Kiyama ni nini?

Kiyama ni nini?

Kiyama au kiama..maana yake ni ‘siku ya ufufuko’

Neno hilo linapatikana sehemu kadha wa kadha katika biblia. Kwamfano hivi ni baadhi ya vifungu ambavyo utakatana nalo;

Mathayo 22:23-28

[23] Siku ile Masadukayo, watu wasemao ya kwamba hakuna kiyama, wakamwendea, wakamwuliza,

[24]wakisema, Mwalimu, Musa alisema, Mtu akifa, akiwa hana watoto, ndugu yake na amwoe yule mkewe, ili ampatie nduguye mzao.

[25]Basi, kwetu kulikuwa na ndugu saba; wa kwanza akaoa, akafariki, na kwa kuwa hana mzao, akamwachia nduguye mke wake.

[26]Vivyo hivyo wa pili naye, na wa tatu, hata wote saba.

[27]Mwisho wa wote yule mwanamke akafa naye.

[28]Basi, katika kiyama, atakuwa mke wa yupi katika wale saba? Maana wote walikuwa naye.

Hapo ni mafarisayo  walitaka kujua kutoka kwa Yesu siku ya ufufuo wa wafu, mambo ya ndoa yatakuwaje.?

Soma pia..Wafilipi 3:10-11

[10]ili nimjue yeye, na uweza wa kufufuka kwake, na ushirika wa mateso yake, nikifananishwa na kufa kwake;

[11]ili nipate kwa njia yo yote kuifikia kiyama ya wafu.

Akimaanisha afikie siku ya ufufuko wa wafu.

Neno hilo utalisoma pia katika vifungu hivi;

2 Timotheo 2:17-18,22

[17]na neno lao litaenea kama donda-ndugu. Miongoni mwa hao wamo Himenayo na Fileto,

[18]walioikosa ile kweli, wakisema ya kwamba kiyama imekwisha kuwapo, hata kuipindua imani ya watu kadha wa kadha.

Hivyo na sisi pia hatuna budi kuyaelekeza mawazo yetu katika ufufuo wa wafu..Tumaini hilo ni lazima liwepo ndani yetu. Na ufufuo huo utakuja siku ile ya UNYAKUO ambapo parapanda italia, kisha wafu wote waliokuwa makaburini waliompokea Kristo, watafufuliwa na  moja kwa moja wataungana na sisi tuliohai kisha kwa pamoja tutapaa kumlaki Bwana Yesu mawinguni.

Swali la kujiuliza. Je, tumejipangaje kwa ajili ya siku hiyo ya kiyama? Je matendo yetu wanastahili kukubaliwa?

Majibu sote tunayo.

Tukumbuke kuwa Siku ya kiyama ipo karibuni sana.

Shalom

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

NINI KINATOKEA BAADA YA KIFO?

NA JINA LAKE AITWA, NENO LA MUNGU.

Je mtu akifa anakuwa hana dhambi tena?

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
1 Comment
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Jonel
Jonel
1 year ago

Mungu, nipr moyo wa Toba.