Mwerezi ni nini?

Mwerezi ni nini?

Mwerezi ni aina ya mti uliokuwa unapatikana maeneno ya nchi ya Lebanoni, Ulikuwa unastawi pia sehemu mbalimbali za dunia, lakini ulistawi zaidi katika nchi ya Lebanoni, iliyopo kaskazini mwa nchi ya Israeli.

Aina hii ya mti ilitumika kwa matumizi mengi, kutokakana ubora wake na uimara wake ukulinganisha na aina nyingine ya miti. Mti huu wa Mwerezi  ulikuwa ni mgumu na usiooza kirahisi.

Nchi ya Lebanoni, ilijipatia utajiri kutokana na biashara ya miti hii, ambapo Mataifa mengi duniani kama Misri, Ashuru, Babeli na Israeli ilinunua miti hii kutoka huko Lebanoni, kwaajili ya matumizi mbalimbali ikiwemo ya ujenzi.

Mfalme Daudi alitumia miti hii ya Mierezi kutoka Lebanoni kuijenga nyumba yake.

2Samweli 5:11 “Kisha Hiramu, mfalme wa Tiro, akatuma wajumbe kwa Daudi, AKAMPELEKEA NA MIEREZI, NA MASEREMALA, NA WAASHI; NAO WAKAMJENGEA DAUDI NYUMBA”.

2Samweli 7:2 “mfalme akamwambia Nathani, nabii, Angalia sasa, mimi ninakaa katika NYUMBA YA MIEREZI, bali sanduku la Mungu linakaa ndani ya mapazia.”

Lakini pia Nyumba ya Mungu ambayo ilikuja kujengwa na Sulemani, Mwana wa Daudi, ilitengenezwa pia kwa Mierezi mingi kutoka Lebanoni.

1Wafalme 5:5 “Nami, tazama, nakusudia kujenga nyumba kwa jina la Bwana, Mungu wangu, kama Bwana alivyomwambia Daudi baba yangu, akisema, Mwana wako, nitakayemweka katika kiti chake cha enzi mahali pako, ndiye atakayeijenga nyumba kwa jina langu.

6 BASI UAMURU WANIKATIE MIEREZI YA LEBANONI; na watumishi wangu watafuatana na watumishi wako; na ujira wa watumishi wako nitakupa kama utakavyosema; kwa kuwa wajua ya kwamba hakuna kwetu mtu ajuaye kukata miti kama Wasidoni”.

Na hata baada ya Mfalme Nebukadneza kuliharibu hekalu hilo la Sulemani, hekalu la pili lilipokuja kujengwa na wakina Zerubabeli, lilijengwa sehemu kwa miti hiyo ya Mierezi.

Ezra 3:6 “Tangu siku ya kwanza ya mwezi wa saba walianza kumtolea Bwana sadaka za kuteketezwa, lakini msingi wa hekalu la Bwana ulikuwa haujawekwa bado.

7 Tena waliwapa waashi na maseremala fedha; wakawapa watu wa Sidoni, na watu wa Tiro, chakula, na vinywaji, na mafuta, ili walete MIEREZI KUTOKA LEBANONI mpaka Yafa kwa njia ya bahari, kwa kadiri walivyopewa ruhusa na Koreshi, mfalme wa Uajemi”.

Hivyo Mwerezi katika biblia imetumika kama ishara ya UTAJIRI. Kama vile DHAHABU.

Tunaona vitu vikuu viwili vilivyotajwa sana katika ujenzi wa nyumba ya Mungu ni MWEREZI pamoja na DHAHABU.  Kutokana na uthamani wa vitu hivyo.

Na kama Mti wa Mwerezi ulivyojipatia sifa hivyo, Bwana Mungu anasema walio Haki wote watasitawi kama Mwerezi.

Zaburi 92:12 “Mwenye haki atasitawi kama mtende, Atakua kama MWEREZI WA LEBANONI.

13 Waliopandwa katika nyumba ya Bwana Watasitawi katika nyua za Mungu wetu.

14 Watazaa matunda hadi wakati wa uzee, Watajaa utomvu, watakuwa na ubichi.

15 Watangaze ya kuwa Bwana ni mwenye adili, Mwamba wangu, ndani yake hamna udhalimu”.

Je! Wewe ni mwenye HAKI?

Kumbuka mwenye haki sio mtu anayesema anafanya mema huku yupo nje ya Kristo, hiyo sio tafsiri ya mwenye haki. Bali tafsiri ya mwenye haki ni mtu Yule, aliyempokea Yesu, na kubatizwa na kupokea kipawa cha Roho Mtakatifu, huyo ndiye anayehesabiwa haki kwa IMANI HIYO ya kumwamini Yesu. Mwingine yeyote ambaye hamwamini Bwana Yesu, na kujitumainia katika mambo yake anayoyafanya anayoamini kuwa ni mema, anakuwa bado si mwenye haki mbele za Mungu.

Lakini wote waliompokea Yesu, watasitawi na kuwa na heshima kama miti ya Mierezi.

Bwana atubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

WALA MSIUANGALIE MWILI, HATA KUWASHA TAMAA ZAKE.

Biblia inamaanisha nini inaposema “Mwenye haki huufikiri uhai wa mnyama wake”?

HUYU MELKIZEDEKI NI NANI?

Kwanini Bwana alirejea Tiro na Sidoni kwa mfano wa Sodoma?

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments