavumilia wala kuchukuliana nayo..

Na maonyo hayo yanatuhusu pia sisi kwamba hatupaswi kuwavumilia watu wanohubiri Injili nyingine, au yesu mwingine au roho mwingine.

Na hatuwavumilii kwa namna gani?

  • KWA KUTOENDELEA KUDUMU KATIKA KUISIKILIZA INJILI ZAO.

Tunapoijua kweli, hatuna budi kuachana na yale mafundisho ya uongo ya manabii wa uongo na Kama tumeshajua kuwa ULEVI ni dhambi, hatuna haja ya kuendelea kusikiliza mafundisho au kuwasikiliza wahubiri wanaofundisha kuwa Ulevi si dhambi!!…kwasababu injili yao ni injili nyingine, ambayo si ya YESU WA NAZARETI.

Tunapojua kuwa IBADA ZA SANAMU ni dhambi!, hatuna budi kuachana na mafundisho ya kipagani ya ibada za sanamu, yanaohubiriwa na wachungaji wa uongo, na maaskofu wa uongo, na vile vile kuacha kufuatilia mafundisho yao kwasababu wanahubiri roho nyingine tofauti na Roho Mtakatifu.

  • KWA KUWAONYA NA KUZIDHIHIRISHA KAZI ZAO HADHARANI KUWA NI MBOVU.

Tunapogundua kuwa yupo mtu au watu, wanafundisha kinyume na kweli, tena kwa makusudi, na huku wanajua kabisa wanachokifanya sio sawa..hapo hatupaswi kuivumilia injili yao.. badala yake kuupinga uharibifu wao hadharani..ili kusudi wasiendelee kuwapotosha wengine wasiojua..

Wagalatia 1:6 “Nastaajabu kwa kuwa mnamwacha upesi hivi yeye aliyewaita katika neema ya Kristo, na kugeukia INJILI YA NAMNA NYINGINE.

7 WALA SI NYINGINE; lakini wapo watu wawataabishao na kutaka KUIGEUZA INJILI YA KRISTO

8 Lakini ijapokuwa sisi au malaika wa mbinguni atawahubiri ninyi injili yo yote isipokuwa hiyo TULIYOWAHUBIRI, NA ALAANIWE.

9 Kama tulivyotangulia kusema, na sasa, nasema tena, mtu awaye yote akiwahubiri ninyi injili yo yote ISIPOKUWA HIYO MLIYOIPOKEA, NA ALAANIWE”.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

FANYA KAMA UONAVYO VEMA.

NI YESU YUPI UMEMPOKEA?, NI ROHO IPI UMEIPOKEA? NA INJILI IPI UMEIPOKEA?

Je Mungu ana njia ngapi za kuzungumza?

NI KWA NAMNA GANI SHETANI ANAIZUIA INJILI?

Kula uzao wa tumbo lako maana yake nini? (Kumbukumbu 28:53)

Rudi nyumbani

Print this post

Wana wa Asafu ni akina nani katika biblia?

Wingu la Mashahidi
Wingu la Mashahidi
Wana wa Asafu ni akina nani katika biblia?
/

Kabla ya kuwafahamu wana wa Asafu, ni vizuri kumfahamu Asafu mwenyewe alikuwa ni nani.

Asafu alikuwa ni mmoja wa walawi ambao, mfalme Daudi alimuweka  kama kiongozi wa mbele wa sifa, atakayesimama mbele ya sanduku la Mungu daima kumsifu Mungu. (Soma 1Nyakati 6:31-32, 39).

1 NYAKATI: MLANGO 16

1 Wakaliingiza sanduku la Mungu, na kuliweka katikati ya hema aliyoipiga Daudi kwa ajili yake; wakatoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani mbele za Mungu.

2 Na Daudi alipokwisha kuitoa sadaka ya kuteketezwa na sadaka za amani, akawabariki watu kwa jina la Bwana.

3 Kisha akawagawia kila mtu wa Israeli, waume kwa wake, kila mtu mkate wa ngano, na kipande cha nyama, na mkate wa zabibu.

4 Akawaagiza baadhi ya Walawi kwamba watumike mbele ya sanduku la Bwana, wamfanyie ukumbusho, na shukrani, na sifa, Bwana, Mungu wa Israeli;

5 Asafu mkuu wao, na wa pili wake Zekaria, na Yeieli, na Shemiramothi, na Yehieli, na Matithiya, na Eliabu, na Benaya, na Obed-edomu, na Yeieli, wenye vinanda na vinubi; naye Asafu mwenye kupiga matoazi;

Kulingana na maandiko, biblia inasema huyu Asafu hakuwa tu mwimbaji, bali Mwonaji pia,

2Nyakati 29:30 “Tena Hezekia mfalme na wakuu wakawaamuru Walawi, wamwimbie Bwana sifa kwa maneno ya Daudi, na ya Asafu mwonaji. Wakaimba sifa kwa furaha, wakainama vichwa, wakaabudu”.

Baadaye, uzao wake uliendeleza  nyayo zake, na wote wakawa waimbaji katika hekalu la Mungu lililokuja kujengwa baadaye, na hata baada ya ule uhamisho wa Babeli, waliporudi bado waliweza kuwekwa katika kazi hiyo hiyo ya Sifa..

Soma, Ezra 2:41 “Waimbaji; wana wa Asafu, mia moja ishirini na wanane”.,

Pia Nehemia 7:44

Halikadhalika kuna baadhi ya Zaburi zilijulikana kama Zaburi za Asafu,Ambazo ni Zaburi 50 na ya 73-83. (Baadhi ya tafsiri zinaonyesha hivyo). Hiyo ni kuonyesha kuwa Mungu alimtumia yeye na uzao wake kwa njia ya uimbaji, kutoa nabii ambazo zinatusaidia hadi sasa.

Lakini kwasasa wana wa Asafu ni akina nani? Na tunapata funzo gani?

Wana wa Asafu ni watu wote wanaotumikia madhabahuni pa Bwana katika huduma ya kumsifu na kumwimbia Mungu. Watu hawa wanatenda kazi kubwa inayompendeza Mungu na kwa kupitia wao, Mungu huwa anapitisha, jumbe zake nyingi, na nabii nyingi zinazookoa na kuponya watu kama ilivyokuwa kwa wana  wa Asafu, hii ikiwa na maana, kwamba wakitumika vema katika kazi yao, basi ni utumishi mkubwa sana, hata Zaidi ya huduma nyingine zote.

Lakini, watu hawa walijua kanuni ya kumwimbia Mungu, walimwimbia Mungu katika “uzuri wa utakatifu”, sawasawa 1Nyakati 16:29. Tofauti na sasa, waimbaji wengi, wamekuwa wasanii, wanageuza uimbaji wa injili kuwa Sanaa na sio wito na huduma ya Kristo Yesu.

Wanasahau kuwa huduma yao ndio ya kwanza kabisa inayomkaribia Mungu Zaidi ya nyingine zote,..Huduma ya Maserafi na Makerubi malaika watakatifu wasimamao mbele ya Mungu daima

Lakini kinyuma chake, Mwimbaji wa injili, utamkuta anakata mauno, anavaa vimini, anapamba uso kama Yezebeli, anaimba kwa staili za wasanii wa kidunia.. Twategemea vipi Mungu atasema au atawaponya, au atawafungua na watu wake kupitia uimbaji huo?, Haiwezekani..Inasikitisha kuona, kanisa la sasa, kundi kubwa la watu walioharibikiwa linatoka kwa wanakwaya na waimbaji.

Kumbuka Sababu  iliyowafanya wana wa Israeli,wapelekwe utumwani haikuwa tu kuabudu maashera hapana, ilikuwa pia ni hiyo ya unafki katika kumwimbia.

Amosi 6:5 “ninyi mnaoimba nyimbo za upuzi pamoja na sauti ya vinanda, na kujifanyizia vinanda vya namna nyingi, kama vile Daudi;”

Bwana anatuonya vikali, na sisi pia atatuadhibu vikali kama tutakuwa na tabia kama za wao,  anataka anapoimbiwa aimbiwe katika “uzuri wa utakatifu” (1Nyakati 16:29)..Maana yake ni kwamba wewe mwongoza sifa, wewe mwimbaji, wewe mpiga kinanda,wewe mpiga gitaa, uwe kielelezo kuanzia mavazi yako, usemi, hadi tabia, mbele za watu. Utakatifu ndio uwe leseni yako, ya kumwimbia Mungu.

Kama utashindwa utakatifu, ni heri uache tu, ukafanye kazi nyingine, kwasababu utakuwa unajizombea laana badala ya baraka.

Mahali Mungu anasifiwa na kuabudiwa ni kuwa makini sana.. wengine walipoteza Maisha walipojaribu kuvuruga utaratibu pindi Mungu anapokuwa anasifiwa (Soma 2Samweli 6:1-11 ), Vivyo hivyo na wewe mwimbishaji kanisani, usipokuwa siriazi na huduma yako, uwezekano wa kukutwa na hayo upo mkubwa sana.

Bwana anataka sote tuwe wana wa Asafu, ili atutumie kumtukuza yeye, Pamoja na kuzungumza na watu wake, ili aziponye roho za watu..

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

MAOMBI YA YABESI.

NI KITU GANI TUNAJIFUNZA KWA RISPA, BINTI AYA?

SOMO no.02 (BINTI WA YEFTHA).

Gongo na Fimbo ni nini? Na vinawezaje kumfariji mtu? (Zaburi 23:4).

Nini maana ya “Heri kuchagua jina jema kuliko mali nyingi”?

NI SALAMA ROHONI MWANGU Lyrics

WINGU KUBWA LA MASHAHIDI.

Mimi ni mweusi-mweusi, lakini ninao uzuri.

Rudi nyumbani

Print this post

Maongeo ni nini?(Wakolosai 2:19)

Maongeo ni maongezeko,

Kwa mfano Neno hilo utalisoma katika vifungu hivi;

 Kutoka 23:10 “Utapanda mbegu katika nchi yako muda wa miaka sita na kuyavuna maongeo yake;

11 lakini mwaka wa saba utaiacha nchi ipumzike na kutulia; hao maskini miongoni mwa watu wako wapate kula; na hicho watakachosaza wao, wapate kula wanyama wa kondeni. Utafanya vivyo katika shamba lako la mizabibu, na katika shamba lako la mizeituni”.

Soma pia Walawi 19:24

Maana yake ni kuwa kwa muda wa miaka sita Mungu aliwaruhusu wana wa Israeli wapande na kuvuna, hata na vile vinavyoongeza katika mavuno yao. Lakini ufikapo mwaka wa saba, hawakuruhusiwa kuvuna chochote bali waviache kwa ajili ya maskini na Wanyama wa kondeni.

Isaya 9:7 “Maongeo ya enzi yake na amani Hayatakuwa na mwisho kamwe, Katika kiti cha enzi cha Daudi na ufalme wake; Kuuthibitisha na kuutegemeza Kwa hukumu na kwa haki, Tangu sasa na hata milele. Wivu wa Bwana wa majeshi ndio utakaotenda hayo”.

Maana yake ni kuwa maongezeko ya enzi yake, na amani hayatakuwa na mwisho yataendelea kuongezeka na kuongezeka milele. Na anayezungumziwa hapo si mwingine Zaidi ya Yesu Kristo Bwana wetu.

Wakolosai 2:18 “Mtu asiwanyang’anye thawabu yenu, kwa kunyenyekea kwa mapenzi yake mwenyewe tu, na kuabudu malaika, akijitia katika maono yake na kujivuna bure, kwa akili zake za kimwili;

19 wala hakishiki Kichwa, ambacho kwa yeye mwili wote ukiruzukiwa na kuungamanishwa kwa viungo na mishipa, hukua kwa maongeo yatokayo kwa Mungu”.

Hapo anaposema, “hukua kwa maongeo yatokayo kwa Mungu”, ana maana kuwa, mwili huo(ambao ndio kanisa la Kristo) ukishakwisha kushikamanishwa Pamoja viungo vyote.. Basi hukua, kwa maongezeko (maongeo), yatokayo kwa Mungu..Sio maongezeko yatokayo kwa mwanadamu.

Hii ikiwa na maana hata sisi kama wakristo, tukishikama Pamoja na Kristo tukamfanya kuwa kichwa chetu, basi, tutakuwa katika ukuaji (maongezeko )unaotoka kwa Mungu mwenyewe..

Lakini kinyume chake ni kweli tukimkataa Kristo, kama kichwa cha kanisa, na kuwafanya wanadamu kuwa ndio vichwa vyetu, basi hatutakuwa na maongezo yoyote ya rohoni au mwilini, na hata kama tukiwa nayo, basi yatakuwa hayatokani na Mungu bali ibilisi.

Hivyo hatuna budi kumfanya Kristo kichwa cha kila kitu.. kwasababu ufalme wake unadumu milele. Lakini tukifanya tunajua kujenga ngome zetu au falme zetu, tufahamu kuwa taabu zetu zitakuwa ni bure mwisho wa siku.

Ukuaji wetu wa ndani na nje, unamtegemea Yesu Kristo tu, zaidi yake hakuna mwingine.

Sifa heshima na utukufu vimrudie yeye milele na milele daima.

Bwana atusaidie.

Shalom..

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Sadaka ya kinywaji ilikuwaje? Na inawakilisha nini?

Mkatale ni nini katika biblia? (Matendo 16:24)

SIFONGO NA SIKI NI NINI?

Pakanga ni nini?

Talanta ni nini katika biblia (Mathayo 25:14-30)

Santuri ni nini? (Danieli 3:5,10)

Bushuti ni nini?

Donda-Ndugu ni nini?

Pango la Makpela ni lipi, je lina umuhimu wowote kwetu?

Rudi nyumbani

Print this post

Sadaka ya kinywaji ilikuwaje? Na inawakilisha nini?.

Katika biblia (Agano la kale), kimiminika kilichokuwa kinatolewa sadaka ni “Divai” na si kitu kingine,

Walawi 23:13 “Na sadaka yake ya unga itakuwa sehemu za kumi mbili za efa za unga mwembamba uliochanganywa na mafuta, ni kafara iliyosongezwa kwa Bwana kwa moto kuwa harufu ya kupendeza; na SADAKA YAKE YA KINYWAJI ITAKUWA NI DIVAI, robo ya hini”.

Unaweza kuona pia sadaka hii ya Kinywaji ikitajwa katika kitabu cha Kutoka 29:40, Kutoka 30:9, na Walawi 23:18, Hesabu 6:15, Hesabu 15:6 na Hesabu 28:17..

Sasa swali linakuja kwanini IWE DIVAI na si kitu kingine?

Sasa Sadaka ya kinywaji (Divai) iliyokuwa inapelekwa katika madhabahu haikuwa kwa kazi ya Ulevi, bali kwa matumizi ya Nishati.

Katika sheria za Musa, Bwana aliagiza pia wana wa Israeli watoe sadaka ya kinywaji, ambayo ilikuwa ni DIVAI. Na divai hiyo ilipelekwa kwa kuhani, na kuhani aliingia nayo ndani ya hema, na kuitwaa sehemu ndogo ya ile Divai, na kisha kuimimina juu ya madhahabu Pamoja na unga mwembamba, na kuwasha moto juu yake.

Asili ya sadaka hii ni wapi?

Matoleo ya sadaka ya kinywaji yalianzia kwa Yakobo kipindi alipotokewa na Mungu kule Betheli, kama vile sadaka ya Zaka ilivyoanzia kwa Ibrahimu kipindi anakutana na Melkizedeki na hatimaye ikaja kuwa sheria kwa Israeli yote. Vivyo hivyo na sadaka ya kinywaji.

Mwanzo  35:9 “MUNGU AKAMTOKEA YAKOBO TENA, aliporudi kutoka Padan-aramu akambariki.

10 Mungu akamwambia, Jina lako ni Yakobo; hutaitwa tena Yakobo, lakini Israeli litakuwa jina lako. Akamwita jina lake, Israeli.

11 Mungu akamwambia, Mimi ni Mungu Mwenyezi, uzidi ukaongezeke. Taifa na kundi la mataifa watatoka kwako, na wafalme watatoka viunoni mwako.

12 Na nchi hii niliyowapa Ibrahimu na Isaka nitakupa wewe, na uzao wako baada yako nitawapa nchi hiyo.

13 Mungu akakwea juu kutoka kwake mahali hapo aliposema naye.

14 Yakobo akasimamisha nguzo mahali aliposema naye, nguzo ya mawe, AKAMIMINA JUU YAKE SADAKA YA KINYWAJI, AKAMIMINA MAFUTA JUU YAKE.

15 Yakobo akapaita mahali pale, Mungu aliposema naye, Betheli.”

Sasa Sadaka ya Kinywaji inawakilisha nini katika Agano jipya?

Sadaka ya kinywaji katika Agano jipya inawakilisha damu ya YESU, ambayo ilimwagika/kumiminwa kwaajili yetu, mara moja tu! (kumbuka damu ya Yesu, inafananishwa na Divai), Bwana Yesu alilisema hilo wazi..

Luka 22:19 “Akatwaa mkate, akashukuru, akaumega, akawapa, akisema, [Huu ndio mwili wangu unaotolewa kwa ajili yenu; fanyeni hivi kwa ukumbusho wangu.

20 Kikombe nacho vivyo hivyo baada ya kula; akisema, KIKOMBE HIKI NI AGANO JIPYA KATIKA DAMU YANGU, INAYOMWAGIKA KWA AJILI YENU”.

Umeona hapo! Kile kikombe (Divai) kilikuwa ni  Damu ya Yesu iliyotiririka na iliyomwagika pale Kalvari, na ni ufunuo wa Ile sadaka ya kinywaji ambayo ilikuwa inamiminwa juu ya madhabahu. Na pia ni ufunuo wa meza ya Bwana.

Bwana Yesu akubariki

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

Sadaka ya Amani ilikuwaje?

Sadaka ya kutikiswa ilikuwaje?

Nini maana ya.. “Utoapo sadaka mkono wako wa kuume usijue ufanyalo mkono wako wa kushoto”

NI NINI BWANA ANATAZAMIA KILA TUNAPOSHIRIKI MEZA YAKE.

BWANA alimaanisha nini kwenye mstari huu Marko 2:21″ Hakuna mtu ashonaye kiraka cha nguo mpya katika vazi kukuu?

Rudi nyumbani

Print this post

KWANINI KUWE NA UTAWALA WA MIAKA 1000

Biblia inatuonyesha baada ya tukio la unyakuo, ambapo watakatifu watakwenda mbinguni kwenye karamu ya mwana-kondoo kwa kipindi cha miaka saba, ..watarudi tena duniani wakiwa na Bwana Yesu ili kutawala naye kwa muda wa miaka 1000.

Sasa utajiuliza ni kwanini Bwana Yesu asiwe nao milele mbinguni bali arudi tena dunia kutawala nao. Makusudi ya Bwana ni yapi?

Sasa leo hatupo  kueleza kwa urefu, huo utawala utakujaje kujaje na wakati gani..ikiwa utapenda kupata somo lake kwa urefu basi fungua link hii >>> UTAWALA WA MIAKA 1000.

Lakini nataka tuone sababu za kuwepo kwa utawala huo…

Sababu zipo  mbili kuu

  1. Ni kwamba Yesu anataka kuwapa raha watu wake.

Raha hiyo inajulikana kama raha ya sabato..

Waebrania 4:9-11

[9]Basi, imesalia raha ya sabato kwa watu wa Mungu.

[10]Kwa maana yeye aliyeingia katika raha yake amestarehe mwenyewe katika kazi yake, kama vile Mungu alivyostarehe katika kazi zake.

[11]Basi, na tufanye bidii kuingia katika raha ile, ili kwamba mtu ye yote asije akaanguka kwa mfano uo huo wa kuasi.

Hichi ndicho kipindi ambacho Bwana atawarejeshea vyote watumwa wake walivyovipoteza kwa ajili yake walipokuwa hapa duniani  kwa kuwapa ufalme ulio bora wenye nguvu na wa kudumu. (Yoeli 2:25)

Watatawala kama wafalme na mabwana, na makuhani,..na Yesu Kristo mwenyewe akiwa kama Bwana wa Mabwana na Mfalme wa Wafalme.

Kipindi hicho dunia hii itarejeshwa na kuwa nzuri sana hata zaidi ya ilivyokuwa Edeni. Dunia yote itajawa na amani..kwasababu kipindi hicho ibilisi atakuwa amefungwa kwa muda wa miaka 1000,

Ikiwa wewe iliishi maisha ya kujikana na huu ulimwengu wa kitambo unaopita, basi kule utakuwa na nafasi kubwa sana kwa Yesu Kristo, tutakuwa na miili mipya ya utukufu isiyougua wala kuzeeka, utaburudishwa kwelikweli,

Na raha isiyo na kifani itatawala nyuso za watu wa Mungu, mtu ambaye ulionekana umerukwa na akili kwa kumtumikia kwako Mungu, binti ulionekana mshamba kwa kujisitiri kwako, Bwana atakupa heshima na faraja yako ya kumiliki.

Wote waliotaabika kwa ajili ya injili ya Kristo kwa namna moja au nyingine huo  ndio utakuwa wakati wa kuburudishwa na kuyafurahia maisha.. Ni lazima Bwana Yesu afanye hivi, ili kuwathibitishia watu wake kwamba hakuna chochote walichokipoteza walipokuwa hapa duniani walipomfuata yeye.

2.   Jambo la pili: Ni ili kuweka maadui zake wote chini.

ambapo wa mwisho atakuwa ni mauti.

1 Wakorintho 15:24-26

[24]Hapo ndipo mwisho, atakapompa Mungu Baba ufalme wake; atakapobatilisha utawala wote, na mamlaka yote, na nguvu.

[25]Maana sharti amiliki yeye, hata awaweke maadui wake wote chini ya miguu yake.

[26]Adui wa mwisho atakayebatilishwa ni mauti.

Kumbuka hata katika utawala ule watu watakuwa wanaendelea kufa, wale ambao walizaliwa humo..lakini sisi hatutakufa kwasababu tutakuwa na miili ya utukufu tuliyotoka nayo mbinguni.

Hivyo Bwana Yesu atadhibiti maadui zake waliosalia (wa rohoni) na wa mwisho wao atakuwa ni mauti,

Kwasasa, bado maadui baadhi wa Bwana Yesu hawajadhibitiwa, na ndio maana bado utaona watu wanakufa, lakini mambo hayo yote, atayamaliza ndani ya huo utawala wa amani wa miaka 1000.

Hivyo mpaka utalawa unakwisha..mambo yote mabaya yatakuwa yamekwisha kabisa kabisa.

Na baada ya hapo sasa ndio inakija mbingu mpya na nchi mpya..huko hakutakuwa na kilio wala mateso, wala huzuni, wala mauti, kwasababu tayari vilishakomeshwa na Yesu Kristo vyote katika utawala ule.

Na ile Yerusalemu itakushuka sasa kutoka mbinguni, ambapo Mungu kwa mara ya kwanza atafanya maskani pamoja na wanadamu.(Ufunuo 21&22)

Yaani kwa ufupi ni kwamba Mungu atahamishia makao yake hapa..

Uzuri na mambo yaliyopo huko..biblia inasema jicho halijawahi kuona wala sikio kusikia,

Jua na mwezi havitakuwepo..ulimwengu huu utageuzwa na kuwa sehemu ya tofauti kabisa..

Lakini ikiwa wewe upo nje ya wokovu, unayo hasara ya mambo mengi, ya kwanza ni karamu ya mwana-kondoo mbinguni, ya pili ni utawala wa miaka 1000 na mwisho mbingu mpya na nchi mpya.

Hivyo itakufaidia nini uupate ulimwengu mzima kisha upoteze roho yako.

Kumbuka kwa jinsi hali ilivyo hichi ni kizazi kitakachoshuhudia tukio la unyakuo, hatuweki siku lakini kwa dalili zinavyoonyesha hatuna muda mrefu Kristo anarudi..labda pengine leo usiku.

Hivyo tuanze kuelekeza mawazo yetu mbinguni, tuachane na mambo haya ya kitambo ya ulimwengu. Yesu ameshatuandalia makao, ambayo atakuja kutuburudisha kwa kipindi cha miaka 1000. Tutubu dhambi zetu kwa kumaanisha kabisa kuziacha. Na Bwana atatupokea na kutusamehe.

Bwana akubariki

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

IMESALIA RAHA YA SABATO KWA WATU WA MUNGU.

UMUHIMU WA KUBATIZWA.

Kiyama ni nini?

JE KANISA LITAPITIA DHIKI KUU?

MAOMBOLEZO YA HADADRIMONI.

USICHELEWE KUMPAKA BWANA MARHAMU!

Kupiga ramli ni nini katika biblia?

NI SALAMA ROHONI MWANGU Lyrics

Rudi nyumbani

Print this post

Tofuati kati ya kifo na mauti ni ipi?

Kifo ni ile hali ya uhai kutoka ndani ya kiumbe hai chochote. Kifo kinaweza kumtokea mtu, mnyama, bakteria, kirusi, mmea, jani n.k. Vyote hivi maadamu vina uhai ndani yao, vinapotokwa tu huo  uhai basi vinakuwa vimekufa.

Lakini Mauti ni nini?

Mauti ni kile kile kifo, isipokuwa ni mahususi tu kwa mwanadamu.. Huwezi kusema “mti” umekumbwa na mauti, au “mbwa” amepatwa na mauti.. Bali utasema, mti umekufa au mbwa amekufa. Ni mwanadamu tu ndiye anayekumbwa na mauti.

Lakini kwanini Kifo kitofautishwe na mauti?

Ni kuonyesha uzito wa hali hiyo kwa mwanadamu.. Kwamfano “Kilio” kinaweza kutokea kwa mtu yeyote yule, iwe ni mtoto au mtu mzima Lakini kikiwa kwa mtu mzima, hakiwezi kuchukuliwa kama kile cha mtoto, kwasababu kama vile wasemavyo wanajamii, “ukiona mtu mzima analia basi ujue kuna jambo”

Maana yake ni kuwa hadi mtu mzima anatoa machozi, ujue hayajaja bure bure tu, bali yana sababu nyuma yake, na matokeo mbele yake, kwasababu si desturi ya mtu mzima kulia. Nyuma yake utagundua aidha kuna msiba, au magonjwa, au kuumizwa moyo kusikoelezeka, kusalitiwa au kupoteza mali zake nyingi, au vitu, n.k.. Lakini mtoto mdogo anaweza akalia kwasababu zisizokuwa na maana au msingi wowote.

Vivyo hivyo katika kifo na mauti ni tendo lilelile..kuondoka kwa uhai.. isipokuwa linapokuja kwa mtu, linakuwa na uzito wa namna yake, kwasababu mwanadamu hakuumbiwa kifo, halidhalika kwa sifa yake na heshima na akili alizopewa na Mungu, jambo kama hilo ni anguko kubwa sana kwake..Mauti ni pigo kwa mwanadamu.

Sababu ya mauti kumpata mtu ni nini?

Ni dhambi..

Warumi 6:23 “Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti; bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu”.

Sisi wanadamu tulipoasi, adhabu hii ya mauti ilitukumba.. Hilo ni pigo kubwa sana kwetu, tofauti na Wanyama, wenyewe hawajui chochote, wala hawaelewi, kufa na kupotea kwao ni kitu cha kawaida, lakini sisi tunajua kwamba ipo siku uhai utatutoka..

Lakini heri ingekuwa ni kifo cha miili yetu tu halafu basi.. Lakini Huko mbeleni pia baada ya kifo, kuna adhabu ya kifo cha roho. Hiyo ndio inayoitwa mauti ya pili..Ambazo roho hizi zitamalizwa kabisa katika lile ziwa la moto..Hapo ndipo utaona, tofauti ya kifo cha mnyama, na kile cha mwanadamu.

Ndugu, ukikumbwa na mauti sasa, toa yale mawazo kwamba utakuwa kama mnyama tu.. Hapana, ukifa katika dhambi, utanyoshea moja kwa moja hadi jehanamu, ukisubiri siku ya ufufuo ifike uhukumiwe kisha utupwe katika ziwa la moto milele na milele.

Lakini Habari njema ni kwamba, Bwana Yesu alikuja kukomesha mauti kwa mwanadamu, na kwamba yeyote amwaminiye yeye, anakuwa amevuta kutoka katika mauti na kuingia kwenye uzima..

Yohana 5:24 “Amin, amin, nawaambia, Yeye alisikiaye neno langu na kumwamini yeye aliyenipeleka yuna uzima wa milele; wala haingii hukumuni, bali amepita kutoka mautini kuingia uzimani”.

Umeona? Yaani Yesu akikuoa mauti inakuwa haina nguvu tena ndani yake..

Hivyo ndugu, wasubiri nini, leo usimkaribishe Yesu moyoni mwako.? Kumbuka hakuna mtu mwenye garantii ya kuishi milele. Au anayeijua kesho yake kama atakuwa duniani au la. Ukifa katika dhambi ni nani atakayekuponya na mauti ya roho yako? Huko utakapokwenda utakuwa mgeni wa nani. Kama huna uhakika, unajisikiaje kubaki katika hali hiyo?

Lakini nafasi sasa unayo, Ikiwa upo tayari kufanya hivyo leo, yaani kuongozwa sala ya toba ya kumpokea Yesu.. Basi fungua hapa kwa ajili ya mwongozo huo >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Hivyo kwa kuhitimisha ni kuwa kifo kinampata kiumbe hai chochote, lakini mauti ni mahususi kwa mwanadamu, kwasababu yenyewe inabeba maana kubwa zaidi ya kifo cha kutoka uhai tu. Mauti imebeba uchungu, majuto, masononeko, hukumu, nyuma yake, jambo ambalo kifo hakina.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

jiunge kwenye group la whatsapp la mafundisho ya kila siku kwa kubofya hapa >>> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

Jehanamu ni nini?

Kuna hukumu za aina ngapi?

Roho, Nafsi, na Mwili vina utofauti gani?

NINI KINATOKEA BAADA YA KIFO?

UNYAKUO.

DHAMBI YA MAUTI

BALI WANA WA UFALME WATATUPWA NJE!.

Rudi nyumbani

Print this post