Jambo hilo hilo linajirudia leo hii, kwanini wanaojiita wakristo wengi hawataenda mbinguni? Sababu ni ile ile, wanajua historia yote ya Bwana Yesu na biblia yote, wanajua mwanzo wote wa ukristo na utakavyokuwa mwisho wake, lakini bado ni wakoma wa rohoni, bado ni wajane wa rohoni, wasiotaka msaada,.. Wanapoletewa habari ya wokovu, na kuhubiriwa watubu dhambi, na waponywe nafsi zao, wanajiona hawawezi kuongezewa kitu kingine cha ziada, sababu tu wao wamezaliwa katika ukristo, na wamepitia mafundisho yote ya biblia na vyuo vyote vya biblia, lakini ndani yao wanapinga maneno ya neema ya Kristo yahusuyo wokovu, utakuta ni mkristo lakini ni mlevi, ni mkristo lakini ni mzinzi, ni mkristo lakini ni msengenyaji, ni mkristo lakini ni mtazamaji wa pornography na mfanyaji wa mustarbation, ni msagaji, ni mvaaji wa vimini, ni mtukanaji, mtu asiyesamehe n.k. Na akiambiwa habari za kutubu dhambi na kujazwa Roho atasema naifahamu biblia, nilishaenda katika mafundisho hayo zamani, huo ni ulokole tu, atakwambia hayo yote chimbuko lake ni hili au hili n.k. hivyo anakuona huna chochote cha kumwongezea yeye…