Ni nani aliyemshawishi Daudi akawahesabu Israeli? Ni Mungu au shetani?

Ni nani aliyemshawishi Daudi akawahesabu Israeli? Ni Mungu au shetani?

Katika 2Samweli 24:1 tunaona maandiko yanasema ni Mungu ndiye aliyemtia Daudi nia, lakini tukirudi katika 1Nyakati 21:1, tunaona maandiko yanasema ni shetani.


Tuanze na 2Samweli 24:1..

2Samweli 24:1 “Tena hasira ya BWANA IKAWAKA JUU YA ISRAELI, AKAMTIA DAUDI NIA JUU YAO, AKISEMA, NENDA, UKAWAHESABU ISRAELI NA YUDA”.

Tusome pia…

1Nyakati 21:1 “TENA SHETANI AKASIMAMA JUU YA ISRAELI, AKAMSHAWISHI DAUDI KUWAHESABU ISRAELI.

2 Basi Daudi akamwambia Yoabu, na wakuu wa watu, Nendeni kawahesabu Israeli toka Beer-sheba mpaka Dani; mkanipashe habari, nipate kujua jumla yao”.

Hapo tukiangalia tunaona ni kweli sentensi mbili zinajichanganya..lakini je! Ni kweli zinajichanganya?

Jibu ni la! Hazijichanganyi..fahamu zetu ndizo zinazojichanganya..lakini biblia siku zote itabaki kuwa Neno la Mungu, lililohakikiwa na Roho Mtakatifu na lisiloweza kukosewa.

Ili tuelewe vizuri maana ya mistari hiyo, hebu tutafakari katika mfano wa kawaida wa kimaisha.

Watu wawili tofauti wameshuhudia ajali barabarani.. Mmoja akatoa ushuhuda akasema “Yule mtu alipokuwa anavuka gari lilimgonga na halikusimama”…Na mwingine akatoa ushuhuda akasema.. “Yule mtu alipokuwa anavuka, Yule dereva alimgonga na hakusimama..akakimbia ”. Je! Katika hao mashuhuda wawili kuna ambaye hayupo sahihi?.. Bila shaka wote wapo sahihi!!.. aliyesema “gari limemgonga” na aliyesema “dereva kamgonga”..wote wapo sahihi..

Kwasababu Yule aliyesema gari limemgonga, hajahusisha dereva aliyekuwa analiendesha lile gari, kadhalika Yule aliyesema ni dereva kamgonga hajahusisha kifaa kilichotumika kumgongea Yule mvuka barabara, ambacho ni gari.

Kadhalika katika mistari hiyo hapo juu..Tunaona mmoja kamtaja kuwa ni Bwana Mungu ndiye aliyemtia nia Daudi, bila kuhusisha chombo alichokitumia (yaani shetani)..kadhalika mwandishi mwingine wa kitabu cha Mambo ya Nyakati, kakitaja chombo tu (yaani shetani)na bila kumhusisha aliyekitumia hicho chombo (yaani Mungu).

Kwahiyo kwa ujumla aliyeleta hayo yote ni Mungu, na shetani katumika tu kama chombo!..na hiyo yote ni kwasababu ya makosa ya Israeli. Na pia ilikuwepo sababu kwanini iwe ni kosa Daudi kwenda kuwahesabu Israeli kama utapenda kujua zaidi juu ya hilo, unaweza kufungua hapa >>>> USIZITEGEMEE NGUVU ZAKO

Kwahiyo tunachoweza kujifunza ni kwamba, Mungu anaweza kutumia chombo chochote kile kutimiza kusudi lake.

Kwamfano utaona Mungu alipotaka kuwatoa Israeli kuwapeleka Babeli, hakushuka yeye mwenyewe na kuwaondoa, bali utaona alimtumia Nebukadneza kama chombo chake cha kufanya hiyo kazi.

Kadhalika Bwana Mungu anaweza kumtumia shetani kutimiza kusudi lake.

Kwamfano mtu anayemkataa Mungu kwa makusudi, anaweza kuruhusu shetani ayaharibu maisha yake, mpaka atakapofikia hatua ya kujitambua.. Na hata wakati mwingine kama mtu huyo kama bado anazidi kushupaza shingo, basi Mungu anaweza kumweka chini milki ya shetani moja kwa moja.

Hivyo hatuna budi kukaa katika neema ya Mungu, na kuishi maisha yampendezayo, ili tusimkasirishe Bwana Mungu wetu aliyetuumba. Kwasababu maandiko yanasema.. yeye mwenyewe hapendi kumtesa mwadamu wala kumhuzunisha.. (Maombolezo 3:34).

Hivyo kwa hitimisho ni kwamba kama bado hujampokea Yesu, fahamu kuwa hizi ni siku za mwisho. Na Kristo yupo mlangoni kurudi, unyakuo wa kanisa ni wakati wowote. Je akija leo na kukukuta katika hali hiyo ya dhambi, utakuwa mgeni wa nani?

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

Ni miaka mingapi ya njaa Daudi aliyoambiwa achague? Ni miaka 7 au miaka 3?

Ni miaka mingapi ya njaa Daudi aliyoambiwa achague? Ni miaka 7 au miaka 3?

KUOTA UNAENDESHA GARI.

KUOTA NYOKA.

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments